settings icon
share icon
Swali

Ni namna gani Wakristo wanastahili kuwarudi watoto wao? Bibilia inasema nini?

Jibu


Vile unaweza kurudi mtoto wako vizuri sana laweza kuwa jambo gumu kujifunza, lakini ni la muimu. Wengine wanadai kwamba adhabu ya fimbo kama vile kumchapa matakoni ndio njia pekee Bibilia ayaunga mkono. Wengine wanasisitiza “zile zimepitwa na wakati” na adhabu zingine ambazo haziusishi adhabu ya fimbo ndiso sinaweza kuzaidia. Bibilia inasema nini? Bibilia inafunza kuwa adhabu ya fimbo ndiyo ya kadri, ya muimu na inastahili.”

Usielewe vipaya-kamwe hatupendekezi dhuluma kwa watoto. Mtoto kamwe asipewe adhabu kwa fimbo kiwango ambacho kunamletea maumivu kwa mwili. Kulingana na Bibilia, ingawa, adhabu inayostahili na ambayo ni fimbo imezuiliwa na wengi ndio kitu kizuri na huchangia uuwaji wema wa mtoto na njia nzuri ya kumlea mtoto.

Maandiko mengi kweli yanaunga mkono adhabu ya fimbo. “Usimnyime mtoto wako mapigo; maana ukimpiga kwa fimbo hatakufa. Utampiga kwa fimbo, Na kumwokoa nafsi yake na kuzimu” (Methali 23:13-14; ona pia 13:24; 22:15; 20:30). Bibilia kwa dadhi yasisitiza umuimu wa adhabu; ni kitu ambacho wote lazima tuwe nacho ili tuwe watu zalishi, na hasa kwa muda mwingi husomwa kwa urahisi tukiwa wadogo. Watoto ambao hawaadhibiwi kira mara wanakuwa wakaidi, hawana heshima kwa mamlaka na kwa matokeo wanapata wakati mgumu kwa chaguo lao kumtii na kumfuata Mungu. Mungu mwenyewe anatumia adhabu kuturekebisha na kutuongoza katika mapito mazuri na anatusii tutubu makosa yetu (Zaburi 94:12; Methali 1:7; 6:23; 12:1; 13:1; 15:5; Isaya 38:16; Waebrania 12:9).

Ili tutumie adhabu inavyopasa na kulingana na kanuni ya Bibilia, wazazi lazima waujue ushauri wa maandiko kuihusu adhabu. Kitabu cha Methali kiko na wingi wa hekima kuhusu kuwalea watoto, kama vile, “Fimbo na maonyo hutia hekima; Bali mwana aliyeachiliwa humwaihisha mamaye” (Methali 29:15). Aya hii yaorodhesha madhara ya kutomrudi mtoto kwa mzazi zimekataliwa. Kweli maonyo malengo yake lazima yawe ya manufaa kwa mtoto na kamwe yasitumike kuidhinisha dhuluma kwa mtoto. Kamwe yasitumike kumweka mtoto hasira na mahangaiko.

Adhabu inatumika pale tu kuwaonya na kuwafunza watu kuenenda katika njia sawa. “Kila adhabu wakati wake haionekani kuwa kitu cha furaha, bali cha huzuni; lakini baadaye huwaletea wao waliozoezwa nayo matunda ya haki yenye amani” (Waebrania 12:11). Adhabu ya Mungu ni upendo, vile inavyostahili kati ya mzazi na mtoto wake. Adhabu ya fimbo kamwe isitumike kuleta madhara ya mwili yanayodumu au uchungu. Adhabu ya fimbo kila mara lazima iwe imefuatwa pindi tu tunapokabiliana na mtoto kwa uakikisho kuwa amempendwa. Nyakati hizi ni nyakati kamilifu kumfunza mtoto kuwa Mungu anatuadhibu kwa sababu anatupenda, vile tunavyofanya kwa watoto wetu.

Je! Aina zingine za adhabu kama vile “kumnyima wakati” zinaweza kutumka kama adhabu ya fimbo? Wazazi wengine wanapata kuwa watoto wao hawaitikii vizuri kwa adhabu ya fimbo. Wazazi wengine wanapata kuwa “kuwanyima wakati,” au kumanyanganya mtoto kitu itafanya kazi vizuri kwa kumtia mtoto moyo ili abadilishe tabia yake. Kama kwa kweli hiyo ndio hali, kwa vyovyote vile, mzazi lazima mtindo ambao utaleta mabadiliko yanayojitajika kwa mtoto. Bibilia inaposema bila kataa lolote adhabu ya fimbo, Bibilia hasa imehusika na lengo la kujenga tabia ya kiungu, ili kwamba katika mtindo huu bainifu utumike kwa kuleta makisio yanayokusudiwa kwa mtoto.

Kufanya mambo haya magumu zaidi ni dhana kwamba serikali imeanza kujumlisha kila aina ya adhabu yoyote kwa mtoto kama dhuluma kwa mtoto. Wazazi wengi hawapigi watoto wao kwa mkono kwa kuogopa kuripotiwa kwa serikali kutahatarisha watoto wao kuchukuliwa na serikali. Wazazi wanastahili kufanya nini ikiwa serikali imefanya adhabu ya fimbo kuwa kinyume na sheria? Kulingana na Warumi 13:1-7, wazazi wanastahili kuitii serikali. Serikali kamwe isiwai kuhitilafiana na Neno la Mungu, na adhabu ya fimbo, na kunena Kibibilia ni kwa manufaa ya mtoto. Ingawa kuwalelea watoto katika familia ambazo kwa uchache sana wanapokea adhabu ni ya muimu zaidi kuliko kuwapoteza watoto wetu kwa serikali “ituchungie.”

Katika waefeso 6:4, akina baba wameambiwa wasiwachokoze watoto wao. Badala wanastahili kuwalea kwa njia ya Mungu. Kumlea mtoto kwa “kumfunza na kumuonya kuhusu Mungu” yajumlisha kuzuilia, maonyo na naam adhabu ya fimbo.

English



Rudi kwa ukurasa wa nyumbani wa Kiswahili

Ni namna gani Wakristo wanastahili kuwarudi watoto wao? Bibilia inasema nini?
Shiriki ukurasa huu: Facebook icon Twitter icon Pinterest icon Email icon
© Copyright Got Questions Ministries