settings icon
share icon
Swali

Je, ni lazima niami kuwa Biblia haina makosa ili niokolewe?

Jibu


Hatuokolewi kwa kuamini katika upumzi au kutokuwa na kasor kwa Biblia. Tunaokolewa kwa kumwamini Bwana Yesu Kristo kama Mwokozi wetu kutoka kwa dhambi (Yohana 3:16, Waefeso 2:8-9; Warumi 10:9-10). Wakati huo huo, ingawa, ni kwa njia ya Biblia kwamba sisi hujifunza kuhusu Yesu Kristo na kifo chake na ufufuo kwa niaba yetu (2 Wakorintho 5:21, Warumi 5:8). Hatustahili kuamini kila kitu katika Biblia ili tuokolewe - lakini ni lazima tuamini katika Yesu Kristo, ambaye anatangazwa katika Biblia. Ni lazima basi sisi tushikilie dhahiri Biblia kama neno la Mungu na tunapaswa kuamini kabisa kila kitu Biblia inafundisha.

Wakati watu kuokolewa kwanza, wao kwa ujumla wana ufahamu kidogo sana kuhusu Biblia. Wokovu ni mchakato ambao huanza na kuelewa hali yetu ya dhambi, si uelewefu wa Biblia kutokuwa na kasoro. Dhamira yetu hutuambia kwamba sisi hatuna uwezo wa kusimama mbele ya Mungu mtakatifu kwa matendo yetu wenyewe. Tunajua kwamba sisi si wenye haki ya kutosha kufanya hivyo, hivyo sisi humgeukia na kukubali sadaka ya mwana wake juu ya msalaba kwa malipo ya dhambi zetu. Sisi huweka matumaini yetu yote kwake. Kutokana na hali hiyo, tuna asili mpya kabisa, safi na isiyo na hitilafu na dhambi. Roho Mtakatifu wa Mungu anaishi ndani ya mioyo yetu, kututia mhuri wa uzima wa milele. Sisi huenda mbele kutoka uhakika huo, kumpenda na kumtii Mungu zaidi na zaidi kila siku. Sehemu ya "kwendelea mbele" ni kula chakula kila siku ya neno lake, kukua na kutuimarisha katika kutembea kwetu na yeye. Biblia peke yake ndio ina uwezo wa kufanya muujiza huu katika maisha yetu.

Kama tunaamini katika utu na kazi ya Bwana Yesu Kristo, kama inavyo fundishwa katika Biblia, sisi tumeokolewa. Tunapomwamini Yesu Kristo, ingawa, Roho Mtakatifu atafanya kazi katika mioyo yetu na akili - na kutushawishi sisi kwamba Biblia ii kweli na ni ya kauminiwa (2 Timotheo 3:16-17). Kama kuna shauku katika akili zetu kuhusu maandiko kutokuwa na kasoro, njia bora ya kushughulikia jambo hili ni kumwomba Mungu kutupa uhakika kuhusu neno lake na imani katika neno lake. Yeye you tayari zaidi kujibu wale ambao wanamtafuta kwa uaminifu na kwa mioyo yao yote (Mathayo 7:7-8).

English



Rudi kwa ukurasa wa nyumbani wa Kiswahili

Je, ni lazima niami kuwa Biblia haina makosa ili niokolewe?
Shiriki ukurasa huu: Facebook icon Twitter icon Pinterest icon Email icon
© Copyright Got Questions Ministries