settings icon
share icon
Swali

Je, ni makosa kufadhaika au kukasirikia Mungu?

Jibu


Ubatilisho ni kuwa na hisia ya kutokuvumilia na wasiwasi tunayopata wakati tunadhani mahitaji yetu hayajafikiwa au wakati tunapokabiliana na shida zinazoonekana zisizoweza kushindwa. Wakati mwingine, tunamlaumu Mungu wakati tunapokosa subra na kutoridhika. Kukasirikia Mungu, njia zake na matendo Yake kwetu inaweza kuwa kizuizi kwa Wakristo. Mungu anaweza kushughulikia shida hii kwa urahisi-basi kwa nini asifanye hivyo? Mungu anajua ninahitaji-basi yuko wapi? Kuna Wakristo wachache ambao hawajafadhaika kwa Bwana kwa sababu moja au nyingine wakati fulani katika maisha yao.

Katika Luka 10: 38-42) tunapata kwamba Martha ni suala la kuzungumzia. Yesu alikuwa akimtembelea nyumbani kwake, na Martha alitaka kumtengenezea Yesu mlo mzuri. Andiko linasema "lakini Martha alikuwa anashughulika na mambo mengi .'' Wakati huo huo, dada ya Martha, Maria, "aliketi kwa miguu ya Bwana akisikiliza yale aliyosema." Katika shughuli zake nyingi, Martha alihisi kuwa anastahili msaada katika jikoni, na kukasirika kwake kukazidi. Yeye "alikuja kwake yesu na kumwuliza, 'Bwana, hujali kwamba dada yangu ameniacha kufanya kazi peke yangu? Mwambie anisaidie! '"Kumbuka kwamba Martha alikuwa amefadhaika kwa sababu ya Maria kutosaidia pamoja na Bwana kwa kuruhusu Maria kuwa" mvivu. "Yesu alimshawishi rafiki yake:"' Martha, Martha, ''unahangaika na kusumbuka kwa mambo mengi.'' "Kisha akachukua fursa ya kufundisha somo juu ya kutulia na kumjua Mungu (tazama Zaburi 46:10) — somo ambalo tunasahau wakati tunapofadhaika.

Hadithi nyingine inayojulikana ni ya Yona. Yeye, pia, alielewa ni nini haswa kufadhaika katika Bwana. Yona alisikia kutoka kwa Mungu, lakini hakupenda yale aliyasikia (Yona 1: 1-3a). Baada ya kutangaza shingo upande ujumbe wa Mungu kwa watu wa Ninawi , Yona alikuwa na uhakika kwamba hawatasikia na kwamba atakuwa na furaha ya kuwaona wakiuawa na Mungu mwenye kisasi. Kwa uchungu wa Yona, watu wa Ninawi waliitikia kwa toba na unyenyekevu kwa Mungu (Yona 3: 5-10). Yona alifadhaika. Hisia yake ya haki ilitofautiana na huruma ya Mungu.Mambo yakawa mabaya zaidi wakati ambapo mmea y ambao Yona alikuwa anaota kivuli uliponyauka na kumwacha Yona akiwa kwa jua kali (Yona 4: 7). Yona alifadhaika zaidi hadi alitamani kifo. Yona 4: 9). Mungu hakua na budi kukumbusha nabii wake mwenye hasira kwamba mtazamo wake ulikuwa mbaya: Yona alijali zaidi mmea kuliko mji mkuu uliojaa watu. Kufadhaika kunaweza kuondokana maono yetu na kutufanta watu wasio na huruma.

Je, ni kosa kufadhaika au kukasirikia Mungu? Ndiyo. Kufadhaika kunaxsababishwa na asili yetu ya kimwili ya dhambi. Kufadhaikia Mungu inaweza kuthibitisha ukosefu wa imani katika Mungu au kutomuelewa Mungu. Ikiwa Mungu ni mkamilifu-na Biblia inasema hivyo (Zaburi 18:30) — basi Yeye ana nia kamili, wakati kamili, mbinu kamilifu, na matokeo kamilifu. Tunapozingatia mawazo yetu katika Bwana na kumtegemea Yeye, tutajua amani, sio kufadhaika(Isaya 26: 3).

Kufadhaika katika Mungu kunaweza kuchangiwa na ukaidi wetu wenyewe. Wakati tamaa zetu zinapingana na madhumuni ya Mungu, kwa kawaida tutafadhaika. Sio vyema kupigana dhidi ya Mungu. Saulo wa Tarso alijifunza somo hili kwa njia ngumu, na Yesu hakua na budi kumkumbusha, "Unajiumiza bure kama ng'ombe anayepiga teke fimbo ya bwana wake" (Matendo 26:14). Sala rahisi ya unyenyekevu hutoa faraja kubwa zaidi kuliko kusisitiza kwa bidii juu ya mipango yetu.

Mungu anawaambia baba wa kidunia, "Nanyi wazazi msiwachukize watoto wenu" (Wakolosai 3:21). Hakika, Mungu hataki kuwachukiza watoto Wake mwenyewe. Tunapofadhaika na Mungu maranyingi hiwa ni kutokana na ukosefu wa ufahamu kwa upande wetu, sio kosa lolote kwa upande wa Mungu. Njia bora ya kutofadhaika ni kunyenyekea kwa mapenzi yake, kukubali muda wake, na kuamini wema wake. "Mwekeeni matatizo yenu yote, maana yeye anawatunzeni " (1 Petro 5: 7).

English



Rudi kwa ukurasa wa nyumbani wa Kiswahili

Je, ni makosa kufadhaika au kukasirikia Mungu?
Shiriki ukurasa huu: Facebook icon Twitter icon Pinterest icon Email icon
© Copyright Got Questions Ministries