settings icon
share icon
Swali

Nimechomwa na kuumizwa na kanisa katika siku za nyuma? Niwezaje kushinda hili na kufanya upya shauku kwa kanisa na hamu ya kuhudhuria kanisa?

Jibu


Maumivu yaliyosababishwa na kanisa ni "muuaji wa kimya." Hii haimaanishi kwamba maneno na matukio ambayo yanaumiza moyo wako si mbaya sana na ya umma. Ni "muuaji wa kimya" kwa sababu ya kile inafanya ndani ya akili, moyo, na nafsi ya aliyejeruhiwa. Ikiwa haitashughulikiwa, itaharibu furaha ya baadaye, raha, na ustawi. Uharibifu unaathiri vibaya huduma na ufikiaji wa kanisa, pia, na makanisa mengine hayaponi kamwe. Kutambua kwamba tabia ambayo imeleta uharibifu huo kwa moyo wako sio tofauti sana kuliko maumivu yeyote kati yetu anaweza kukutana nayo mahali pa kazi, sokoni, au nyumbani. Tofauti ni sisi hatutarajii watu wa Mungu kufanya kama wale wasio na Kristo katika maisha yao. Kanisa ni mahali moja karibu kila mtu anakubali kunapaswa kuwa salama, kukubali, kusamehe, na huru kutokana na migogoro na maumivu. Bado katika makanisa mengi angalau baadhi ya vipengele vya ugomvi, migogoro, na chuki huingia na kuharibu ukamilifu huo.

Inafanyika zaidi katika makanisa mengine kuliko mengine. Afya ya kiroho ya watu kanisani na nguvu za uongozi huamua jinsi inavyoenea na kwa kiasi gani tabia hiyo ya kugawanya inaweza kupata udhibiti. Kutokana na udhibiti, kwa polepole na kwa hakika huharibu msingi wa maisha ya kiroho ya mkutano.

Ni muhimu kugeuza lengo lako mbali na watu wanaohusika na kanisa yenyewe na kutambua sababu ya msingi wa maumivu, msukosuko, na kuishiwa kwa Imani yako. Ufafanue kwa uaminifu unachohisi. Ikiwa uko kama watu wengi, hapa kuna baadhi ya uwezekano: hasira, huzuni, kukata tamaa, kukataliwa, kuumizwa, wivu, udhaifu, hofu, uasi, kiburi, aibu, kuaibishwa, au kupoteza. Jua ni nini kiini cha maumivu yako-sio kile mtu aliyesema au alikufanyia, lakini ni nini kinachosababisha maumivu yako? Kisha tafuta Maandiko ili kugundua kile Mungu anasema kuhusu hilo. Chukua upatano wa Biblia na kuangalia juu ya kila neno na kusoma, kufikiria, kuomba, na kutumia mstari. Kwa mfano, unaweza kufikiri kwamba umekasirika wakati kwa kweli unahisi kukataliwa. Je, Mungu anasema nini kuhusu kukataliwa? Anasema, "Sitakupungukia kabisa, wala sitakuacha kabisa"(Waebrania 13:5); "Naam nimekupenda kwa upendo wa milele" (Yeremia 31:3); na, "na tazama, mimi nipo pamoja nanyi siku zote" (Mathayo 28:20).

Unapotambua kwa kweli chazo cha maumivu yako, Mungu ana faraja ya hekima, huruma, na upendo wa kuponya majeraha yako. Ikiwa utamwomba Yeye kwa msaada, malengo yako yanabadilika Kwake na mbali na watu wengine na matendo yao. Utaacha kusimulia tukio ambalo lilikusababishia maumivu. Kwa kweli unaweza kuumia, kujeruhiwa, au kukosewa. Hakika unalihisi. Hisia hizo ni mazao ya ndani sana, uhalisi muhimu zaidi ambao umeangusha hisia zako kwa Mungu, kanisa Lake, na kusudi Lake kwa maisha yako. Ikiwa zitasalia bila kushughulikiwa, hisia hizo zitasababisha chazo cha uchungu ambao utaathiri vibaya kila utembo wa nafsi yako na kukuibia maisha yako mengi katika Kristo (Yohana 10:10). Hutaki hili lifanyike katika maisha yako.

Tunawezaje kuweka uzoefu wa kuumiza kutoka kusongeza uharibifu wao ndani ya nafsi zetu? Kitabu cha hekima kutoka Biblia kinasema lazima "linda moyo wako kuliko yote uyalindayo; maana ndiko zitokako chemchemi za uzima" (Methali 4:23). Tunalinda mioyo yetu kwa kuchagua kwa makini mawazo yetu, hisia, mtazamo, na vitendo. Linda moyo wako kwa kukataa kukaa juu ya kile kilichotokea, kukataa kuzingatia watu ambao walikuumiza, na kukataa kushambulia udhaifu wa kanisa. Kutoa uchungu inachukua unyenyekevu, lakini "Mungu huwapinga wajikuzao, bali huwapa neema wanyenyekevu" (Yakobo 4:6; Mithali 3:34). Inachukua mtazamo na matendo ya kusamehe (Mathayo 18:22, Marko 11:27, Waefeso 4:32; Wakolosai 3:13) bila hisia ya kisasi (Warumi 12:19). Zaidi, inachukua uwezo wa Roho Mtakatifu anayefanya kazi ndani na kupitia kwako (Waefeso 3:16).

Usimlaumu Mungu kwa jinsi watoto Wake wanavyofanya. Usiache kanisa, pia. Kuna watu wengi zaidi waliojitolea, kujazwa na neema, kupenda, na kusamehe kuliko si katika makanisa mengi. Watafute. Tumia muda nao. Ikiwa huwezi kuwapata, tafuta kanisa lingine (ni kawaida kwamba huwezi kuwapata hata katika mazingira magumu ya kanisa). Kanisa ni wazo la Mungu, na Yeye hulinda kwa uaminifu hata ingawa wakati mwingine Yeye huumizwa kwa tabia yake (angalia Ufunuo 2-3).

Unaweza kuwa na matumaini kwa sababu unatafuta uponyaji kutoka kwa Bwana. Sasa ni juu yako kufanya jambo linalofaa na kubadilisha lengo lako kwa Mtu ambaye atabadili maisha yako kwa kweli juu na zaidi ya maumivu haya. Yesu aliahidi, "Njoni kwangu, ninyi nyote msumbukao na wenye kulemewa na mizigo, nami nitawapumzisha. Jitieni nira yangu, mjifunze kwangu; kwa kuwa mimi ni mpole na mnyenyekevu wa moyo; nanyi mtapata raha nafsini mwenu; kwa maana nira yangu ni laini, na mzigo wangu ni mwepesi"(Mathayo 11:28-30).

English



Rudi kwa ukurasa wa nyumbani wa Kiswahili

Nimechomwa na kuumizwa na kanisa katika siku za nyuma? Niwezaje kushinda hili na kufanya upya shauku kwa kanisa na hamu ya kuhudhuria kanisa?
Shiriki ukurasa huu: Facebook icon Twitter icon Pinterest icon Email icon
© Copyright Got Questions Ministries