settings icon
share icon
Swali

Je! Mkristo anastahili kufanya mazoezi? Bibilia inasema nini kuhusu afya?

Jibu


Kama vile vitu vingi katika maisha, kuna kule kupita mipaka katika sehemu ya mazoezi. Watu wengine wanaangazia kiroho tu peke, na kuiacha miili yao. Wengine wanaangazia sana umbo na sura ya mwili yao na kupuuza ukuaji wa kiroho na ukomavu. Kati ya hayo yote hakuna lenye linaleta usawa wa Bibilia. Timotheo wa kwanza 4:8 yatujulisha, “Kwa maana kujizoeza kupata nguvu za mwili kwafaa kidogo, lakini utauwa hufaa kwa mambo yote; yaani, unayo ahadi ya uzima wa sasa, na ya ule utakaokuwapo baadaye.” Kumbuka kwamba aya hii haiondoi mokosa aja ya kufanya mazoezi. Bali, yasema kuwa mazoezi ni muimu, lakini yapatiwe kipao mbele kwa njia inayofaa kwa kusema kuwa ucha Mungu ndio wa maana zaidi.

Mtume Paulo pia anataja mafunzo ya mazoezi katika kuonyesha ukweli wa kiroho 1 Wakorintho 9:24-27. Anazawazisha maisha ya Kikristo na mbio ambazo twakimbia “kupata tuzo.” Lakini tuzo tulitafutalo ni la taji ya milele ambayo haitaharibika. Katika 2 Timotheo 2:5, Paulo anasema, “Hata mtu akishindana katika machezo hapewi taji, asiposhindana kwa halali.” Paulo anatumia mfano wa mwanambio pia katika 2 Timotheo 4:7: “Nimevipiga vita vilivyo vizuri, mwendo nimeumaliza, Imani nimeilinda.” Huku angazo la maandiko haya haliko katika mazoezi ya mwili, hoja kwamba Paulo anatumia misemo ya mbio kutufunza ukweli wa kiroho yaonyesha kwamba Paulo aliyachukulia mazoezi ya mwili na hata mashindano kuwa halisi. Sisi wote ni viumbe wa kimwili na kiroho. Huku sehemu ya kiroho yetu ni kunena kibibilia, ya maana, hatustahili kupuuza sehemu ya mwili na kiroho ya afya yetu.

Kwa uwazi, hakuna kitu cho chote kibaya na Mkristo kufanya mazoezi. Kwa kweli, Bibilia ii wazi kuwa tunastahili kiutunza miili yetu (1 Wakorintho 6:19-20). Kwa wakati huo huo, Bibilia inatuonya kinyume na majivuno (1 Samweli 16:7; Methali 31:30; 1 Petero 3:3-4). Lengo letu katika kufanya mazoezi liziwe kuongeza uzito wa miili yetu ili watu watambue na kututhamani. Bali, lengo la mazoezi liwe kuijenga afya yetu ya mwili ili tuweze kuwa na nguvu ambayo tutaitolea kwa malengo ya kiroho.

English



Rudi kwa ukurasa wa nyumbani wa Kiswahili

Je! Mkristo anastahili kufanya mazoezi? Bibilia inasema nini kuhusu afya?
Shiriki ukurasa huu: Facebook icon Twitter icon Pinterest icon Email icon
© Copyright Got Questions Ministries