settings icon
share icon
Swali

Biblia inasema kuhusu ni nini tunastahili kufanya mtoto mkaidi?

Jibu


Mtoto ambaye anaonyesho tabia ya ukatili anaweza fanya hivyo kwa sababu mbalimbali. Ukali, kutopendwa, na ulezi wa matatizo kwa karibu daima utasababisha ukatili wa aina fulani. Hata mtoto mtiifu zaidi atakatili aidha kwa undani au wazi-dhidi ya ulezi kama huo. Kwa kawaida, aina hii ya uzazi unapaswa kuepukwa. Aidha, kiasi fulani cha uasi dhidi ya wazazi ni asili katika vijana ambao wanaojitenga polepole mbali na familia zao katika mchakato wa kuanzisha maisha na utambulisho wao wenyewe.

Chukulia kwamba mtoto mkatili kwa kawaida ana nafsi ya utu ya nguvu, atakuwa na sifa ya mwelekeo wa kupima mipaka, tamaa kuu ya kudhibiti, na ahadi ya kupinga mamlaka yote. Kwa maneno mengine, ukali ni jina lake la katikati. Aidha, watoto hawa wa nafsi ya nguvu mara nyingi huwa wenye akili sana na anaweza "kufikiri" hali kwa kasi sana, kutafuta njia ya kuchukua udhibiti wa mazingira na watu wa karibu nao. Watoto hawa wanaweza kuwa wa majaribu ya kuchosha sana.

Kwa bahati nzuri, pia ni kweli kwamba Mungu aliwaumba watoto jinsi na vile walivyo. Anawapenda, na hawaacha wazazi bila rasilimali mbinu za kukabiliana na changamoto. Kuna kanuni za kibiblia ambazo hushughulikia kukabiliana na waasi, mtoto aliye na nafsi ya nguvu kwa neema. Kwanza, Mithali 22:6 inatuambia na "Mlee motto katika njia impasayo, naye hataiacha, hata akatakpokuwa mzee" Kwa watoto wote, njia wanapaswa kufuata ni ya Mungu. Kufundisha watoto katika neno la Mungu ni muhimu kwa watoto wote, ambao ni lazima waelewe Mungu ni nani na njia bora ya kumtumikia. Kwa mtoto aliye na nafsi gumu, kuelewa ni nini kinamfanya kuwa hivyo-hamu kwa ajili ya kutawala-itachukua mda mrefu kumsaidia kujua "njia" yake. Mtoto mkatili ndiye ambaye anapaswa kuelewa hatawali duniani bali ni Mungu ni-na kwamba yeye tu lazima afanye mambo kwa njia ya Mungu. Hii inahitaji wazazi kuamini kabisa ukweli huu na kuishi ipasavyo. Mzazi ambaye yeye mwenyewe ni mkatili dhidi ya Mungu hawezi kuwa na uwezo wa kuwashawishi mtoto wake kuwa mtiifu.

Pindu tu tunajua kwamba Mungu ndiye hufanya sheria, wazazi lazima wayaweke hayo katika akili ya mtoto kwamba wao ni vyombo vya Mungu na kufanya kitu chochote na kila kitu muhimu kutekeleza mpango wa Mungu kwa familia zao. Mtoto katili lazima afundishwe kwamba mpango wa Mungu wazazi kuongoza na mtoto kufuata. Hakutakuwa na udhaifu juu ya hatua hii. Mtoto mwenye nafsi ngumu kwa kutofikiria anaweza ona nafasi kwa mbali na kurukia nafasi hiyo iliyo tupu na kuchukua udhibiti. Kanuni ya kujiwasilisha kwa mamlaka ni muhimu kwa motto aliye na nafsi ngumu. Kama kunyenyekea hakukusomwa katika utoto, baadaye itakuwa na sifa ya migogoro na mamlaka yote, ikiwa ni pamoja na waajiri, polisi, mahakama, na viongozi wa kijeshi. Warumi 13:1-5 ii wazi kwamba mamlaka tulio chini yake yamewekwa Mungu, na sisi ni kunyenyekea kwao.

Pia, mtoto mwney nafsi ngumu ataitikia sheria kwa hiari tu ikiwa sheria au amri sitakuwa za maana kwake. Mpe sababu imara ya utawala, mara kwa mara akielezea ukweli kwamba lazima tufanye mambo kwa njia ambayo Mungu anataka yafanyike na kwamba kweli hi sio ya kupingwa. Mweleze kwamba Mungu amewapa wazazi wajibu wa kuwapenda na kuwapa nidhamu watoto wao na kwamba kushindwa kufanya hivyo watakuwa wanaasi Mungu. Kila inapowezekana, hata hivyo, mpe fursa mtoto kusaidia kufanya maamuzi ili yeye asijione kuwa hana nguvu kabisa. Kwa mfano, kwenda kanisani sio jambo la kuhojiana sababu Mungu ametuamuru kukusanya pamoja na waumini wengine (Waebrania 10:25), lakini watoto wanaweza kuwa na usemi (ndani ya sababu) juu ya kile watavaa, mahali ambapo familia itakaa, nk Wape miradi ambayo wanaweza kutoa mchango kama vile mipango ya likizo ya familia.

Zaidi ya hayo, uzazi lazima ufanyike kwa uthabiti na uvumilivu. Wazazi lazima wajaribu wasiinue sauti zao au kuinua mikono yao katika hasira au kupoteza upole wao. Hii itampa fursa mtoto mwenye nafsi ngumu hali ya kutaka kudhibiti yeye anatamani kuwa nayo, ile kwa haraka yeye hufikiri jinsi ya kukudhibiti kwa kukukasirisha kwango cha kukufanya kuguswa kihisia. Nidhamu ya kimwili mara nyingi sio ya manufaa kwa watoto kama hawa kwa sababu wao hufurahia kusukuma wazazi hatua ya kukwasika kiasi kwamba wanahisi maumivu kidogo ni gharama ya thamani kulipa. Wazazi walio na wototo wa nafsi ngumu mara nyingi husema kuwa mtoto anawacheka wakati wanamchapa, hivyo kiboko hakiwezi kuwa njia bora yao ya nidhamu. Labda hamna mahali katika maisha matunda ya Kikristo ya Roho ya uvumilivu katika (Wagalatia 5:23) yanahitajika zaidi kuliko kwa mtoto mwenye nafsi ngumu au mkatili.

Haijalishi ni ya kuchoshanamna gani kulea watoto hawa inaweza kuwa, wazazi wanaweza kuchukua faraja katika ahadi ya Mungu kuwa hawezi kutujaribu zaidi ya uwezo wetu kuvumilia (1 Wakorintho 10:13). Kama Mungu anawapa mtoto nafsi ngumu , wazazi wanaweza kuwa na uhakika Yeye hajafanya makosa na atatoa ushauri na rasilimali wanahitaji kufanya kazi. Labda hamna mahali katika maisha ya mzazi maneno "kuomba bila kukoma" (1 Wathesalonike 5:17) yatakua na maana zaidi kuliko kuwa na mtoto aliye na nafsi ngumu. Wazazi wa watoto hawa watatumia muda wao mwingi katika magoti yao mbele za Bwana kuuliza hekima, ambayo ameahidi kutoa (Yakobo 1:5). Hatimaye, kuna faraja katika kujua kwamba watoto weneye nafsi ngumu ambao wamefunzwa vizuri mara nyingi hukua na kuwa wenye unawili wa juu, watu wazima na wa mafanikio. Watoto wengi wakatilii wamegeuka kuwa wajasiri, Wakristo wenye bidii ambao wanatumia vipaji vyao vikubwa kumtumikia Bwana wao wamekuja kwa upendo na heshima kupitia kwa juhudi za uvumilivu wao na wazazi wa bidii.

English



Rudi kwa ukurasa wa nyumbani wa Kiswahili

Biblia inasema kuhusu ni nini tunastahili kufanya mtoto mkaidi?
Shiriki ukurasa huu: Facebook icon Twitter icon Pinterest icon Email icon
© Copyright Got Questions Ministries