settings icon
share icon
Swali

Je! Tuna wakati uliowekwa wa kifo?

Jibu


Biblia inatuambia kwamba “Siku zangu zote ulizonipangia ziliandikwa katika kitabu chako

kabla haijakuwepo hata moja” (Zaburi 139:16). Kwa hiyo, naam, Mungu anajua ni linii, wapi na ni jinsi gani tutakufa. Mungu anajua kabisa kila kitu kutuhusu (Zaburi 139:1-6). Kwa hivyo hii inamaanisha kuwa hatima yetu imetiwa muhuri? Je! Hii inamaanisha kwamba hatuna mamlaka kabisa juu ya wakati tutakufa? Jibu ni ndiyo na la, ikitegemea mtazamo.

Jibu ni “ndiyo” kutoka kwa mtazamo wa Mungu, kwa sababu Mungu ni mjuzi wa yote-Yeye anajua kila kitu na anajua hasa ni lini, wapi, na ni jinsi gani tutakufa. Hakuna tunachoweza kufanya kitakachobadilisha kile ambacho Mungu anajua kitatokea. Jibu ni “la” kutoka kwa mtazamo wetu, kwa sababu tunaweza kuathiri wakati, mahali, na jinsi tutakavyokufa. Ni wazi kwamba mtu anayejiua husababisha kifo chake mwenyewe. Mtu anayejiua angeishi muda mrefu zaidi kama hangejiua. Vile vile, mtu anayekufa kwa sababu ya uamuzi wa kipumbavu (kwa mfano, matumizi ya dawa za kulevya “uharakisha” kifo chake mwenyewe. Mtu anayekufa kwa saratani ya mapafu kwa sababu ya kuvuta sigara hangekufa kwa njia ile ile au wakati huo huo ikiwa hagevuta sigara. Mtu anayekufa kwa mshtuko wa moyo kwa sababu ya ulaji usiofaa maishani na mazoezi kidogo hangekufa kwa njia ile ile au wakati huo huo ikiwa angekula lishe bora na kufanya mazoezi zaidi. Naam, maamuzi yetu wenyewe yana matokeo yasiyoweza kukanushwa juu ya namna, wakati, na mahali pa kifo chetu.

Je! hii inaathiri vipi maisha yetu hasa? Tunapaswa kuishi kila siku kwa ajili ya Mungu. Yakobo 4:13-15 inatufundisha, “Basi sikilizeni ninyi msemao, “Leo au kesho tutakwenda katika mji huu ama ule tukae humo mwaka mmoja, tufanye biashara na kupata faida.’ Lakini hamjui hata litakalotukia kesho. Maisha yenu ni nini? Ninyi ni ukungu ambao huonekana kwa kitambo kidogo kisha hutoweka. Badala yake, inawapasa kusema, “Kama Bwana akipenda, tutaishi na kufanya hili ama lile.” tunapaswa kufanya maamuzi yenye hekima kuhusu jinsi tunavyoishi maisha yetu na jinsi tunavyojitunza wenyewe. Na hatimaye, tunamwamini Mungu kwamba Yeye ndiye mwenye enzi na anatawala mambo yote.

English



Rudi kwa ukurasa wa nyumbani wa Kiswahili

Je! Tuna wakati uliowekwa wa kifo?
Shiriki ukurasa huu: Facebook icon Twitter icon Pinterest icon Email icon
© Copyright Got Questions Ministries