settings icon
share icon
Swali

Ikiwa kuzaliwa upya katika mwili mwingine sio kweli, ni kwa nini watu wengine hukumbuka maisha yao ya zamani?

Jibu


Ingawa Biblia haizungumzii kuhusu kuzaliwa upya katika umbo lingine hasa, ni wazi kwamba mtindo wa kibiblia wa maisha, kifo, na maisha baada ya kifo haupatani na aina yoyote ya kuzaliwa upya katika mwili kama ilivyowekwa katika dini kama vile Uhindu, Ubuddha, na Enzi Mpya, au imani Mamboleo ya Kipagani. Katika Waebrania 9:27-28, tunaambiwa kwamba “Kama vile mwanadamu alivyowekewa kufa mara moja tu na baada ya kufa akabili hukumu, vivyo hivyo Kristo alitolewa mara moja tu kuwa dhabihu ili azichukue dhambi za watu wengi. Naye atakuja mara ya pili, sio kuchukua dhambi, bali kuwaletea wokovu wale wanaomngoja kwa shauku.” Kifungu hiki pekee kinaonekana kuondoa uwezekano wa kukumbuka maisha ya zamani/kuzaliwa upya.

Pamoja na mistari hiyo hiyo, katika Luka 23:43 Yesu anamwambia mwizi msalabani kwamba atakuwa pamoja Naye katika paradiso siku hiyo hiyo, ambayo inafikiri kwamba mtu huyo hatazaliwa upya katika maisha ya duniani. Vile vile, vifungu kama vile Yakobo 4:14, vinavyojadili asili ya muda ya maisha ya mwanadamu, haviendani na wazo la kuzaliwa upya katika mwili wa kuishi maisha ya kidunia tena na tena kwa karne nyingi milenia, au umilele wote. Juu ya hayo yote, ikiwa nafsi za wanadamu zilifanywa upya tena na tena, basi watu fulani katika Biblia wangewezaje kuona roho za watu waliokufa muda mrefu, kama vile Musa alivyoonwa na mitume katika Mathayo 17:3 katika wakati wa kugeuka sura kwa Kristo?

Tunapaswa kufanya nini kwa wale wanaodai kuwa wana kumbukumbu za maisha yao ya zamani/uzoefu wa kuzaliwa upya? Sawali la kwanza na labda muhimu ziadi tunalopaswa kuuliza ni kama “kumbukumbu” hizi ni za kweli au la. Kumbukumbu ya binadamu inajulikana kuwa haiwezi kutegemewa (uliza tu wakili au mpelelezi yeyote), na mara kwa mara watu hukumbuka mambo vibaya, wakiamini kwamba wanakumbuka mambo ambayo hayajawahi kutokea au kutokumbuka mambo yaliyotokea. Kwa wale wanaodai kukumbuka maisha yao ya zamani, mtu anaweza kuwawazia kwa urahisi wakikumbuka vibaya piach za pindi vya runinga au sinema, mawazo ya kiakili kutoka katika vitabu walivyoosoma miaka ya mapema, au kupotosha ndoto kwa ajili ya kumbukumbu za kweli. Tunawezaje kujua kwa uhakika kwamba kumbukumbu zao za maisha ya zamani si mojawapo ya mambo haya? Je, ni jambo la akili kudhani kwamba kumbukumbu zao ni za maisha ya zamani badala ya mojawapo ya mambo haya mengine? Wakati baadhi ya “wataalam wa maisha ya zamani” wanadai kupata ushindi wa kuzaliwa upya kwa kuunganisha vitu kama vile woga na magonjwa ya kimwili kwa watu wanaoishi sasa na matuko ya kiwewe katika maisha ya zamani, “wataalam” wa maisha ya zamani wanafikiri kuwepo kwa maisha ya zamani (au maisha ya kale) katika kueleza matatizo ya sasa ya afya, bila kuonyesha kwamba maisha hayo ya zamani yalitokea kweli.

Ukweli wa mambo ni kwamba hakuna ushahidi thabiti, unaokubalika kisayansi kwamba kumbukumbu za maisha ya zamani yanayodaiwa na baadhi ya watu ni ya kweli, badala ya matukio ya kumbukumbu mbaya au sadiki zilizoundwa. Hatimaye, swali huibuka, ikiwa tutapata ukweli katika akili zisizotegemeka na kumbukumbu za wanadamu walioanguka na wanaotenda dhambi au kutoka kwa Neno takatifu la Mungu lipitalo nyakati zote. Wakristo wanaweza kusisitiza kwa uhakika kwamba kuzaliwa upya katika umbo jingine si jambo linalowezekana kwa nafsi ya mwanadamu; maisha haya yanapoisha, umilele wetu katika maisha ya baadaye huanza.

English



Rudi kwa ukurasa wa nyumbani wa Kiswahili

Ikiwa kuzaliwa upya katika mwili mwingine sio kweli, ni kwa nini watu wengine hukumbuka maisha yao ya zamani?
Shiriki ukurasa huu: Facebook icon Twitter icon Pinterest icon Email icon
© Copyright Got Questions Ministries