settings icon
share icon

Kitabu cha 1 Samweli

Mwandishi: Mwandishi hajulikani. Tunajua kwamba Samweli aliandika kitabu (1 Samweli 10:25), na inawezekana kabisa kwamba yeye aliandika sehemu ya kitabu hiki pia. Wachangiaji wengine wa 1 Samweli ni manabii / wanahistoria Nathani na Gadi (1 Mambo ya Nyakati 29:29).

Tarehe ya Kuandikwa: Awali, vitabu vya Samweli 1 na 2 vilikuwa ni kitabu kimoja. Watafsiri wa miaka kati ya sabini na sabini na tisa walivitenga, na sisi tumeweka mtengo huo tangu. Matukio ya 1 Samweli yanachukua muda wa takriban miaka 100, kutoka c. 1100 KK hadi c. 1000 KK. Matukio ya 2 Samweli yanachukua kipindi kingine cha miaka 40. Tarehe ya kuandika, basi, wakati mwingine itaezakuwa baada ya 960 BC.

Kusudi la Kuandika: Samuel ya kwanza inatoa historia ya Israeli katika nchi ya Kanaani kama hoja kutoka utawala wa waamuzi kuwa taifa ya umoja chini ya wafalme. Samuel anaibuka kama Mwamuzi wa mwisho, na yeye anawateua, wafalme wawili wa kwanza, Sauli na Daudi.

Mistari muhimu:” Lakini neno hilo likawa baya machoni pa Samweli, waliposema, Tupe mfalme atuamue. Naye Samweli akamwomba BWANA. BWANA akamwambia Samweli, Isikilize sauti ya watu hawa katika kila neno watakalokwambia; kwa maana hawakukukataa wewe, bali wamenikataa mimi, ili nisiwe mfalme juu yao.”(1 Samweli 8;6-7)

"'Naye Samweli akamwambia Sauli, Umefanya upumbavu;hukuishika amri ya BWANA, Mungu wako, aliyokuamuru; kwa maana BWANA angaliufanya ufalme wako kuwa imara juu ya Israeli milele. Lakini sasa ufalme wako hautadumu; BWANA amejitafutia mtu aupendezaye moyo wake, naye BWANA amemwamuru yeye kuwa mkuu juu ya watu wake, kwa sababu wewe hukulishika neno lile BWANA alilokuamuru. '"(1 Samweli 13: 13-14).

"Naye Samweli akasema, je! BWANA huzipenda sadaka za kuteketezwa na dhabihu sawasawa na kutii sauti ya BWANA? Angalia, kutii ni bora kuliko dhabihu, Na kisikia kuliko mafuta ya beberu. Kwani kuasi ni kama dhambi ya uchawi, Na ukaidi ni kama ukafiri na vinyago; Kwa kuwa umelikataaneno la BWANA, Yeye naye amekukataa wewe usiwe mfalume. "(1 Samweli 15: 22-23).

Muhtasari kwa kifupi: kitabu cha 1 Samweli inaweza kwa nadhifu kugawanywa katika sehemu mbili: maisha ya Samweli (sura 1-12) na maisha ya Sauli (sura 13-31).

Kitabu huanza na muujiza wa kuzaliwa kwa Samuel kwa mujibu wa maombi ya mama yake kwa bidii. Kama mtoto, Samweli aliishi na kutumikia katika hekalu. Mungu akamtenga kama nabii (3: 19-21), na unabii wa kwanza wa mtoto ulikuwa mmoja wa hukumu juu ya makuhani wapenda rushwa.

Israeli wanaenda vitani na maadui wao wa kudumu, Wafilisti. Wafilisti wanakamata sanduku la agano na kulimilki kwa muda , lakini wakati Bwana analeta hukumu, Wafilisti wanarudisha sanduku. Samue anatoa wito kwa Israeli ili watubu (7: 3-6) na kisha ushindi juu ya Wafilisti.

Watu wa Israeli, kutaka kuwa kama mataifa mengine, wanatamani mfalme. Samweli hakufurahishwa na madai yao, lakini Bwana anamwambia kwamba si uongozi wa Samweli wamekataa bali ni wake mwenyewe. Baada ya kuwaonya watu kuwa mfalme itakuwa na maana gani, Samweli anampaka mafuta, Mbenyamini aitwaye Sauli, ambaye anatawazwa Mizpa (10: 17-25).

Sauli anafurahia mafanikio ya awali, kuwashinda Waamoni katika vita (sura ya 11). Lakini kisha yeye hufanya mfululizo wa atua mbaya: yeye kujikinai anatoa sadaka (sura ya 13), hufanya kiapo ya kijinga kwa gharama ya mwanawe Jonathan (sura ya 14), na yeye anaasi amri moja ya Bwana ya moja kwa moja (sura ya 15). Kama matokeo ya uasi wa Sauli, Mungu anchagua mwingine kuchukua nafasi ya Sauli. Wakati huo huo, Mungu anaondoa baraka zake kwa Sauli, na roho mbaya huanza kuchochea Sauli kuelekea wazimu (16:14).

Samweli anasafiri Bethlehemu na kumpaka mafuta kijana aitwaye Daudi kuwa mfalme baadaye (sura ya 16). Baadaye, Daudi ana mapambano yake maarufu na Goliathi anakuwa shujaa wa kitaifa (sura 17). Daudi anakuwa mtumishi katika makao ya Sauli, anaoa bintiye Sauli, na anafanya urafiki na mwana wa Sauli. Sauli mwenyewe anakuwa na wivu kwa mafanikio ya Daudi na umaarufu, na yeye anajaribu kumuua Daudi. Daudi anakimbia, na hivyo kuanza kipindi ajabu kisicho cha kawaida , fitina, na mahaba. Kwa msaada usio wa kawaida, Daudi anaponea chuchupu lakini mara kwa mara anaepuka Sauli mwenye kiu ya damu (sura 19-26). Wakati wote huo, Dauidi anadumisha uadilifu wake na urafiki wake na Jonathan.

Karibu na mwisho wa kitabu, Samweli amefariki, na Sauli ni mtu aliyepotea. Katika usiku wa vita na Wafilisti, Sauli anataka majibu. Baada ya kukataa Mungu, yeye anaona hakuna msaada kutoka mbinguni na yeye anatafuta ushauri kutoka kwa mpatanishi badala yake. Wakati wa mkusanyiko, roho wa Samweli anafufuka kutoka kwa wafu ili kutoa unabii moja wa mwisho: Sauli atakufa katika vita siku ifuatayo. Unabii unatimia, Wana wa Sauli watatu, ikiwa ni pamoja na Jonathan, kushindwa vitani, na Sauli anajiua.

Kuonyesha: Maombi ya Hana katika 1 Samweli 2: 1-10 hufanya marejeleo ya kinabii kadhaa kwa Kristo. Yeye anamtukuza Mungu kama Mwamba wake (v. 2), na tunajua kutoka kwa rekodi ya injili kwamba Yesu ni Mwamba ambaye juu yake tunapaswa kujenga nyumba yetu ya kiroho. Paulo anamrejelea Yesu kama "mwamba wa kosa" kwa Wayahudi (Warumi 9:33). Kristo anaitwa "mwamba wa kiroho" ambaye aliwatolea kinywaji cha kiroho kwa Waisraeli katika jangwa kama yeye hutoa "maji yaliyo hai" kwa nafsi zetu (1 Wakorintho 10: 4; Yohana 4:10). Maombi ya Hana pia yanafanya kumbukumbu ya Bwana ambaye atahukumu mwisho wa dunia (v 2:10.) Huku Mathayo 25: 31-32 inarejelea Yesu kama Mwana wa Mungu ambaye atakuja katika utukufu kuhukumu kila mtu.

Vitendo tekelezi: Hadithi ya kutisha ya Sauli ni utafiti katika nafasi iliyoaribika. Hapa kuna mtu ambaye alikuwa na vyote- heshima, mamlaka, utajiri, afya nzuri, na zaidi. Bado alikufa katika kukata tamaa, hofu ya maadui zake na kujua alikuwa ameangusha taifa lake, familia yake, na Mungu wake.

Sauli alifanya makosa ya kufikiri angeweza kumpendeza Mungu kwa njia ya kutomtii. Kama wengi siku hizi, aliamini kwamba nia ya busara ni mbadala kwa tabia mbaya. Labda nguvu zake zikamwiingia kwa kichwa chake, na yeye alianza kufikiri alikuwa juu ya sheria. Kwa namna fulani alijenga maoni ya amri za Mungu kuwa duni na maoni ya yake mwenyewe kuwa juu. Hata wakati alipokabiliwa na makosa yake, alijaribu kujitetea mwenyewe, na hapo ndipo Mungu alimkataa yeye (15: 16-28).

Tatizo la Sauli ni moja sisi sote tunakumbana nalo- tatizo la moyo. Kutii mapenzi ya Mungu ni muhimu sana kwa ajili ya mafanikio, na kama tukifanya katika kiburi kuasi dhidi yake, sisi twajiweka wenyewe juu kwa hasara.

Daudi, kwa upande mwingine, hakuwa anaonekana kwa kiasi kikumbwa mwanzoni. Hata Samweli alijaribiwa kumdunisha (16: 6-7). Lakini Mungu anaona moyo na akaona katika Daudi, mtu baada ya moyo wake mwenyewe (13:14). Unyenyekevu na uadilifu wa Daudi, pamoja na ujasiri wake kwa Bwana na ahadi zake za maombi, uliweka mfano mzuri kwutu sisi sote.

English

Rudi kwa ukurasa wa nyumbani wa Kiswahili

Kitabu cha 1 Samweli
Shiriki ukurasa huu: Facebook icon Twitter icon Pinterest icon Email icon
© Copyright Got Questions Ministries