settings icon
share icon
Swali

Ni ishara gani za nyakati za mwisho?

Jibu


Mathayo 24:5-8 inatupa hoja muimu sana, kwa hivyo tunaweza gundua njia tutakayo tatua swala la nyakati za mwisho, “Kwa sababu wengi watakuja kwa jina langu, wakisema, Mimi ni Kristo, nao watawadanganya wengi. Nanyi mtasikia habari za vita na matetesi ya vita; angalieni, msitishwe; maana hayo hayana budi kutukia; lakini ule mwisho bado. Kwa maana taifa litaondoka kupigana na taifa, na ufalme kupigana na ufalme kutakuwa na njaa, na matetemeko ya nchi mahali mahali.” Kutaongezeka na Masia wa uongo, kutaongezeka na viata, njaa, mapigo, na majanga- hizi ndizo ishara za nyakati za mwisho. Katika ukurasa huu, ingawa tumepewa onyo: hatustahili kudanganywa, kwa sababu matukio hayo ni ishara ya mwanzo wa machungu; mwisho bado utakuja.

Wafafanusi wengine wa Bibilia huwa wanaashiria kila tetemeko, kila mchafuko wowote wa kisiasa, na kila ufamishi wowote kwa Israeli kama ishara mathubuti ya nyakati za mwisho zikikaribia. Bali matukio yanaweza ashiria nyakati za mwisho, hizo si ishara kamili kwamba nyakati za mwisho zimekaribia. Mtume Paulo alionya kuwa katika siku za mwisho kutaongezeka na mafundisho ya uongo. “Basi Roho anena waziwazi ya kwamba nyakati za mwisho wengine watajitenga na imani, wakisikiliza roho zidanganyazo, na mafundisho ya mashetani” (1 Timotheo 4:1). Siku za mwisho zimeelezewa kuwa kama, “nyakati za kuogofya” kwa sababu ya kuongezeka kwa maovu kwa mwanadamu na watu wanaoendelea “kukataa ukweli” (2 Timotheo 3:1-9; angalia pia 2 Wathesalonike 2:3).

Ishara zingine ziwezekanazo ni, ujenzi wa hekalu ya Kiyahudi katika Yerusalemu, ongezeko la uadui kwa taifa la Israeli, na mwelekeo wa kuwa na serikali moja ulimwenguni. Ishara kuu ya nyakati za mwisho, ni taifa la Israeli. Mwaka wa 1948, Israeli ilitambulika kama taifa huru linaojisimamia, kwa mara ya kwanza tangu A.D 70 (Baada ya Yesu kuzaliwa), na Ezekieli alitabiri kuwa kutakuwa na uhuisho wa kimwili na kiroho kwa Israeli (Ezekieli 37). Kuwa na Israeli kama taifa linalojisimamia katika ardhi yao ni muimu kwa ufunuo wa nabii wa nyakati za mwisho kwa sababu ya Israeli itatawala nyakati za mwisho (Danieli 10:14; 11:41; Ufunuo Wa Yohana 11:8)

Ishara hizi zikiwa katika mawazo, tutakua na hekima ya kutambua na kwa kungojea nyakati za mwisho. Kamwe tusifafanue matukio yoyote kuwa ishara kamili za kufika kwa nyakati za mwisho. Mungu ametupa habari ya kutosha ambayo tunaweza kujitayarisha, na hiyo ndiyo tumeitiwa tuwe.

English



Rudi kwa ukurasa wa nyumbani wa Kiswahili

Ni ishara gani za nyakati za mwisho?
Shiriki ukurasa huu: Facebook icon Twitter icon Pinterest icon Email icon
© Copyright Got Questions Ministries