settings icon
share icon
Swali

Ni kwa nini nasaba ya Yesu katika Mathayo na luka ni tofauti?

Jibu


Ukoo wa Yesu umetolewa katika maeneo mawili katika Maandiko: Mathayo 1 na Luka 3:23-38. Mathayo athari nasaba kutoka kwa Yesu hadi Abrahamu. Luka athari nasaba inaanzia Yesu hadi Adamu. Hata hivyo, kuna sababu nzuri ya kuamini kwamba Mathayo na Luka ni kwa nini zinaangazia nasaba tofauti kabisa. Kwa mfano, Mathayo inatoa Yusufu kama babake Yakobo (Mathayo 1:16), wakati Luka anamtaja Yusufu kama babake Eli (Luka 3:23). Mathayo athari ya uzao wa Yesu kupitia Daudi mwanake Suleimani (Mathayo 1:6), wakati Luka athari ya uzao yapitia Nathani mwanawe Daudi (Luka 3:31). Kwa kweli, kati ya Daudi na Yesu, majina tu ya nasaba ambayo wako nayo pamoja ni Shealtieli, na Zerubabeli (Mathayo 1:12, Luka 3:27).

Baadhi ya wengine hutaja tofauti hizi kama ushahidi wa makosa katika Biblia. Hata hivyo, Wayahudi walikuwa watunzi wa kumbukumbu, hasa kuhusiana na nasaba. Haidhaniwi kwamba Mathayo na Luka waweza kuwa na nasaba mbili ambazo zapingana kabisa za ukoo mmoja. Tena tangu Daudi hadi wakati wa Yesu nasaba mbili kupingana kabisa za ukoo huo. Tena tangu Daudi kwa njia ya Yesu, ukoo ni tofauti kabisa. Hata kumbukumbu ya Shealtieli, na Zerubabeli kuna uwezekano kuwa zarejelea watu tofauti wa jina moja. Mathayo inamtoa Yekonia kama babake Shealtieli huku Luka akimleta Niri kama babake Shealtieli. Itakuwa kawaida kwa mtu wa kawaida aitwaye Shealtieli kumpa mwanawe jina mwanawe Zerubabeli katika mwanga wa watu maarufu wa majina hayo (angalia vitabu vya Ezra na Nehemia).

Maelezo mengine ni kwamba Mathayo anafuatilia ule ukoo wa msingi huku Luka akizingatia matukio ya “ndoa ya kilawi” Kama mtu alikufa bila ya kuwa na mwana wa kiume, ilikua utamaduni kwa ndugu wa huyo mtu kuoa mke wake na kuwa na mwana wa kiume ambaye angeweza kuendeleza jina la huyo mtu. Huku kukiwa na uwezekano, mtazamo huu sio ule uwezekanavyo wa kila kizazi kutoka Daudi hadi Yesu bila kuwa na “ndoa ya kilawi” ili tafauti iwepo kwa kila kizazi. Hili ni jambo lizilo wezekana kabisa.

Pamoja na dhana hizi kwa mtazamo wasomi wengi wa Biblia hudhania kuwa Luka amenakili nasaba ya Maria na Mathayo kurekodi nasaba ya Yusufu. Mathayo anafuatilia uzao Yusufu (baba mzazi wa Yesu), kupitia Suleimani mwanawe Daudi, wakati Luka anafuatilia ukoo wa Maria (jamii ya Yesu) kupitia Nathani mwanawe Daudi. Hakukuwa na neno la Kiyunani la “mwana-mkwe” na Yusufu angechukuliwa kuwa mwana mkwe wa Eli kwa kumuoa Maria bintiye Eli. Kupitia aidha, Yesu ambaye ni wa uzao wa Daudi na kwa hivyo ako na haki ya kuwa Masihia. Sio jambo la kawaida kufuatilia nasaba kupitia upande wa mama, lakini hivyo ndivyo ilivyokua kwa kuzaliwa na bikira. Maelezo ya Luka ni kuwa Yesu alikuwa mwana wa Yusufu, “hivyo ndivyo ilivyowazwa” (Luka 3:23).

English



Rudi kwa ukurasa wa nyumbani wa Kiswahili

Ni kwa nini nasaba ya Yesu katika Mathayo na luka ni tofauti?
Shiriki ukurasa huu: Facebook icon Twitter icon Pinterest icon Email icon
© Copyright Got Questions Ministries