settings icon
share icon
Swali

Sala kimya - ni ya kibiblia

Jibu


Biblia inaweza kosa kutaja kuomba kwa kimya, lakini hiyo haina maana kuwa sio ya halali kuliko kuomba kwa sauti. Mungu anaweza kusikia mawazo yetu kwa urahisi vile vile asikiavyo maneno yetu ( Zaburi 139:23; Yeremia 12:3). Yesu alijua mawazo mabaya ya Mafarisayo (Mathayo 12:24-26, Luka 11:7). Hakuna chenye sisi hufanya, kusema, au kufikiri ni siri kutoka kwa Mungu, ambaye hana haja ya kusikia maneno yetu ya kujua mawazo yetu. Yeye anazipta sala zote zilizo elekezwa kwake, hata kama zimetajwa au hasijasemwa.

Biblia pia inataja kuomba kisiri (Mathayo 6:6). Nini itakuwa tofauti kati ya kuomba kwa sauti au polepole kama uko peke yako? Kuna baadhi ya mazingira ambapo sala ya kimya ni sahihi, kwa mfano, kuomba kwa ajili ya kitu kati yako na Mungu, kuombea mtu ambaye ako hapo, nk hakuna kitu kibaya na kuomba kimya kimya, kwa muda mrefu ili mradhi tu kama hatufanyi hivyo kwa sababu tunaona aibu kuonekana kuomba.

Labda mstari bora unaaonyesha uhalali wa maombi ambayo hayakusemwa kwa sauti ni 1 Wathesalonike 5:17: "Ombeni bila kukoma." Kwa kuomba bila kukoma ni wazi hakuwezi maanisha kuwa tunaomba kwa sauti wakati wote. Badala yake, ina maana kuwa tunapaswa kuwa katika hali ya fahamu ya kiungu mara kwa mara - ambapo sisi huchukua kila wazo mateka kwake (2 Wakorintho 10:5) na kuleta kila hali, mpango, hofu, au wasiwasi mbele ya kiti chake cha enzi. Sehemu ya sala isiyo koma itakuwa maombi ambayo yanatajwa, yaliyo semwa kwa souti ya chini, pasa sauti, imbwa, na kimya tunapoelekeza mawazo yetu ya sifa, dua, na shukrani kwa Mungu.

English



Rudi kwa ukurasa wa nyumbani wa Kiswahili

Sala kimya ni nini?
Shiriki ukurasa huu: Facebook icon Twitter icon Pinterest icon Email icon
© Copyright Got Questions Ministries