settings icon
share icon
Swali

Kuna mtu yeyote aliyemwona Mungu?”

Jibu


Biblia inatuambia kwamba hakuna mtu aliyewahi kumuona Mungu (Yohana 1:18) ila Bwana Yesu Kristo pekee. Katika Kutoka 33:20, Mungu anatangaza, “Huwezi kuuona uso wangu, kwa sababu hakuna mtu anaweza kuniona na aishi. “Maandiko haya yanaonekana kinyume na maandiko mengine ambayo yanaelezea watu mbalimbali “kuwa wamemuona” Mungu. Kwa mfano, Kutoka 33:11 inaeleza Musa akizungumza na Mungu “uso kwa uso.” Ni jinsi gani Musa angeweza kuongea na Mungu “uso kwa uso” kama hakuna mtu anaweza kuuona uso wa Mungu na aishi? Katika tukio hili, maneno “uso kwa uso” ni takwimu ya hotuba kuonyesha walikuwa katika ushirika wa karibu sana. Mungu na Musa walikuwa wakizungumza wao wawili vile binadamu huwa na mazungumzo ya karibu.

Katika kitabu cha Mwanzo 32:30, Yakobo alimuona Mungu akionekana kama malaika; hakuweza kweli kumwona Mungu mwenyewe. Wazazi wa Samsoni walishikwa na hofu wakati waligundua kuwa wamemuona Mungu (Waamuzi 13:22), lakini walimwona kwa mfano wa malaika. Yesu alikuwa Mungu katika mwili (Yohana 1:1, 14) hivyo wakati watu kulimwona, walikuwa wamemwona Mungu. Kwa wakati huo, naam, Mungu anaweza “kuonekana” na watu wengi “wamemuona” Mungu. Wakati huo huo, hakuna mtu aliyemwona Mungu wazi katika utukufu wake wote. Katika hali yetu ya kuanguka kwa binadamu, kama Mungu mwenyewe angejifunua kwetu kikamilifu, basi tungemezwa na kuharibiwa. Kwa hivyo, Mungu hujihijabu mwenyewe na kuonekana katika aina ambayo tunaweza “kumwona” yeye. Ingawa hivyo, hii ni tofauti na kumuona Mungu kwa utukufu wake wote na utakatifu. Watu wameona maono ya Mungu, picha ya Mungu, na vile Mungu anakaa, lakini hakuna mtu aliyepata kumwona Mungu kwa ukamilifu wake wote (Kutoka 33:20).

English



Rudi kwa ukurasa wa nyumbani wa Kiswahili

Kuna mtu yeyote aliyemwona Mungu?”
Shiriki ukurasa huu: Facebook icon Twitter icon Pinterest icon Email icon
© Copyright Got Questions Ministries