settings icon
share icon
Swali

Je! Imani katika Mungu inahitilafiana na sayansi?

Jibu


Sayansi inaweza fafanuliwa kuwa “utazamo, ufanano, maelezo, jaribio, utafiti na maelezo ya nadharia ya mambo.” Sayansi ni mtindo ambao mwanadamu anaweza kutumia kupata uelewo zaidi wa ulimwengu. Ni utafutaji wa maarifa kupitia utazamo. Kupiga hatua kisayansi yaonyesha upeo wa mwanadamu wa kimawazo na ubunifu. Ingawa imani ya Mkristo katika sayansi haistahili kuwa sawa na imani yetu katika Mungu. Mkristo anaweza kuwa na imani katika Mungu na aiheshimu sayansi, bora tu tukumbuke ni gani kamilifu na ni gani sio kamilifu.

Imani yetu katika Mungu ni kuamini kwa imani. Tuko na imani katika Mwanawe kwa wokovu, imani katika neno lake kwa maelezo, na imani katika Roho wake Mtakatifu kwa uongozi. Imani yetu kwa Mungu lazima iwe kamili kwa vile wakati tunapoweka imani yetu wa Mungu, tunamtegemea muumbaji makamilifu, anayejua mambo yote, aliye kila mahali. Imani yetu katika sayansi yastahili kuwa ya kiakili tu peke yake bila kuongeza kitu kingine. Tunaweza kuhesabu kwa hisia kufanya mambo mengi, lakini tunaweza kuhesabu makosa ya sayansi. Ikiwa tutaweka imani katika sayansi, tunategemea mwanadamu ambaye si mkamilifu, mwenyedhambi, aliye na mipaka na anayeharibika. Sayansi katika historia yote imekuwa na kasoro kuhusu mambo mengi, kama vile sura ya nchi, mwangaza wa nguvu, chanjo, ubadilisho wa damu na hata uzao. Kamwe Mungu hana makosa.

Ukweli sio kitu cha kuogofya, kwa hamna sababu ya Mkristo kuogopa sayansi nzuri. Kusoma mengi zaidi jinsi vile Mungu aliiumba ulimwengu inamsadia mwanadamu wote kutika maajabu ya uumbaji. Kupanua hekima yetu inatusaidia kukabiliana na magonjwa, kutojua na elewo ovu. Ingawa kuna hatari wakati wanasayansi wanaposhikilia kuwa imani yao kwa akili ya mwanadamu iko juu ya imani yetu katika muumba. Watu hawa ni tofauti na yule mtu ambaye amejitolea kwa dini; wamechagua imani kwa mwanadamu na watapata hoja za kuitetea imani yao.

Bado, wanasayansi ya kirazini, hata wale hukataa kumwamini Mungu, wanakubali kuwa wanakosa ukamilifu katika uelewo wetu wa ulimwengu. Bado wanakubali kwamba hata Mungu au Bibilia haiwezi kuthibitishwa au kosa thibitishwa na wanasayansi, vile wingi wa nadharia yao waipendayo haiwezi thibitishwa au kosa thibitishwa imelengwa kuwa adabu ya katikati, kutafuta ukweli pekee sio kuendeleza agend.

Sayansi nyingi yaunga mkono uwepo na kazi ya Mungu. Zaburi 19:1 yasema, “Mbingu zauhubiri utukufu wa Mungu, Na anga laitangaza kazi ya mikono yake.” Kama wanasayansi wa kisasa wanavyo gundua mengi kuhusu anga, tunapata ushahidi mwingi wa uumbaji. Kitu cha kushangaza na uhalisi wa ongezeko la DNA, utatanishi na sheria inayofunga ya fisikia, na umoja wa hali za kemia hapa ulimwenguni zote zafanya kazi zikiunga mkono ujumbe wa Bibilia. Mkristo lazima aikubali sayansi ambayo yatafuta ukweli, lakini akatae “makuani wa sayansi” wanaoweka hekima ya mwanadamu mbele kuliko Mungu.

English



Rudi kwa ukurasa wa nyumbani wa Kiswahili

Je! Imani katika Mungu inahitilafiana na sayansi?
Shiriki ukurasa huu: Facebook icon Twitter icon Pinterest icon Email icon
© Copyright Got Questions Ministries