settings icon
share icon
Swali

Biblia inasemaje juu ya kiumbe dinosauri? Je, viumbe hawa dinosauri wamo ndani ya biblia?

Jibu


Hili ni swali linalotokana na umri wa dunia tunayoikalia. kulengana na muda unaodhaniwa viumbe hawa waliishi, hakuna mwanadamu angekuwako kuwaona wakiishi. Biblia hutaja viumbe waliokuwa wakiitwa kwa kiebrania “tannyn’ kiumbe kikubwa chenye asili ya kufanana na mamba mkubwa. Tafsiri tofauti tofauti za neno hili la kiebrania ndizo zinachangia kiumbe hiki kuitwa dinosauri. Viumbe hawa wametajwa karibu mara thelathini katika agano la kale na wanapatikana nhi kavu na ndani ya maji.

Biblia inataja viumbe wengine ambao wanaitwa behemoth. hawa hutajwa kuwa wenye nguvu kuliko viumbe wote Mungu alivyoviumba wakubwa ambao mikia yao inafananishwa na msonobari (Ayubu 40:15 na kuendelea). Dinosauri alikuwa na mkia mkubwa hivyo kustahili kufananishwa na msonobari.

Karibu kila aina ya michoro ya kizamani ya kila mahali ulimwenguni ina alama za kufanana na viumbe wakubwa wa asili ya mamba. Mabaki ya kazi za mikono ya kizamani kutoka amerika kaskazini yanaashiria kuwako kwa dinosauri.

Katika mabaki yaliyopatikana bara asia na amerika kaskazini yana alama za miguu ya wanadamu na viumbe hawa dinosauri kithibitisho cha kuwako kwa viumbe hawa dinosauri duniani.

Kwa hivyo je, mna dinosauri katika biblia? Sisi katika GotQuestions.org tunaamini yakuwa wanadamu na dinosauri waliishi wakati sawa. Tunaamini dinosauri walikufa wakati wa gharika katika siku za Nuhu na pia kwa vile walikuwa wakiwindwa sana na wanadamu.

English



Rudi kwa ukurasa wa nyumbani wa Kiswahili

Biblia inasemaje juu ya kiumbe dinosauri? Je, viumbe hawa dinosauri wamo ndani ya biblia?
Shiriki ukurasa huu: Facebook icon Twitter icon Pinterest icon Email icon
© Copyright Got Questions Ministries