settings icon
share icon
Swali

Kunayo kitu kama ukweli kamili/Ukweli wa watu wote?

Jibu


Ili tuelewe maana ya ukweli kamili, lazima tuanze kwa kuelezea ukweli. Ukweli, kulingana na kamusi, ni “kupatana na hoja au uakikisho; kauli ambayo umethibitishwa, ambao unastahili kukubaliwa kuwa kweli.” Watu wengine watasema kuwa hakuna ukweli halisi, ni mitazamo na maoni. Wengine watapinga kuwa lazima kuwa na ukweli au uhalisi.

Mtazamo mmoja wasema kuwa hakuna ukamili ambao waelezea uhalisi. Wale wanaoshikilia mtazamo huu wanaamini kuwa kila kitu kimehusiana na kitu kingine, kwa hivyo hakutakuwa na uhalisi kamili. Kwa sababu ya hiyo, hamna maadili halisi, hamna mamlaka ya kuamua kama tendo ni la kujenga au kupomoa, zuri au baya. Mtazamo huu waelekeza kwa “maadili ya hali” imani kuwa chenye ni bora au baya limehusiana na hali. Hakuna kweli na baya; kwa hiyvo cho chote kinahisika kuonekana kizuri au kibaya kwa wakati na katika hali hiyo kiko sawa. Hata hivyo, maadili ya hali, zaelekeza kwa dhahania, “cho chote unahisi ni kizuri” kimawazo na kimaisha, ambacho kiko na matokeo ya kudhuru katika jamii na mtu binafsi. Hii jamii ya kisasa ambayo yakubali maadili yote, imani, njia ya kuishi na ukweli chadai kuwa zote ziko sawa.

Mtazamo mwingine washikilia kuwa kweli kunayo uhalisi kamili na vitimisho ambavyo vyafafanua chenye ni kweli na chenye si kweli. kwa hivyo, matendo yanaweza kuamuliwa kuwa zuri au baya kulingana na vile yamechangia kwa mizani halisi. Ikiwa hakuna uhalisi, ukweli, mfurugano. Chukua sheria ya mvutano, kwa mfano. Kama hatuko kwa uhalisi, hatungekuwa na uhakika kuwa tungesimama au kukaa katika sehemu moja hadi tuamue kusonga. Sheria za sayansi na fisikia sitakuwa sa muhimu, sheria ya biashara haitawezekana. Hayo yatakuwa makosa ya aina gani! Nashukuru, mbili jumlisha mbili ni nne. Kuna ukweli halisi na unaweza patikana na kueleweka.

Kusema kauli kuwa hakuna ukweli halisi sio kuwa na mantiki. Bali, hii leo, watu wengi wanalikubali ule usawa wa kitamaduni ambo wakana aina yo yote ya ukweli halisi. Swali zuri la kuuliza watu wanaosema, “Hakuna ukweli halisi” ni hili: “Uko na uhakika kabisa kwa hayo?” Ikiwa watasema “naam,” watakuwa wemefanya kauli halisi- ambayo yenyewe yamaanisha kuwa kuna uhalisi. Wanasema kwamba hoja kwamba hakuna ukweli halisi ndio mmoja na ukweli halisi peke.

Kando na shida ya kujichanganya, kunayo aina nyingi ya shida ya mantiki pai, ambazo mtu lazima aziepuke ili aamini kuwa hakuna uhalisi ua ukweli wa kiulimwengu. Moja ni kuwa wanadamu wote wako na elimu duni na mawazo yaliyo na mwisho na, kwa hivyo hawezi kimantiki kufanya uhalisi uwe kauli ya kutojenga. Mtu hawesi sema kimantiki kuwa, “Hakuna Mungu” (ingawa wengi wafanya hivyo), kwa sababu, ili usema kauli kama hiyo, anahitajika kuwa na elimu halisi ya ulimwengu woter kutoka mwanzo hai mwishi. Kwa kuwa hiyo haiwezekani, chenye mtu yeyote anaweza sema kimantiki ni “kwa elimu hii duni niko nayo, ninaamini kuwa kuna Mungu.”

Shida nyingine ya kataa ya ukweli halisi/ukweli wa kiulimwengu ni kuwa yakosa kuishi kufikia kiwango kile tunacho jua kuwa kweli katika akili zetu wenye, uzoefu wetu, na chenye tunaona katika ulimwengu. Ikiwa hakuna mambo mengi kama ukweli halisi, basi hakuna kitu hasa ni kizuri au kibaya kuhusu kitu cho chote. Chenye kinaweza kuwa “sawa” kwako haimanishi kuwa ni “sawa” kwangu. Huku ikiwa katika juu juu ikiwa aina hii ya ulegevu yaonekana kusihi, chenye inamaanisha ni kuwa kila mtu anajitengenezea sheria zake za kuishi na anafanya chenye anafikiri ni kizuri. Hakika mtu mmoja hisia zake za kweli hivi karibuni zitahitilafiana na za mwingine. Chenye hufanyika kama ni “kweli” kangu kupuuza taa za polisi barabarani, hata kama kama ziko nyekundu? Nitahatarisha maisha ya wengi. Au ninaweza kufikiri kuwa ni vizuri kuiba kutoka kwako, na unaweza kufikiri kuwa si vizuri. Waziwazi, mizani yetu ya zuri na baya zimehitilafiana. Ikiwa hakuna ukweli halisi, hakina mizani ya zuri na baya lenye tumewejibikia, basi kamwe hatutakuwa na uhakikia wa kitu cho chote. Watu watakuwa huru kufanya cho chote watakacho- uuaji, ubakaji, wizi, uongo na ujanja, na kadhalika. Na hakuna mtu anayeweza sema mambo haya ni maovu. Hakutakuwa na serikali, hakuna sheria, na hakuna haki, kwa sababu mtu hawezi sema kuwa wengi wa watu wako na haki kutengeza na kutekeleza sheria zao juu ya zile hafifu. Dunia bila uhalisi itakua dunia hofu sana mtu anaweza fikiria.

Kutoka mtazamo wa kiroho, aina hii ya ulegevu watokea katika kuchanganyikiwa kwa dini, kuwa hakuna dini ya kweli na hakuna njia ya kuwa na uhusiano mzuri na Mungu. Dini zote kwa hivyo zitakuwa za uogo kwa sababu zote zafanya madai ya uhalisi kuhusu maisha ya baadaye. Si jambo geni hii leo watu wakiamini kuwa dini mbili zinazopingana zitakuwa “sawa” hata kama dini zote zadai kuwa na njia peke kuelekea mbinguni au kufunza kweli mbili tafauti. Watu ambao hawamini kuwa kuna ukweli halisi wanapuuza madai haya na kukubali lili la kiulimwengu ambalo lafunza kuwa dini zote ni sawa na barabara zote zaelekea mbinguni. Watu ambao wamekubali mtazamo huu kwa dhadi wanapinga Wakristo wa kievangilisti ambao wanaamini Bibilia wakati inasema kuwa Yesu Kristo ndiye “njia, ukweli na uzima” kuwa Yeye ndiye dhihirisho la ukweli peke na njai peke mtu anaweza kufika mbinguni ( Yohana 14:6).

Wastani umekuwa maadili kuu ya kisasi cha jamii hii leo, uhalisi mmoja, na kwa hivyo, kutokuwa na kiasi ndio uovu peke. Imani yo yote ya dini- hasa imani ya ukweli halisi- imetazamiwa kuwa si ya kiasi, mwisho wa dhambi. Wale wanaokataa ukweli halisi, kila mara watasema kuwa ni sawa kuamini chenye unataka, bora tu haujaribu kulazimisha imani hiyo kwa wengine. Lakini mtazamo huu wenyewe ni imani ya lenye ni zuri na baya, na wale wanaoshkilia hakika wanajaribu kuilazimisha kwa watu wengine. Wanaweka kiwango cha tabia ambacho wasisitiza wengine wakifuate, na hapo wanaasi kila kitu wanacho dai kukishikilia- kujichanganyisha kwingine. Wale wanaoshikilia imani kama hiyo hakika hawataki kuwajibika kwa matendo yao. Kama kuna ukweli halisi, basi kunayo kiwango halisi cha zuri na baya, na tumewajibika kwa viwango hivi. Huu uwajibikaji ndio watu wanakataa wakati wanakata ukweli halisi.

Kataa la ukweli halisi/ukweli wa kiulimwengu na usawa wa tamaduni ambao unakuja na matokeo ya kimantiki ya jamii ambayo imekumbatia nadharia ya ufumbuzi kama elezo la maisha. Ujipushi ambao haukasababishwa na mtu yeyote ni wa kweli, basi maisha hayan maana, hatuna lengo, na hakutawai kuwa na uzuri au ubaya halisi kamwe. Kwa hivyo mwanadamu ako huru kuishi vile anataka na amewajibika kwa matendo yake. Bali haijalishi ni matendo ya uovu namna gani, wanadamu wanakataa uwepo wa Mungu na kweli halisi, bado siku moja watasimama mbele ya kiti cha hukuimu. Bibilia inasema kuwa “…..yanayojulikana yamekuwa dhahiri ndani yao, kwa maana Mungu aliwadhihirishia. Kwa sababu mambo yake yasiyoonekana tangu kuumbwa ulimwengu yanaonekana, na kufahamika kwa kazi zake; yaani, uweza wake wa milele na Uungu wake; hata wasiwe na udhuru; kwa sababu, walipomjua Mungu hawakumtukuza kama ndiye Mungu wala kumshukruu; bali walipotea katika uzushi wao, na mioyo yao yenye ujinga ikatiwa giza. Wakijinena kuwa wenye hekima walipumbazika” (Warumi 1:22).

Kunao ushahidi wo wote wa kuwepo kwa ukweli halisi? Naam. Kwanza kunayo ile akili ya mwanadamu, ambayo kuwa “kitu” ndani yetu chatuambia kwamba ulimwengu lazima uwe katika hali fulani, kuwa mambo mengine ni mazuri au ni mabaya. Akili yetu yatuthibitishia kuwa kuna kitu kibaya na mateso, njaa, ubakaji, uchungu, na uovu, na inatufanya kujua kuwa upendo, ukarimu, huruma, na amani ni mambo yajengayo ambayo tunastahili kuyatafuta. Hii ni kweli kwa kila tamaduni katika nyakati zote. Bibilia inaelezea jukumu la akili ya mwanadamu katika Warumi 2:14-16: “Kwa maana watu wa Mataifa wasio na sheria wafanyapo kwa tabia zao yaliyo ndani ya torati, hao wasio na sheria wameküwa sheria kwa nafsi zao wenyewe. Hao waionyesha kazi ya torati iliyoandikwa mioyoni mwao, dhamiri yao ikiwashuhudia, na mawazo yao, yenyewe kwa yenyewe, yakiwashitaki au kuwatetea; katika siku ile Mungu atakapozihukumu siri za wanadamu, sawasawa na injili yangu, kwa Kristo Yesu.

Thibitisho la pili la uwepo wa ukweli halisi ni sayansi. Sayansi kwa ufupi ni ukimbizaji wa hekima, somo la chenye tunajua na ulizo la kutaka kujua zaidi. Kwa hivyo, somo lote la sayansi ni la lazima lipatikane katika mipaka ya imani kuwa hakuna ukano wa halisi katika ulimwengu anaodumu na halisi hizi zinaweza gunduliwa na kuthibitishwa. Bila uhalisi, kutakuwa na nini cha kusomewa? Mtu anawezaje kujua utafiti wa sayansi ni wa kweli? hakika sheria ile ile ya sayansi simewekwa misingi yao katika uepo wa ukweli halisi.

Thibitisho la tatu la kuupo kwa ukweli halisi/ ukweli wa kiulimwengu ni dini. Dini zote za dunia zinajaribu kutoa maana na elezo la maisha. Vyote vimezaliwa nche ya hitaji la mwanadamu kwa cho chote zaidi ya kuwepo. Kupitia kwa dini, wanadamau wanamtafuta Mungu, tumaini la kesho, msamaha wa dhambi, amani katikati mwa majanga, na majibu kwa maswali yetu magumu. Dini ni ushahidi kuwa mwanadamu kiumbe maalumu ambacho hakikujibuka kutoka kwa wanyama. Ni ushahidiki kuwa lengo kuu kabisa na uwepo wa Muumbaji wa kibinafsi na wa lengo ambaye aliweka ndani ya mwanadamu hitaji la kumjua Yeye. Na kama kwa kwelikuna Muumbaji, basi anakuwa kiwango cha ukweli halisi, na ni mamlaka yake ambayo yaweka msingi ukweli.

Kwa bahati, kunayo mengi sana ambayo Muumbaji, na amefunua kweli yake kwetu kupitia kwa Neno lake, Bibilia. Kwa kujua kweli halisi/ ukweli wa ulimwengu itawezekana peke kupitia kwa uhusiano wa kibianafsi na Yule anayesema kuwa Yeye ndiye kweli- Yesu Kristo. Yes alisema kuwa yeye ndiye njia, na ukweli na uzima na njia peke kuelekea kwa Mungu (Yohana 14:6). Hoja kwamba kweli halisi ipo yatuelekeza kwa ukweli kuwa kuna Mungu mwenye mamlaka yote ambaye aliumba mbingu na nchi na amejidhihirisha kwetu ili tuweze kumjua Yeye binafsi kupitia kwa Mwanaye Yesu Kristo. Huu ndio ukweli halisi.

English



Rudi kwa ukurasa wa nyumbani wa Kiswahili

Kunayo kitu kama ukweli kamili/Ukweli wa watu wote?
Shiriki ukurasa huu: Facebook icon Twitter icon Pinterest icon Email icon
© Copyright Got Questions Ministries