settings icon
share icon
Swali

Je, ni makosa kwa Mkristo kuishi na mwenzako wa jinsia tofauti katika chumba moja?

Jibu


Je, watu wa jinsia tofauti wanaoshi katika chumba kimoja au wenza wa nyumbani wanaruhusiwa kibiblia? Hali ngumu ya kifedha na kijamii huwafanya watu wengi wasio na mume kufikiria kuishi na marafiki wa jinsia zote, walakini Wakristo kila mara hujiuliza kama hilo ni jambo la hekima.

Kwa madhumuni ya makala haya, tutarejelea “wanaoihsi chumba kimoja” kama wale wanaoshiriki nafasi moja ya kuishi lakini wanadumisha uhusiano wa kidunia usio na hisia za kimapenzi au ngono. Wanaoshiriki ngono pamoja wanakiuka amri za Mungu (1 Wakorintho 6:18). Lakini ikiwa mvulana na msichana wanafurahia ushirka wa kila mmoja wao, wana mipaka inayofaa ya kujamiiana, na wote wawili wangefaidika kwa kuishi nyumba moja au viumba vya kuishi, je, kuna amri ya kibiblia iliyo wazi dhidi yao kuishi pamoja?

Mipango ya kuishi ilikuwa tofauti wakati Biblia ilipoandikwa, kwa hiyo hakuna amri iliyo wazi kuhusu kuwa na mtu wa kuishi pamoja naye na ni wa jinsia tofauti. Hata hivyo, hiyo haimaanishi kwamba hakuna kanuni za Biblia tunazoweza kutumia. Tunapomjua Mungu na kutafuta kumpendeza, tunataka kujua zaidi ya kiwango cha chini kabisa. Tunataka kusikia kila minong’ono Yake na kutafuta kuitii.

Katika kuzingatia suala la wenza wa jinsia tofauti kuishi chumba kimoja, tunapaswa kuchunguza vifungu vifuatavyo:

1. Warumi 13:14 inasema, “Bali jivikeni Bwana Yesu Kristo, wala msifikiri jinsi mtakavyotimiza tamaa za miili yenu yenye asili ya dhambi.” “Kufikiria” kunamaanisha kuwa tunajiweka katika hali ambazo huenda mwili wetu dhaifu usiwe na nguvu za kutosha kupigana nayo. Mvulana na msichana wa umri wa miaka 14 waliolala pekee yao gizani “wakitazama sinema” wanauwezesha mwili kufanya ngono. Wamejiweka katika hali ya maelewano ambapo mihemko na kukaribiana kwao kunaweza kuwa na athari ya dhambi. Kwa hivyo, watu wawili wa jinsia tofauti ambao tayari wanafurahiana na kuelewana vizuri wanapohamia pamoja na kucheza kwa nyumba kana kwamba wamefunga ndoa, huenda wakatokeza hali ambayo haikutazamiwa. Msichana akitembea ndani ya nyumba akiwa amejifunika taulo pekee anaweza kumfanya mwenzi wake awe na tamaa zisizohitajika. Kumbatio la kufariji la kirafiki kutoka kwa mwanamume huyo wakati amekasirika linaweza kubadilika kwa urahisi sana kunawezesha hali. Swali ambalo wote wanaoishi katika chumba cha watu wa jinsia tofauti wanapaswa kujibu kwa uaminifu ni hili: je, tunaweza kuwa tunauwezesha miili kujiweka katika hali ya karibu sana kimapenzi?

2. Wakorintho wa Kwanza 10:31-33 inasema, “Basi, lolote mfanyalo, kama ni kula au kunywa, fanyeni yote kwa utukufu wa Mungu. Msiwe kikwazo kwa mtu yeyote, wawe Wayahudi au Wayunani, au kwa kanisa la Mungu, kama hata mimi ninavyojaribu kumpendeza kila mtu kwa kila namna. Kwa maana sitafuti mema kwa ajili yangu mwenyewe bali kwa ajili ya wengi, ili waweze kuokolewa.” Hii ni mojawapo ya vifungu vinavyoainisha mwili, Mkristo mchanga kutoka kwa wale wanaonuia kumweshimu Mungu. Vifungu hivi hutupa uhuru wa kujizuia, sio kwa orodha ya yale tunapaswa kufanya au hatupaswi kufanya, bali kwa ile sharia ya uhuru (Yakobo 2:12). “Kutoa tetezi” ni kuwa kizuizi; kwamba, unamzuia mtu katika mwenendo wao na Mungu. Maswali ya kawaida tunayopaswa kuambatanisha ni haya: kwa kuwa na rafiki wa jinsia tofauti chumba kimoja, ninaweza kuwa ninamzuia mtu katika mwenendo wao na Mungu? Ninaweza kuwa “ninawakwaza” watu wa familia, marafiki zetu Wakristo, au walezi wetu? Je, tunamtukuza Mungu kwa kuishi pamoja na mtu wa jinsia tofauti katika chumba kimoja?

3. Onyo kali zaidi kuhusu makosa iliyotolewa na Yesu katika Luka 17:1: “Mambo yanayosababisha watu watende dhambi hayana budi kutukia. Lakini ole wake mtu yule anayeyasababisha.” Mungu huchukulia kwa uzito sana mtu anapomfanya asiyeamini au mtoto mchanga katika Ukristo kugeuka kutoka ukweli na kukiuka dhamiri yake, nasi tunapaswa kuichukulia kwa uzito pia. Mungu anatuwajibisha kuweka mipaka ya uhuru wetu ili tusiwafanye wengine wajikwae wanapoelekea kwa Yesu. Kwa hiyo swali la wazi la kujiuliza ni hili: Je, kumchukua rafiki wa jinsia tofauti kuishi naye chumba kimoja kunaweza kupunguza ufanisi wangu kama shahidi wa Kikristo?

4. Wathesalonike wa Kwanza 5:22 inasema, “Jiepusheni na uovu wa kila namna.” Tafsiri zingine hutumia umbo la neno au fadhili badala ya sura, lakini maana ya msingi ya mstari huo ni sawa. Hili ni onyo la kuepuka maovu kabisa. Tukiwa na ufahamu wa ushuhuda wetu kwa ulimwengu na wajibu wetu wa kutegemeza waumini wenzetu, tunakaa mbali na chochote ambacho hata kinaonekana kuwa cha dhambi. Tuseme mtu anatembea kwenye ukingo wa mwamba, akidhani kwamba hataanguka kando. Lakini dhana hiyo ni ya kipumbavu kwa sababu inategemea mambo asiyoweza kuyadhibiti, kama vile upepo mkali, hitilafu za viatu, kizunguzungu, na telezi za mwamba. Wathesalonike wa Kwanza 5:22 inatuagiza kujiweka mbali na ukingo wa jabali ili tusiangushwe na mambo yaliyo nje ya uzoefu au matarajio yetu. Tunapaswa kufahamu mielekeo yetu wenyewe kuelekea dhambi. Badala ya kuchezea mambo yanayoweza kutufanya tutende dhambi, tunapaswa kuchukua hatua za kuzuia ili kuepuka dhambi. Maswali tunayopaswa kujiuliza na je, kunalo jambo lolote kuhusu kuishi kwa pamoja kwa watu wa jinsia tofauti ambalo lina sura ya uovu? Je, watu ambao hawatujui vizuri watafikiri kwamba tunaishi katika dhambi ya ngono—na je, hilo litazuia katika kushuhudia kwetu?

Kwa wale wanaokiri imani katika Kristo, maamuzi ya mtindo wa maisha mara nyingi huonyesha uhalali wa taaluma hiyo. Utamaduni huzungumza kwa sauti kubwa, lakini daima imekuwa hivyo. Waumini husikia sauti za Utamaduni na Sababu na Mafanikio, lakini wanashikamana zaidi na sauti ya Mungu katika maisha yao. Yeus ametuita kutoka katika tamaduni, kuishi maisha ya ajabu yaliyojaa kujisalimisha, mapambano, na kujitolea (Mathayo 10:34-39; Warumi 12:1-2). Tunapomwomba atawale maisha yetu, basikila kitu tunachofanya lazima kipite kiwango chake. Hakubaliani kwa sababu amaepta itikio letu katika maamuzi yetu. Ubwana sio demokrasia. Labda Yeye ndiye Bwana, au sisi (Luka 16:13). Tunapokubaliwa na hali zisizoeleweka, bado tunaweza kupata majibu katika Neno Lake ikiwa kweli tunataka kuyapata.

English



Rudi kwa ukurasa wa nyumbani wa Kiswahili

Je, ni makosa kwa Mkristo kuishi na mwenzako wa jinsia tofauti katika chumba moja?
Shiriki ukurasa huu: Facebook icon Twitter icon Pinterest icon Email icon
© Copyright Got Questions Ministries