settings icon
share icon
Swali

Mwiba katika mwili wa Paulo ulikuwa nini?

Jibu


Maelezo yasiyohesabika kuhusu asili ya mwiba wa Paulo katika mwili yametolewa.Yanaanzia kutoka kwa majaribu ya kujamiana, wapinzani kakamavu,maradhi ya kudumu (kama vile matatizo ya jicho, malaria, kipandauso cha maumivu ya kichwa, na kifafa), kwa ulemavu wa hotuba. Hakuna mtu anayeweza kusema kwa uhakika mwiba katika mwili wa paulo ulikuwa nini, lakini pengine ulikuwa mateso ya kimwili.

Tunachojua kuhusu mwiba huu katika mwili linatokana na Paulo mwenyewe katika 2 Wakorintho 12: 7: "Na makusudi nisipate kujivuna kupita kiasi, kwa wingi wa mafunuo hayo nalipewa mwiba katka mwili, mjumbe wa Shetani ili anipige, nisije nikajivuna kupita kiasi. " Kwanza, madhumuni ya mwiba katika mwili ilikuwa kuweka Paulo awe mnyenyekevu. Mtu yeyote ambaye alikutana na Yesu na aliongelezwa na kupewa kibali cha cheo naye (Matendo 9: 2-8) ingekuwa, katika hali yake ya asili, kuwa "wenye kujivuna."ongeza kwa hilo ukweli kwamba kuwa ukiongozwa na Roho Mtakatifu kuandika mengi ya Agano Jipya, na ni rahisi kuona jinsi Paulo angeweza kuwa " mwenye kiburi" (KJV) au "kusifiwa kupita kiwango" (NKJV) au "mwenye majivuno mno " (NCV). Pili, tunajua kwamba dhiki ilikuja kutoka au kwa mjumbe wa Shetani. Tu kama Mungu alimruhusu Shetani amuadhibu Ayubu (Ayubu 1: 1-12), Mungu alimruhusu Shetani amuadhibu Paulo kwa malengo mema ya Mungu mwenyewe na daima ndani ya mapenzi kamili ya Mungu.

Inaeleweka kwamba Paulo angeweza kufikiria mwiba huu kuwa kizuizi kwa huduma pana au ufanisi zaidi (Wagalatia 5: 14-16) na kwamba kwa mara tatu angeomba dua kwa Mungu kwa ajili ya kuiondoa (2 Wakorintho 12: 8). Lakini Paulo alijifunza kutokana na funzo hili ambayo inatawala maandishi yake: Lakini tuna hazina hii katika vyombo vya udongo, ili adhdama kuu ya uwezo iwe ya Mungu, wala si kutoka kwetu. (2 Wakorintho 4: 7) ili kwamba Mungu peke yake asifiwe (2 Wakorintho 10:17).”Lakini, yeye ajisifuye, na ajisifu katika Bwana.” Badala ya kuondoa tatizo, Mungu alimpa neema na nguvu kwa njia hiyo, na alitangaza kwamba neema ilitosha."

English



Rudi kwa ukurasa wa nyumbani wa Kiswahili

Mwiba katika mwili wa Paulo ulikuwa nini?
Shiriki ukurasa huu: Facebook icon Twitter icon Pinterest icon Email icon
© Copyright Got Questions Ministries