settings icon
share icon
Swali

Je, mtazamo wa Kikristo ni upi kuhusu uumbwaji wa binadamu kujamiana?

Jibu


Huku kukiwa kwamba Biblia haishugulikii hasa swala la uumbaji wa binadamu bila kujamiana, kuna kanuni katika maandiko ambazo zinaweza kutupa mwanga zaidi juu ya dhana. Uumbaji bila kujamiana unahitaji chembe za damu (DNA) kutolewa katika seli kiinitete. Kwanza, DNA kuondolewa kutoka chumba kidogo cha kiini kiumbe. Vifaa, vilivyo na habari maumbile, kisha huwekwa katika kiini cha chumba kidogo cha kiinitete. Kiini kupokea maelezo mapya ya jeni bila kuwa na DNA yake mwenyewe kuondolewa ili kukubali DNA mpya. Kama kiini kinapokea DNA mpya, kiinitete ya aina mbili hukuwa. Hata hivyo, kiinitete kiini kinaweza kukataa DNA mpya na kufa. Pia, inawezekana kabisa kuwa kiinitete kinaweza kuishi baada ya vifaa vya asili ya maumbile kuondolewa kutoka kwa kiini chake. Katika matukio mengi, wakati bila kujamiana ni jaribio, kijusi kadhaa hutumiwa ili kuongeza tabia mbaya ya uamishaji mpya wa maumbile ili kuongeza mafanikio ya vifaa. Huku ikiwezekana kwa kiumbe sawia kuundwa kwa namna hii (kwa mfano, mwansesere wa kondoo), nafasi ya mafanikio kuiga kiumbe bila tofauti, na bila matatizo, ni ndogo sana.

Mtazamo wa Kikristo wa mchakato wa uumbaji wa binadamu bila kujamiana unaweza kuelezwa katika mwanga wa kanuni kadhaa wa maandiko. Kwanza, binadamu wameumbwa kwa mfano wa Mungu na kwa hiyo, ni waa kipekee. Mwanzo 1:26-27 inadai kwamba mtu ameumbwa kwa sura na mfano wa Mungu na ni wa kipekee miongoni mwa ubunifu wote. Ni wazi, maisha ya binadamu ni kitu cha thamani na si kuchukuliwa kama bidhaa inayonunuliwa na kuuzwa. Baadhi ya watu hukuzwa dhana ya uumbaji wa binadamu bila kujamiana kwa lengo la kuunda viungo badala ya watu katika haja ya kuvivukisha ambao hawawezi kupata wafadhili. Fikira ni kwamba kuchukua chembe za damu (DNA) ya mtu mwenyewe na kuumba chombo sawia inajumuisha DNA ambayo kwa kiasi kikubwa hupunguza uwezekano wa chombo kukataliwa . Wakati huu inaweza kuwa kweli, tatizo ni kwamba kufanya hivyo inarahizisha maisha ya binadamu. Mchakato wa uumbaji bila kujamiana unahitaji kijusi binadamu kutumika. Wakati seli zinaweza tumika na kufanya viungo mpya, ni muhimu kwa kuua mimba kadhaa kupata chembe za damu (DNA) zinazohitajika. Katika kiini uumbaji bila kujamiana "itatupilia" mbali kijusi binadamu kama "vifaa taka," kuondoa nafasi kwa hicho kijusi kukua katika ukomavu kamili.

Watu wengi wanaamini kwamba maisha hayaanzi saa kutiwa mimba na ukuaji wa kiinitete, na kwa hiyo mimba si binadamu halisi. Biblia inafundisha tofauti. Zaburi 139:13-16 anasema, "maana Wewe ndiwe uliyeniumba mtima wangu, Uliniunga tumboni mwa mama yangu. Nitakushukuru kwa kuwa nimeumbwa kwa jinsi ya ajabu ya kutisha. Matendo yako ni ya ajabu, mifupa yangu haikusitirika kwako, nilipoumbwa kwa siri nilipoungwa kwa ustadi pande za chini za nchi. Macho yako yaliniona kabla sijakmailika; chuoni mwako ziliandikwa zote pia, siku zilizoamriwa kabla hazijawa bado." Mwandishi, Daudi, anatangaza kwamba yeye alikuwa anajulikana binafsi na Mungu kabla ya kuzaliwa, kwa maana ya kuwa katika mimba yake yeye alikuwa binadamu na aliyeteuliwa na Mungu kwa siku zijazo.

Zaidi ya hayo, Isaya 49:1-5 inazungumzia Mungu akimwita Isaya kwa huduma yake kama nabii wakati alipokuwa bado tumboni mwa mama yake. Pia, Yohana Mbatizaji kujazwa na Roho Mtakatifu wakati alipokuwa bado tumboni (Luka 1:15). Hizi hoja zote zinaonyesha msimamo wa Biblia juu ya maisha kuanzia saa ya mimba. Katika mwanga wa hili, uumbaji wa binadamu bila kujamiana, kwa uharibifu huu wa viinitete vya binadamu, hautakuwa sawia na lengo la Biblia juu ya maisha ya binadamu.

Aidha, kama binadamu aliumbwa, basi lazima kuna Muumba, na kwa hivyo binadamu anawajibika kwa Muumba huyo. Ingawa fikira maarufu - saikolojia ya kidunia na mawazo kibinadamu - ingekuwa imani moja kwamba mtu atawajibika sio kwa mtu lakini kwake mwenyewe na mtu huyo ni mamlaka ya mwisho, Biblia inafundisha tofauti. Mungu aliumba mtu na alimpa wajibu juu ya nchi (Mwanzo 1:28-29, 9:1-2). Pamoja na jukumu hili anawajibika kwa Mungu. Mwanadamu sio wa mamlaka ya mwisho juu yake mwenyewe, na hiyo ni katika nafasi ya kufanya maamuzi juu ya thamani ya maisha ya binadamu. Wala, basi, sayansi ina mamlaka ambayo maadili ya uumbaji wa binadamu bila kujamiana, utoaji mimba, au kifo cha huruma uamuliwa. Kulingana na Biblia, Mungu pekee ndiye ana haki ya udhibiti wa maisha ya binadamu. Kwa kujaribu kudhibiti mambo kama hayo ni ni mtu kujiweka katika mwenyewe katika nafasi ya Mungu. Ni wazi, mwanadamu hapazwi kufanya hivyo.

Kama sisi twamwona mwanadamu kama kiumbe chochote na si kama kiumbe kipekee yeye yuko, si vigumu kuona binadamu kama utaratibu tu unaohitaji ukarabati na utunzaji. Lakini sisi si mkusanyiko wa molekuli na kemikali. Biblia inafundisha kwamba Mungu aliumba kila mmoja wetu na ana mpango maalum kwa ajili ya kila mmoja wetu. Zaidi ya hayo, yeye anatafuta uhusiano binafsi na kila mmoja wetu kwa njia ya Mwana wake, Yesu Kristo. Wakati kuna masuala ya uumbaji wa binadamu bula kujamiana ambayo inaweza kuonekana na faida, mwanadamu hana mamlaka kuhus mahali umbaaji wa mwanadamu bila kujamiana kiteknolojia unaweza kwelekea. Ni upumbavu kwa kudhani kuwa nia nzuri ni matumizi ya uumbaji bila kujamiana. Mwanadamu hayuko katika nafasi zoezi la wajibu au hukumu ambayo inatakiwa serikali uumbaji wa binadamu bila kujamiana.

Swali la mara kwa mara ni kama uumbaji wa binadamu bila kujamiana, chukulia kwamba uumbaji wa binadamu bila kujamiana siku moja umefanikiwa, na uwe na nafsi. Mwanzo 2:7 inasema, "Bwana Mungu akamfanya mtu kwa mavumbi ya ardhi, akampulizia puani pumzi ya uhai;. Na mtu akawa nafsi hai " Hapa ni maelezo ya Mungu vile alivyo umba uhai, na mwanadamu akawa kiumbe hai. Nafsi mi kile sisi tulicho (1 Wakorintho 15:45). Swali ni ni aina gani ya nafsi hai ya mwanadamu ingekuwa inaumbwa bila kujamiana? Hiyo siyo swali ambalo linaweza jibiwa kikamilifu. Hata hivyo, inaonekana kwamba, kama binadamu walikuwa mafanikio ya uumbaji bila kujamiana, kilichoumbwa kingekuwa kama mwanadamu yeyote, akiwa pamoja na nafsi ya milele, kama binadamu yeyote.

English



Rudi kwa ukurasa wa nyumbani wa Kiswahili

Je, mtazamo wa Kikristo ni upi kuhusu uumbwaji wa binadamu kujamiana?
Shiriki ukurasa huu: Facebook icon Twitter icon Pinterest icon Email icon
© Copyright Got Questions Ministries