settings icon
share icon

Kitabu cha Zekaria

Mwandishi: Zekaria 1: 1 inatambua mwandishi wa Kitabu cha Zekaria kama Nabii Zakaria.

Tarehe ya kuandikwa: Kitabu cha Zakaria huenda kiliandikwa kimsingi katika makundi mawili, kati ya 520 na 470 kk

Kusudi la Kuandika: Zakaria alisisitiza kuwa Mungu ametumia manabii wake kufundisha, kuonya na kusahihisha watu wake. Kwa bahati mbaya, walikataa kusikiliza. Dhambi zao zilileta adhabu ya Mungu. kitabu pia kinatoa ushahidi kwamba hata unabii unaweza kupotosha. Historia inaonyesha kwamba katika kipindi hiki unabii hukuheshimiwa miongoni mwa Wayahudi, na kusababisha kipindi cha kati ya maagano wakati ambao hakuna sauti ya kinabii ambayo iliwahi kuzungumzwa kwa watu wa Mungu.

Mistari muhimu: Zekaria 1: 3, "Basi, uwaambie, Bwana wa majeshi asema hivi, Nirudieni mimi, asema Bwana wa majeshi, nami nitawarudia ninyi, asema Bwana wa majeshi."

Zakaria 7:13, "Ikawa kwa sababu alilia, wao wasitake kusikiliza; basi, wao nao watalia, wa mimi sitasikiliza, asema Bwana wa majeshi."

Zekaria 9: 9, "Furahi sana, Ee binti Sayuni; piga Kelele, Ee Binti Yerusalemu; Tazama, mfalme wako anakuja kwako, ni mwenye haki, naye ana wokovu; ni mnyenyekevu, amepanda punda, naam, mwana- punda, mtoto wa punda!. "

Zekaria 13:. 9, "Nami nitalileta fungu lile la tatu na kulipitisha kati ya moto, nami nitawasafisha kama fedha isafishwavyo, nami nitawajaribu kama dhahabu ijaribiwavyo; wataliitia jina langu, nami nitawasikia; mimi nitasema, watu hawa ndio wangu; nao watasema, Bwana ndiye Mungu wangu."

Muhtasari kwa kifupi: kitabu cha Zekaria kinafundisha kwamba wokovu unaweza kupatikana kwa wote. sura ya mwisho inaonyesha watu kutoka duniani kote kuja kumwabudu Mungu, ambaye anataka watu wote kumfuata. Hii si mafundisho ya kilimwengu, yaani, kwamba watu wote wataokolewa kwa sababu ni asili ya Mungu kuokoa. Badala yake, kitabu kinafundisha kwamba Mungu anatamani kwamba watu wote kumwabudu na anapokea wale ambao hufanya, bila kujali sura yao ya kitaifa au kisiasa, kama katika kukomboa kwa Yuda na Yerusalemu kutoka kwa maadui wao wa kisiasa. Hatimaye, Zakaria alihubiri ya kuwa Mungu ni mkuu juu ya dunia hii, bila ya kuonekana mpinzani yeyote. Maono yake ya baadaye yanaonyesha kwamba Mungu anaona yote yatakayotokea. Maonyesho ya Mungu kuingilia kati katika ulimwengu hufundisha kwamba hatimaye ataleta matukio ya binadamu kwa mwisho auchaguao. Yeye haondoi uhuru wa mtu binafsi wa kumfuata Mungu au kuasi, lakini anawashirikisha watu kuwajibika kwa maamuzi wafanyao. Katika sura ya mwisho, hata nguvu za asili huitikia udhibiti wa Mungu.

Ishara: Unabii kuhusu Yesu Kristo na enzi za kimasiya uko kwa wingi katika Zakaria. Kutokana na ahadi kwamba Masihi atakuja na kukaa katikati yetu (Zekaria 2: 10-12; Mathayo 1:23) hadi kwa mfano wa Tawi na jiwe (Zakaria 3: 8-9, 6: 12-13; Isaya 11 : 1; Luka 20: 17-18) hadi kwa ahadi ya kuja kwake mara ya pili ambapo waliomdunga watamwangalia na kuomboleza (Zekaria 12:10; Yohana 19: 33-37) Kristo ni kusudi la kitabu cha Zakaria. Yesu ni Mwokozi wa Israeli, chemchemi ambaye damu yake inafuta dhambi za wote ambao huja kwake kwa ajili ya wokovu (Zakaria 13: 1; 1 Yohana 1: 7).

Vitendo Tekelezi: Mungu anatarajia ibada ya kweli na maisha ya maadili yetu siku hizi. Mfano wa Zakaria kupenya madhara ya kitaifa kunatukumbusha kuyafikia maeneo yote ya jamii yetu. Sisi lazima tupanue mwaliko wa Mungu wa wokovu kwa watu wote wa asili ya kila taifa, lugha, tabaka na tamaduni. Wokovu huo unapatikana tu kwa njia ya kumwagwa damu ya Yesu Kristo juu ya msalaba, ambaye alikufa kwa ajili yetu ili kubadilishana na dhambi. Lakini ikiwa tutakataa sadaka hiyo, hakuna kafara nyingine ambayo kwayo tunaweza kupatanishwa na Mungu. Hakuna jina jingine chini ya mbingu ambayo watu wanaokolewa kwalo (Matendo 4:12). Hakuna muda wa kupoteza; leo ni siku ya wokovu (2 Wakorintho 6: 2).

English

Rudi kwa ukurasa wa nyumbani wa Kiswahili

Kitabu cha Zekaria
Shiriki ukurasa huu: Facebook icon Twitter icon Pinterest icon Email icon
© Copyright Got Questions Ministries