settings icon
share icon
Swali

Nimeweka imani yangu kwa Yesu … sasa ni fanyeje?

Jibu


Hongera! Umefanya uamuzi wa kubadilisha maisha! Huenda ikawa unauliza, “sasa ni fanye nini?Nianze vipi safari yangu na Mungu?” Hatua tano zilizo orodheshwa hapo chini zitakupatia muongozo kutoka kwa Bibilia. Iwapo una maswali safarini mwako,tafadhali tembelea https://www.gotquestions.org/Kiswahili.

1. Hakikisha unaelewa maana ya wokovu.

1 Yohana 5:13 anatuambia,” Nimewaandikia ninyi mambo hayo, ili mjue yakuwa mna uzima wa milele. Mungu anataka tuelewe maana ya wokovu.Mungu anataka tuwe na ujasiri wa kufahamu kwa kweli kwamba tumeokoka. Kwa ufupi tu,wacha tuviendee vipengele muhimu vya wokovu:

(a) Sote tumefanya dhambi.Sote tumefanya mambo ambayo hayampendezi Mungu (Warumi 3:23).

(b) Kwasababu ya dhambi zetu,tunastahili kuadhibiwa kwa kutengwa milele na Mungu (Warumi 6:23).

(c) Yesu alikufa msalabani kwa ajili ya dhambi zetu (Warumi 5:8; 2 Wakorintho 5:21).Yesu alitufia pahali petu,kwa kuchukua adhabu ambayo sisi tulistahili. Kufufuka kwake kulidhihirisha yakuwa kifo chake Yesu kilitosha kutulipia dhambi zetu.

(d) Mungu hutoa msamaha na wokovu kwa wote wale wamuaminio Yesu – kwa kuamini kifo chake kama malipo ya dhambi zetu (Yohana 3:16; Warumi 5:1; Warumi 8:1).

Hizo ndizo habari za wokovu! Ikiwa umeweka imani yako kwa Yesu kama mwokozi wako, umeokoka! Dhambi zako zote zimesamehewa na Mungu ana ahidi kutokuacha wala kutokutenga (Warumi 8:38;Mathayo 28:20).Kumbuka,wokovu wako uko salama ndani ya Yesu Kristo (Yohana 10:28-29). Ukiwa unamuamini Yesu pekee kama mwokozi wako, unaweza kuwa na uhakika yakuwa utaishi milele na Mungu mbinguni!

2. Tafuta Kanisa Zuri linalo fundisha Bibilia.

Usilifikirie Kanisa kama jengo.Kanisa ni watu. Ni muhimu sana kwa wamuaminio Yesu kristo kushirikiana mmoja na mwengine. Hiyo ndiyo sababu ya kwanza muhimu ya Kanisa. Sasa kwa kuwa umeweka imani yako kwa Yesu Kristo, tunakuhimiza vilivyo kutafuta Kanisa linalo amini mafundisho ya Bibilia katika eneo lako na uzungumze na Mchungaji. Mfahamishe upya wa imani yako katika Yesu Kristo.

Sababu ya pili ya Kanisa, ni kufundisha Bibilia.Unaweza kujifundisha jinsi yakuyatumia maagizo ya Mungu katika maisha yako. Kulielewa Bibilia ni ufunguo wa kuishi katika ushindi na nguvu/ uthabiti katika maisha ya kikristo. 2Timotheo 3:16-17 yasema “kila andiko, lenye pumzi ya Mungu, lafaa kwa mafundisho,na kwa kuwaonya watu makosa yao,na kwa kuwaongoza,na kwa kuwaadibisha katika haki; ili mtu wa Mungu awe kamili, amekamilishwa apate kutenda kila tendo jema.”

Sababu ya tatu ya Kanisa ni kuabudu.Kuabudu ni kumshukuru Mungu kwa yote aliyo fanya!Mungu ametuokoa. Mungu anatupenda.Mungu anatutimizia mahitaji yetu. Mungu anatuongoza na kutuelekeza. Je ni kwanini tusingemshukuru? Mungu ni mtakatifu, mwenye haki,upendo,huruma na amejaa neema.Ufunuo wa Yohana 4:11 asema, “umestahili wewe, Bwana wetu na Mungu wetu, kuupokea utukufu na heshima na uweza; kwa kuwa wewe ndiwe uliyeviumba vitu vyote, na kwasababu ya mapenzi yako vilikuwako, navyo vikaumbwa.”

3. Jitengee mda kila siku wa kutafakari juu za Mungu.

Ni muhimu sana kwetu kuwa na mda wa kutafakari juu za Mungu kila siku. Wengine huuita” wakati wa kutafakari, wengine huuita wakati wa “kujitoa” kwasababu ni wakati tunapo jitolea kwa Mungu. Wngine hupendelea wakati wa asubuhi na wengine jioni. Haijalishi unauitaje wakati huu ama ni lini hujitoa. Kinacho stahili ni kwamba uwe na wakati na Mungu mara kwa mara. Ni matendo gani yanadhihirisha wakati wetu na Mungu?

(a) Maombi. Maombi ni hali ya kuzungumza na Mungu. Kuongea na Mungu kuhusu hali zako na shida zako.Muulize Mungu akupe hekima na muongozo. Muulize Mungu akutane na mahitaji yako. Mwambie Mungu ni kwa jinsi gani unampenda na ni kwa kiwango gani unamshukuru kwa yale yote anayo kutendeaHiyo ndiyo maana halisi ya maombi.

(b) Kusoma Bibilia.Zaidi ya kufundishwa Bibilia kanisani,katika shule ya Jumapili, na au kwa mafundisho ya Bibilia - unahitaji kujisomea Bibilia mwenyewe. Bibilia iko na kila kitu unacho hitaji kujua ili kukuwezesha kuishi maisha ya kikristo yenye ushindi. Ina muongozo wa kiungu katika hali yakufanya maamuzi ya hekima, katika hali ya kujua mapenzi ya Mungu, katika hali ya kuwahudumia wengine, na katika hali ya kukua kiroho. Bibilia ni neno la Mungu kwetu sisi. Bibilia ni muongozo muhimu wa Mungu katika hali ya kuishi maisha yanayo mpendeza ye (Mungu) na kututosheleza sisi.

4. Jenga uhusiano na watu watakao kusaidia kiroho

1Wakorintho 15:33 yasema, “Msidanganyike; mazungumzo mabaya huharibu tabia njema.” Bibilia iko na tahadhari kuhusu ushawishi “mbaya” watu wanaweza kuwa nao juu yetu. Kutumia wakati na wale ambao wanajihusisha katika vitendo hivyo. Tabia za wale ambao tuko nao zitatuambukiza. Hii ndiyo sababu yakuwa ni muhimu tutangamane na watu wanao mpenda Bwana na wana wajibika kwake.

Jaribu kutafuta rafiki mmoja au wawili, labda kwa kanisa yako, ambao wanaweza kukusaidia na kukutia changamoto (Waebrania 3:13;10:24). Waulize rafiki zako wakuajibishe kuhusu wakati wako wa kutafakari, matendo yako na mwenendo wako na Mungu. Uliza kama unaweza kuwafanyia hivyo pia. Hii haimaanishi yakuwa uwachane na marafiki zako wote ambao hawajamjua Yesu Kristo kama mwokozi wao. Endelea kuwa rafiki yao na uwapende. Kwa ufupi wafahamishe yakuwa Yesu amebadilisha maisha yako na huwezi kuyafanya tena yote, yale uliyo kuwa ukiyafanya. Muulize Mungu akupe nafasi ya kumshiriki Yesu pamoja na marafiki zako.

5. Batizwa (Ubatizwe)

Watu wengi wanakosa kufahamu maana ya ubatizo. Neno “ Kubatiza” inamaanisha kuzamisha au kutosa majini. Ubatizo ndiyo njia ya kibibilia ya kujitambulisha hadharani imani yako mpya ndani ya Kristo na jukumu lako la kumfuata yeye. Kitendo cha kuzamishwa ndani ya maji inamaanisha kuzikwa pamoja na Kristo. Kitendo cha kutoka ndani ya yale maji inadhihirisha kufufuka kwa Kristo. Kubatizwa ni kujitambulisha wewe mwenyewe na kifo cha Yesu,maziko na ufufuo (Warumi 6:3-4).

Ubatizo sio ukuokoao.Ubatizo haukuondolei dhambi zako. Ubatizo ni hatua tu ya utiifu, hali ya kujitambulisha hadharani kuhusu imani yako ndani ya Kristo pekee kwa wokovu. Ubatizo ni muhimu kwasababu ni hatua ya utiifu-hadharani ukijitambulisha imani yako ndani ya Kristo na jukumu lako kwake yeye. Kama uko tayari kubatizwa,zungumza na Mchungaji.

English



Rudi kwa ukurasa wa nyumbani wa Kiswahili

Nimeweka imani yangu kwa Yesu … sasa ni fanyeje?
Shiriki ukurasa huu: Facebook icon Twitter icon Pinterest icon Email icon
© Copyright Got Questions Ministries