settings icon
share icon
Swali

Je, Biblia inasema tuombe kwa ajili ya amani ya Yerusalemu?

Jibu


Mungu anatuambia tuombe kwa ajili ya amani ya Yerusalemu katika Zaburi 122: 6-9: “Omba kwa ajili ya amani ya Yerusalemu: “Wote wakupendao na wawe salama. Amani na iwepo ndani ya kuta zako

na usalama ndani ya ngome zako.”Kwa ajili ya ndugu zangu na marafiki, nitasema, “Amani iwe ndani yako.” Kwa ajili ya nyumba ya Bwana Mungu wetu, nitatafuta mafanikio yako.” Mungu aliahidi baraka kwa wale wanaoibariki Israeli na laana juu ya wale wanaoilaani (Mwanzo 12:3), na kwa kuwa Yerusalemu inadhihirishwa kuwa kitovu cha maisha ya Kiyahudi, basi wale wote wanaoimbea amani na usalama nao pia watepewa amani.

Kuomba kwa ajili ya amani ya Yeruslamu kunafaa zaidi kwa jiji ambalo jina lake kihalisi linamaanisha “amani” na ambao ni makazi ya Mungu wa amani. Maneno “Amani iwe juu ya Israeli” yanapatikana pia mwishoni mwa Zaburi 125:5 na 128:6, kuonyesha kwamba ilikuwa kawaida ya kuaga kwa baraka. Zaidi ya hayo, tukio la ujio wa Kristo itakuwa Yerusalemu (Matendo 1:11; Zekaria 14:4), na wakati huo ataweka amani ya kudumu pamoja na kuta zake. Wakristo wote wanapaswa kungojea kwa hamu kurudi Kwake na kusali kwa ajili ya wakati ambapo Mfalme wa Amani atatawala Yerusalemu.

Yesu pia alisema kwamba tunapaswa kuwa wapatanishi wa amani, jambo ambalo litahusisha kuomba kwa ajili ya amani. “Heri walio wapatanishi, maana hao wataitwa wana wa Mungu” (Mathayo 5:9). Na tunaamrishwa kufanya tuwezavyo ili kuishi kwa amani na wengine. “Kama ikiwezekana, kwa upande wenu kaeni kwa amani na watu wote” (Warumi 12:18). Kwa hivyo, Mungu anatutaka tutafute amani kati ya watu wote, na hiyo inajumuisha kuombea Yerusalemu amani, hasa kwa sababu ya nafasi yake ya kipekee moyoni Mwake.

English



Rudi kwa ukurasa wa nyumbani wa Kiswahili

Je, Biblia inasema tuombe kwa ajili ya amani ya Yerusalemu?
Shiriki ukurasa huu: Facebook icon Twitter icon Pinterest icon Email icon
© Copyright Got Questions Ministries