settings icon
share icon
Swali

Je, ninapaswa kufanya nini wakati Mungu anasema la?

Jibu


Tunapenda ukweli kwamba Mungu anajibu maombi (1 Yohana 5:14-15). Lakini tunachopenda zaidi ni wakati anakubaliana na maombi yetu na kusema “ndio.” Lakini wakati mwingine jibu la Mungu ni “la” au “bado.” Kama Baba mzuri, Mungu hawezi tupa kile ambacho si cha manufaa kwetu kwa muda mrefu, hata wakati tunambembeleza. “Ndio” ya Mungu inajibu kujenga imani yetu na ujasiri katika maombi. Lakini tunaweza kujibu vipi wakati anasema “la”?

Kukubali “la” ya Mungu inaweza kuwa hali ya mnato. Kuna mistari ambayo inaonekana kuonyesha kwamba chochote tuombacho kwa Imani tutapokea (kwa mfano, Marko 11:24; Mathayo 21:22). Ikiwa tutatenga mistari hiyo na kujenga theolojia juu yao, inaweza kuwa ya kusambaratisha Imani wakati vitu havitatokea jinsi vilivyo tarajiwa. Ni busara kuchukua hatua nyuma na kuzingatia “kusudi lote la Mungu” (Matendo ya Mitume 20:27). Wakati wowote tunayaunda mafundisho juu ya mstari mmoja au miwili, tunatumbukia kwa shinda.

Mara kadhaa katika Maandiko, Mungu hakufanya vile mtu aliomba. Yeye ni Mungu, na anaweza kuona vitu hatuwezi kuona. Mfalme Daudi aliomba Bwana kwa maisha yake na ya mtoto mchanga wa Bathsheba. Daudi alifunga na kuomba kwa masiku, lakini, kwa siku ya saba, mtoto akafa (2 Samweli 12:16, 18). Mungu alisema “la.” Daudi alijibu kwa njia ambayo ni kielelezo kwetu sisi wote. Alikubali kile ambacho Mungu alifanya kilikuwa sawa na kizuri, “akaingia nyumbani mwa Bwana, akasali” (mstari 20). Alikuwa ametumainia matokeo tofauti. Lakini Mungu ni Mungu, na ana haki ya kufanya uamuzi wa maisha na kifo. Katika maombolezi yake, Daudi hakuwa na uchungu kuelekea kwa Bwana au kugeuka. Jibu la Daudi kwa “la” ya Mungu ilikuwa kuabudu kwa ndani na kutubu, hata wakati wa maumivu ya moyo wake.

Agano Jipya linapeana mifano zaidi ya nyakati wakati Mungu alisema “la” kwa watumishi Wake. Mtume Paulo alitumwa kusafiri Asia Minor nzima kuhubiri, lakini Mungu akasema “la” (Matendo ya Mitume 16:6-9). Paulo alifikiria ameelewa mpango wa Mungu. Aliamini angeendelea katika Asia. Lakini Roho Mtakatifu akasema “la.” Kwa sababu tumaini la Paulo lilikuwa kusikiza na kutii, bila kujali gharama, alitoka Asia Minor na badala yake akaelekea Makedonia. Hapo alianzisha makanisa ambayo yaliathiri dunia yote. Jibu lake kwa “la” ya Mungu lilikuwa utii wa mara moja na ubadili wa mwelekeo.

Katika maisha yake binafsi, Paulo alisumbuliwa na kile aliita “mwiba katika mwili, mjumbe wa Shetani ili anipige” (2 Wakorintho 12:7). Paulo aliomba Bwana katika vipindi tatu tofauti achukue “mwiba” huu kutoka kwake, lakini Mungu akasema “la.” Katika majaribu haya, Paulo alijifunza kutegemea hata kwa ndani zaidi neema ya Mungu na kuishi kwa utukufu wa Mungu kupitia hali ngumu. Jibu lake kwa “la” ya Mungu ilikuwa kutukuza katika udhaifu wake (mstari 9). Badala ya kukata tamaa au kuamua Mungu hakuwa anajali, Paulo alichagua “napendezwa na udhaifu, na ufidhuli, na misiba, na adha, na shida, kwa ajili ya Kristo. Maana niwapo dhaifu ndipo nilipo na nguvu” (mstari 10).

Kile tunajifunza kutoka kwa mifano ya kibiblia ni kwamba Mungu haachi kuwa Mungu. Yeye ni huru: “mimi ndimi Mungu, wala hakuna mwingine aliye kama mimi. Ni mimi nitangazaye mwisho tangu mwanzo, naam, tangu zamani za kale, mambo ambayo hayajatendeka. Ninasema: Kusudi langu ndilo litakalosimama, nami nitatenda mapenzi yangu yote…Lile ambalo nimelisema, ndilo nitakalolitimiza;

lile nililolipanga, ndilo nitakalolitenda” (Isaya 46:9-11).

Kuna mara nyingi wakati Mungu anaweza sema “ndio” kwa maombi yetu kwa sababu yanakaa katika mpango ako nayo katika maisha yetu (Warumi 8:28). Alisema “ndio” kwa ombi la Musa la kuona utukufu Wake (Kutoka 33:17). Alisema “ndio” kwa ombi la Sulemani kwa hekima (1 Wafalme 3:11-13). Na Yesu alisema “ndio” kwa kila mtu ambaye alimwomba Yeye uponyaji na usaidizi (Mathayo 8:16). Lakini maombi yetu yaliyojazwa na imani hayachukui nafasi ya kanuni huru ya Mungu. Ikiwa amefungwa kwa maombi yetu, vile wengine wanafundisha, anaweza, kwa asili, kuacha kuwa Mungu. Tunaweza kuwa miungu kwa kuamuru matendo Yake. Hakuna mahali katika Maandiko tuna mfano kama huo.

Mara nyingi Mungu anasema “la” kwa vitu tunatamani kuona zifanyike. Wale wana Imani change wakati mwingine wanatumia hili kama kizingizio la kumtupa Yeye: “Mungu hakumponya mtoto wangu.” “Mungu hakuokoa ndoa yangu.” “Mungu hakunipa ile kazi nilikuwa nahitaji.” Ikiwa mtazamo wetu ni kwamba Mungu ana wajibu wa kukubali maombi yetu jinsi jini linavyo kubali matakwa, basi tutafadhaika wakati Mungu “hatatutendea.” Tunachagua ikiwa tutaruhusu “la” kutoka kwa Mungu kusambaratisha imani yetu au kuijenga; “la” kutoka kwa Mungu inaweza kutufunza kuvumilia—hata wakati hatuelewi (Yakobo 1:3).

Mara nyingi ni katika nyakati wakati Mungu anasema “la” kwamba tunalazimishwa kumtafuta Mungu kwa bidii zaidi. “La” ya Mungu mara nyingi usambaratisha sanduku ndogo ambalo tumejaribu kumweka Yeye na kuruhu Mungu halisi kujifichua Mwenyewe kwetu. Anasema “la” wakati ni sehemu ya mpango Wake mkubwa zaidi. Anasema “la” wakati ukosaji wetu wa Imani unaonyesha kwamba kwa kweli hatuamini Yeye ni Yule Yule (Waebrania 11:6). Anasema “la” wakati maombi yetu ni yenye mizizi katika ubinafsi (Yakobo 4:3) au wakati “ndio” itatudhuru. Na anasema “la” wakati, kama vile Paulo, lazima tujifunze kwamba neema Yake ni ya kutosha kwetu. Mifano ya kibiblia ya watumishi wa Mungu ambao walikabiliana na “la” ya Mungu inatusaidia kujifunza jibi sahihi wakati Mungu anasema “la” kwetu.

English



Rudi kwa ukurasa wa nyumbani wa Kiswahili

Je, ninapaswa kufanya nini wakati Mungu anasema la?
Shiriki ukurasa huu: Facebook icon Twitter icon Pinterest icon Email icon
© Copyright Got Questions Ministries