settings icon
share icon
Swali

Uyahudi ni nini na Wayahudi wanaamini nini?

Jibu


Uyahudi ni nini, na ni nini au nani Myahudi? Je, Ni Uyahudi dini tu? Je, ni utambulisho wa kiutamaduni au kabila? Je! Wayahudi koo za watu au ni taifa? Je, Wayahudi wanaamini nini, na wao wote wanaamini mambo sawa?

Ufafanuzi wa kamusi wa "Myahudi" pamoja na "mwanachama wa kabila la Yuda," "Msraeli," "mwanachama wa taifa lililopo katika Palestina kutoka karne ya 6 BC kwa karne ya 1 A.D, " "ni uendelezo binafsi kupitia ukoo au uongofu wa watu wa kale kuwa Wayahudi, "na" mtu ambaye dini yake ni ya Kiyahudi."

Kwa mujibu wa marabi Wayahudi, Myahudi ni yule ambaye ana mama Myahudi au mtu ambaye rasmi hubadilishwa kwa Uyahudi. Mambo ya Walawi 24:10 mara nyingi inachukuliwa kuupa uaminifu huu imani, ingawa Torati huifanyi madai maalum kwa msaada wa mila hii. Baadhi ya wanazuoni husema kwamba haina uhusiano wowote na kile mtu anaamini. Wanazuoni hawa hutuambia kwamba Myahudi hana haja ya kuwa mfuasi wa sheria na desturi ili achukuliwe kuwa Myahudi. Kwa kweli, Myahudi hawezi kuwa na imani katika Mungu wakati wote na bado kuwa Myahudi kwa misingi ya tafsiri ya marabi hapo juu.

Wanazuoni wengine hufanya wazi kwamba kama mtu afuatavyo maagizo ya Torati na anakubali "kanuni kumi na tatu za Imani" ya Maimondes (Mwalimu Moshe ben Maimon, mmoja wa Wayahudi wasomi wakubwa wa kipindi), hawezi kuwa Myahudi. Ingawa mtu huyu anaweza kuwa "kibiolojia" Myahudi, hana uhusiano halisi na Wayahudi.

Katika Torati-vitabu vitano vya kwanza vitano katika Biblia Mwanzo 14:13 inafundisha kuwa Abramu, kawaida anayetambuliwa kama Myahudi wa kwanza, alikuwa kama ilivyoelezwa "Kiebrania." Jina "Myahudi" linatokana na jina la Yuda, mmoja wa wana kumi na wawili wa Yakobo na mmoja wa makabila kumi na mawili ya Israeli. Inavyoonekana jina "Myahudi" awali lilijulikana tu kwa wale ambao walikuwa wanachama wa kabila la Yuda, lakini wakati ufalme uligawanyika baada ya utawala wa Sulemani (1 Wafalme 12), neno lilimaanisha mtu yeyote katika ufalme wa Yuda, ambayo ni pamoja na kabila la Yuda, Benjamin, na Lawi. Leo hii, wengi wanaamini kwamba Myahudi ni mtu yeyote ambaye ana uzao wa kimwili na Ibrahimu, na Isaka, na Yakobo, bila ya kujali makabila ya awali kumi na mbili anapotoka.

Hivyo, ni nini ambacho Wayahudi wanaamini, na ni maagizo gani ya msingi ya dini ya Kiyahudi? Kuna aina kuu tano au madhehebu ya dini ya Kiyahudi katika dunia ya leo. Wao ni Orthodox, Conservative, Reformed, Reconstructionist, na Humanistic. Imani na mahitaji katika kila kundi huwa tofauti kwa kiasi kikubwa; Hata hivyo, orodha fupi ya imani za jadi ya Wayahudi itakuwa ni pamoja na yafuatayo:

Mungu ndiye Muumba wa kila kitu kiliopo; Yeye ni mmoja, hana mwili, na Yeye peke astahili kuabudiwa kama mtawala kamili wa ulimwengu.

Vitabu vitano vya kwanza vya Biblia ya Kiebrania vilifunuliwa kwa Musa na Mungu. Havitabadilishwa au kujadiliwa katika siku zijazo.

Mungu aliwasiliana na Wayahudi kwa njia ya manabii.

Mungu achunguza shughuli za binadamu; Huwalipa watu binafsi kwa ajili ya matendo mema na kuwaadhibu waovu.

Ingawa Wakristo huweka msingi wa imani yao juu ya hayo maandiko ya Kiyahudi vile Wayahudi wanafanya, kuna tofauti kubwa katika imani: Wayahudi kwa ujumla hufikiria hatua na tabia kuwa yenye umuhimu wa msingi; imani huja nje ya vitendo. Hii huitilafiana na Wakristo wahafidhina ambao imani ni ya muhimu na vitendo ni matokeo ya imani.

Imani ya Wayahudi haikubali dhana ya Kikristo ya dhambi ya asili (imani ya kwamba watu wote huridhi dhambi ya Adamu na Hawa wakati waliasi maagizo ya Mungu katika Bustani mwa Edeni).

Uyahudi unathibitisha wema asili wa ulimwengu na watu wake kama ubunifu wa Mungu.

Waumini wa Kiyahudi wana uwezo wa kutakasa maisha yao na kusongea karibu na Mungu kwa kutimiza amri za Mungu (mitzvoti).

Hamna mkombozi anahitajika au anapatikana kama mwangalizi.

Amri 613 zinapatikana katika Walawi na vitabu vingine hudhibiti masuala yote ya maisha ya Wayahudi. Amri kumi, kama zimeradhbishwa katika Kutoka 20:1-17 na Kumbukumbu 5:6-21, zaunda muhtasari mdogo wa sheria.

Masihi (mtiwa wakivu wa Mungu) atafika katika siku zijazo na kukusanya Wayahudi mara nyingine tena katika nchi ya Israeli. Kutakuwa na ufufuo wa wafu wakati huo. Yerusalemu Hekalu, iliyoharibiwa katika miaka ya 70 A.D na Warumi, itajengwa upya.

Imani kuhusu Yesu huwa ya kutofautiana. Baadhi humwona kama mwalimu mkuu wa maadili. Wengine humwona kama nabii wa uongo au kama sanamu ya Ukristo. Baadhi ya madhehebu ya dini ya Kiyahudi hata hawawezi taja jina lake kutokana na kukatazwa dhidi ya kusema jina la sanamu.

Wayahudi mara nyingi hujulikana kama wateule wa Mungu. Hii haimaanishi kwamba wao katika njia yoyote wanapaswa kuchukuliwa bora na makundi mengine. Mistari kama vile Kutoka 19:5 inasema kuwa Mungu amechagua Israeli kupokea na kujifunza Torati, kuabudu Mungu tu, kupumzika siku ya Sabato, na kwa kusherehekea sikukuu. Wayahudi hawakuchaguliwa kuwa bora kuliko wengine; walichaguliwa kuwa mwanga kwa mataifa na kuwa baraka kwa mataifa yote.

English



Rudi kwa ukurasa wa nyumbani wa Kiswahili

Uyahudi ni nini na Wayahudi wanaamini nini?
Shiriki ukurasa huu: Facebook icon Twitter icon Pinterest icon Email icon
© Copyright Got Questions Ministries