settings icon
share icon
Swali

Inamaanisha nini kuomba, “Mapenzi yako yatimizwe”?

Jibu


“Mapenzi yako yatimizwe” ni mojawapo ya ombi katika Sala ya Bwana. Kwa sehemu, Yesu aliwafundisha wanafunzi Wake kusali, “Hivi basi, ndivyo iwapasavyo kuomba: “Baba yetu uliye mbinguni, Jina lako litukuzwe. Ufalme wako uje. Mapenzi yako yafanyike hapa duniani kama huko mbinguni” (Mathayo 6:9-10). Yesu mwenyewe alisihi mapenzi ya Mungu yafanyike katika bustani ya Gethsemane. Kable ya kusulubishwa kwake, aliomba, “Baba yangu, kama inawezekana, kikombe hiki na kiniondokee. Lakini si kama nipendavyo mimi, bali kama upendavyo wewe” (Mathayo 26:39). Yesu alijitolea kuona mapenzi ya Mungu yakitimizwa, na sala “Mapenzi yako yafanyike” ilikuwa kichwa kikuu cha maisha yake.

Kuomba kwa urahisi, “Mapenzi yako yatimizwe,” ni kumwomba Mungu afanye anachotaka. Bila shaka, tunasali kwa Mungu aliyesema, “Hebu na kuwe na nuru,” nayo nuru ikawepo (Mwanzo 1:3), kwa hivyo tunajua kwamba agizo lake kuu litatimizwa, iwe tunaomba au la. Lakini kuna kipengele kingine cha mapenzi ya Mungu, ambacho tanakiita mapenzi Yake “yaliyofunuliwa” au mapenzi “ya maagizo”. Haya ni “mapenzi” ya Mungu ambayo Ametufunulia lakini hayalazimishi kwetu. Kwa mfano, ni mapenzi ya Mungu kwamba tuongee ukweli kwa upendo (Waefeso 4:15) na kwamba tusifanye uzinzi (1 Wakorintho 6:18) au kulewa (Waefeso 5:18). Tunapoomba, “Mapenzi yako yatimizwe,” tunamwomba Mungu aongeze haki ulimwenguni kuwaleta watu wengi zaidi kwenye toba, na kuendeleza kazi ya ufalme wa Mwanawe.

Tunaposali, “Mapenzi yako yatimizwe,” tunakiri kwamba Mungu ana haki ya kutawala. Hatuombi, “Mapenzi yangu yatimizwe”; tunaomba, “Mapenzi yako yatimizwe.” Tukiomba kwamba mapenzi ya Mungu yatimizwe ni onyesho la tumaini letu kwamba Yeye anajua lililo bora zaidi. Na kauli ya kunyenyekea njia za Mungu na mipango yake. Tunaomba mapenzi yetu yafanane na Yake.

Sala ya Bwana inaanza kwa kumtambua Mungu kama Baba wa mbinguni. Kisha Yesu anakua kielelezo cha ombi, akiwasilisha maombi matatu kwa Baba: 1) Kwamba Mungu atalifanya jina Lake litukuzwe; kwa maneno mengine, kama mwandishi mmoja alivyosema, kwamba Mungu angetenda kwa njia ambayo inadhihirisha utakatifu wake an utukufu wake (The Prayer That Turns the World Upside Down: The Lord’s Prayer as a Manifesto for Revolution, p. 61). 2) Kwamba Mungu ataleta ufalme wake duniani; yaani, mahubiri ya injili yangewageuza wenye dhambi kuwa watakatifu wanaotembea katika nguvu za Roho Mtakatifu na kwamba Mungu angeondoa uovu duniani na kuumba mbingu mpya na dunia mpya ambapo Mungu atakaa pamoja na watu wake na kusiwe na laana tena na hakuna kifo tena (ona Ufunuo 21-22). 3) Kwamba mapenzi ya Mungu yatafanyika “hapa duniani kama huko mbinguni” (Mathayo 6:10. Kule mbinguni, malaika wanatekeleza mapenzi ya Mungu kikamilifu, kwa shangwe, na papo hapo-huo ungekuwa ulimwengu ulioje ikiwa wanadamu wangetenda hivyo!

Kama jambo la ufafanuzi, “Mapenzi Yako yatimizwe” sio maombi ya kujiuzulu ya kupita kiasi. Maombi ya Yesu katika Gethsemane hayakuwa ya kupita au kutabiri hata kidogo; Aliweka moyo Wake mbele ya Baba na kufunua shauku Yake kuu: kwa mapenzi ya Mungu kutimizwa. Kusali, “Mapenzi yako yatimizwe,” hukubali kwamba Mungu ana ujuzi zaidi kutuliko sisi na kwamba tunaamini kwamba njia Yake ndiyo bora zaidi. Na ni kujitolea kufanya kazi kwa bidii ili kuendeleza utekelezaji wa mapenzi ya Mungu.

Warumi 12:1-2, “Kwa hiyo, ndugu zangu, nawasihi kwa rehema zake Mungu, itoeni miili yenu iwe dhabihu iliyo hai, takatifu na inayompendeza Mungu, hii ndiyo ibada yenu yenye maana. Msifuatishe tena mfano wa ulimwengu huu, bali mgeuzwe kwa kufanywa upya nia zenu. Ndipo mtaweza kuonja na kuhakikisha ni nini mapenzi ya Mungu yaliyo mema, yanayopendeza machoni pake na ukamilifu.” Kuelewa Mungu ni nani, tutajinyenyekeza Kwake na kumuruhus atubadilishe. Kadri tunavyomjua Mungu zaidi, ndivyo maombi yetu yatakavyopatana kwa urahisi na mapenzi Yake na tunaweza kuomba kwa kweli, “Mapenzi yako yatimizwe.” Tunaweza kumwendea Mungu kwa uhakika kwamba “tukiomba kitu sawasawa na mapenzi yake, atusikia” (1Yohana 5:14-15).

Kwa imani, tunajua kwamba kuomba, “Mapenzi yako yatimizwe,” ndilo jambo bora tunaloweza kuomba. “Basi kwa yeye awezaye kutenda mambo ya ajabu yasiyopimika kuliko yote tuyaombayo au tuyawazayo, kwa kadiri ya uweza wake ule utendao kazi ndani yetu, yeye atukuzwe katika kanisa na katika Kristo Yesu kwa vizazi vyote, milele na milele. Amen” (Waefeso 3:20-21).

English



Rudi kwa ukurasa wa nyumbani wa Kiswahili

Inamaanisha nini kuomba, “Mapenzi yako yatimizwe”?
Shiriki ukurasa huu: Facebook icon Twitter icon Pinterest icon Email icon
© Copyright Got Questions Ministries