settings icon
share icon
Swali

Ninawezaje kujua kama nimempenda mtu?

Jibu


Mapenzi ni mhemuko wa nguvu sana. Husukuma sehemu nyingi za maisha yetu. Tunafanya maamuzi kwa misingi ya mihemuko hii, na hata kuoa/kuolewa kwa sababu tunahisi tuko katika “mapenzi.” Hii inaweza kuwa sababu nusu ya ndoa zote huishia talaka. Bibilia inatufunza kwamba mapenzi ya kweli sio mhemuko ambao utakuja na uende, bali ni uamuzi. Hatustahili kupenda wale wanaotupenda pekee; tunastahili kuwapenda hata wale wanaotuchukia, namna ile ile Kristo anawependa wasiopendeka (Luka 6:35). “Upendo huvumilia, hafadhili; upendo hauhusudu; upendo hautakabari; haujivuni; haukosi kuwa na adabu; hautafuti mambo yake; hauoni uchungu; hauhesabu mabaya; haufurahii udhalimu, bali hufurahi mapoja na kweli; huvumilia yote; huamini yote; hatumainia yote; hustahimili yote” (1 Wakorintho 13: 4-7)

Inaweza kuwa rahisi kuingia “katika mapenzi” na mtu, lakini kuna maswali ya kujiuliza kabla ya kuamua kama chenye tunahisi ni upendo wa kweli. Kwanza, huyu mtu ni Mkristo, kumaanisha, ameyatoa maisha yake kwa Kristo? Anamwamini Kristo pekee kwa wokovu? Pia, kama unapndelea kufungulia moyo wako na mihemuko kwa mtu mmoja, inastahili kujiuliza kama uko tayari kumweka huyo mtu mbele ya vitu vyote, na kuuweka uhusiano wenu kuwa wa pili baada ya Mungu. Bibilia inatuambia kwamba, wakati watu wawili wanaoana, wanakuwa mwili mmoja (Mwanzo 2:24; Mathayo 19:5).

Kitu kingine cha kuangalia ni kama anayependwa ni mtu amefusu kuwa mwenzi. Amekwisha mweka Mungu kuwa wa kwanza katika maisha yake? Ako tayari kuutoa wakati wake nguvu yake kuujenga uhusiano ukomae hadi ndoa ambayo itadumu? Hakuna mizani ya kutambua kama kwa kweli tuko na mapenzi na mtu mwingine, lakini ni muimu kutambua kama twafuata mihemuko yetu au twafuata mapenzi ya Mungu kwa maisha. Upendo wa kweli ni uamuzi, sio mhemuko. Upendo wa kweli wa kibibilia na kumpenda mtu wakati wote, sio wakati unahisi “kupenda.”

English



Rudi kwa ukurasa wa nyumbani wa Kiswahili

Ninawezaje kujua kama nimempenda mtu?
Shiriki ukurasa huu: Facebook icon Twitter icon Pinterest icon Email icon
© Copyright Got Questions Ministries