settings icon
share icon
Swali

Shetan ni nani?

Jibu


Imani ya watu kuhusu shetani huwa tofauti kutoka kutojua hadi upotovu kutokana kwa kijana mdogo mwekundu aliye na pembe anaketi juu ya mabega yako akikusii utende dhambi, ni elezolimetolewa likitambulisha jinsi dhambi simehuishwa. Bibilia ingawa inatupa picha kamili vile Shetani alivyo na vile anavyo shawishi maisha yetu. Lakini kwa uchache, Bibilia inamfafanua Shetani kama malaika aliyeanguka kutoka kwa nafasi yake mbinguni kwa sababu ya dhambi na sasa anampinga Mungu, akifanya juhudi zake ili ageuze mapenzi ya Mungu.

Shetani aliumbwa malaika mtakatifu. Isaya 14:12 inampa Shetani jina kabla aanguke kuwa nyota ya alfajiri. Ezekieli 28:12-14 inamwelezea Shetani kuwa, aliumbwa awe kerubi, kawaida mlaika mkuu. Aligeuka na kuwa mkali kwa ajili ya urembo wake na cheo chake na akaamua kuwa aketi kwenye kiti kilicho juu ya Mungu (Isaya 14:13-14; Ezekieli 28:15; 1 Timotheo 3:6). Kiburi cha Shetani kilimfanya aanguke. Kumbuka usemi wa wengi “nita” katika Isaya 14:12-15. Kwa sababu ya dhambi zake, Mungu alimfukuza Shetani kutoka mbinguni.

Shetani akawa kiongozi wa ulimwengu na mfalme wa anga (Yohana 12:31; 1 Wathesalonike 3:5), na mwongo (Mwanzo 3; 2 Wakorintho 4:4; Ufunuo Wa Yohana 20:3). Jina lake linamaanisha Mwenye “majanga” au “mpingamizi.” Majina yake mengine ni, Ibilisi kumaanisha “mdanganyaji.”

Hata kama alifukuzwa kutoka mbinguni, bado anazidi kuinua kiti chake juu ya Mungu. Anayageuza yale Mungu anayafanya, akitumaini kuabudiwa na ulimwengu na anatia tumaini kwa pingamizi zote za ufalme wa Mungu. Shetani ndiye ako nyuma ya dini zote za uongo na dini za dunia. Shetani atafanya na kila kitu katika uwezo wake ili ampinge Mungu na wale wote wanaomfuata. Ingawa hatima ya Shetani imewekwa muhuri kuwa tanuru la moto milele (Ufunuo Wa Yohana 20:10).

English



Rudi kwa ukurasa wa nyumbani wa Kiswahili

Shetan ni nani?
Shiriki ukurasa huu: Facebook icon Twitter icon Pinterest icon Email icon
© Copyright Got Questions Ministries