settings icon
share icon
Swali

Nitawezaje kuwasamehe wale wanaonikosea?

Jibu


Kila mtu amekosewa, chukizwa na tumetenda dhambi wakati mmoja. Mkristo anastahili kukabiliana namna gani wakati makosa kama hayo yametokea? Kulingana na Bibilia, tunastahili kusamehe. Waefeso 4:32 yasema, “Tena iweni wafadhili ninyi kwa ninyi, wenye huruma, mkasameheane kama na Mungu katika Kristo alivyowasamehe ninyi.” Vilevile wakolosai 3:13 yasema, “Mkichukuliana, na kusameheana, mtu akiwa na sababu ya kumlaumu mwenzake; kama Bwana alivyowasamehe ninyi, vivyo na nyinyi.” Neno kuu katika katika maandiko hayo yote mawili ni kwamba tunastahili kuwasamehe wengine vile Mungu ametusamehe. Ni kwa nini tunasamehe? Kwa sababu tumekwisha samehewa. Wale ambao sio Wakristo, ingwa hawajasemehewa na Mungu na hawana pia uwezo wa kuwasemehe wengine.

Musamaha utakuwa rahisi ikiwa tutautoa kwa wale ambao wamekuja kuuliza kwa sikitiko na toba. Bibilia yatuambia kwamba tunastahili kusamehe bila vikwazo/masharti kwa wale wanaotukosea. Kukataa kumsamehe mtu inaonyesha chuki, uchungu, na hasira, kwa hayo hakuna lenye ambalo ni tabia ya Mkristo. Katika sala ya Bwana, tunamuuliza Mungu kutusamehe makosa yetu, vile tunavyowasamehe wanaotukosea (Mathayo 6:12). Yesu alisema katika Mathayo 6:14-15, “Kwa maana mkiwasamehe watu makosa yao, na Baba yenu wa mbinguni atawasamehe ninyi. Bali msipowasamehe watu makosa yao, wala Baba yenu hatawasamehe ninyi makosa yenu.” Kwa umoja na maandiko mengine ambayo yzungumzia msamaha wa Mungu, Mathayo 6:14-15 imeeleweka kusema kuwa, watu wanaokataa kuwasamehe wengine hawajauonja msamaha wa Mungu wao wenyewe.

Popote tunapoasi amri yoyote ya Mungu, tunamkosea Mungu. Popote tunapomkosea mtu mwingine, hatumkosei huyo mtu pekee, pia twamkosea Mungu. Tunapoangalia urefu ambao Mungu anasamehe makosa yetu, tunagundua kwamba hatuna haki kuweka neema kwa wengine. Tumemkosea Mungu mara nyingi sana, zaidi ya mtu yeyote vile ametukosea. Ikiwa Mungu alitusamehe sana, tunawezaje kukataa kusamehe wengine vitu vidogo wanaotukosea? Mfano wa Yesu katika Mathayo 18:23-35 ni elezo zuri sana la mfano wa ukweli huu. Mungu anaahidi kuwa wakati tunakuja kwake kuuliza msamaha, anatusamehe (1 Yohana 1:9). Msamaha tunaoutoa haustali kuwa na mipaka, vile msamaha wa Mungu hauna mipaka (Luka 17:3-4).

English



Rudi kwa ukurasa wa nyumbani wa Kiswahili

Nitawezaje kuwasamehe wale wanaonikosea?
Shiriki ukurasa huu: Facebook icon Twitter icon Pinterest icon Email icon
© Copyright Got Questions Ministries