settings icon
share icon
Swali

Je, nitawezaje kuacha kufurahisha watu?

Jibu


Kufurahisha watu ni nguvu ya motisha ambayo inamfanya mtu kufanya maamuzi kulingana na kiwango cha kibali ambacho wanaamini watapokea. Inayohusiana na kufurahisha watu ni utegemezi na kuwezesha; ndani ya mpango wa kibiblia, kufurahisha watu kunakaribiana na ibada ya sanamu.

Wanaofurahisha watu wamejifunza kwamba inapendeza kupendwa na wengine, kwa hivyo wanaelekeza maneno na matendo yao katika mwelekeo ambao utatoa kibali zaidi. Nje, wanaofurahisha watu wanaonekana wasio na ubinafsi, wanyenyekevu na wakarimu. Hata hivyo, kwa ndani, hawana usalama na wanaamini kwamba kibali ni sawa na thamani. Hatimaye wanapata kwamba kujaribu kufurahisha watu kila wakati sio kitu cha kuchokesha tu, bali haiwezekani. Baadhi ya wanaofurahisha watu wanaweza anza kuendesha mahusiano na hali ili waweze kupata uridhisho unaohusishwa na kuunda majibu ya kufurahisha watu wengine. Kwa hivyo neno kufurahisha watu kwa kweli ni jina lisilo sahihi. Wanaofurahisha watu wanatamani kufurahisha kila mtu kwa sababu wanajiribu kujifurahisha wenyewe.

Watu wengine, kiasili, ni wepesi zaidi katika kufurahisha watu. Wanaofanya vile inavyotakikana, wanaochukuliwa rahisi na fikra mara nyingi wana ufahamu wa majibu ya watu wengine, kwa hivyo wanapima maneno na chaguzi hili kuepuka maoni ya kinyume. Wakati mwingine wanachukulia tabia hii kama njema, wakilinganisha ile yao ya kufurahisha watu na matendo yasio ya ubinafsi ya Bwana Yesu Kristo (ona Matendo 10:38). Hata hivyo, tofauti kati ya huduma isiyo ya ubinafsi ya Yesu na matendo ya wanaofurahisha watu ni nia. Yesu aliishi kumsifu na kumtii Baba Yake (Yohana 8:29). Alipenda, akatoa, na kuhudumia watu, lakini pia hakuogopa kusema kile kilichohitajika kusemwa, hata wakati watu walikasirika. Mara nyingi alikemea watu mbele ya umma kwa unafiki wao na kwa kukosa Imani (kwa mfano, Mathayo 23:15). Hakujali jinsi wasikilizaji Wake wangepokea maneno Yake. Alinena hasa kile kilihitajika kusemwa, hata wakati kilisababisha kifo Chake (Marko 15:1-2; Yohana 18:37). Yesu alikuwa kinyume cha wanaofurahisha watu.

Tunaweza chukua hatua ya kuacha tabia ya kufurahisha watu, kwanza kwa kuikubali kama dhambi. Wakati nguvu yetu ya kutuongoza ni umaarufu, tumegeuza miungu, na hiyo ni ibada ya sanamu. Wakati tunaruhusu chochote kutudhibiti badala ya Roho Mtakatifu, mioyo yetu inasimamisha hekalu kwa miungu inayoshindana (Waefeso 5:18; Wagalatia 5:16, 25). Kutafuta sifa kutoka kwa binadamu walioshindwa badala ya kutafuta kibali kutoka kwa Mungu ni makosa. Yohana 12:43 inatuambia kwamba, hata wakati wa siku za Yesu, watu wengine waliamini ujumbe Wake lakini wakakataa kumfuata kwa sababu “walipenda utukufu wa wanadamu kuliko utukufu wa Mungu.” Kufurahisha watu inaweza sababisha utengano wa milele kutoka kwa Mungu wakati tunairuhusu kuamru chaguzi zetu.

Tanapotambua mwelekeo wetu wa kufurahisha watu kama dhambi na kutubu, lazima tutafute motisha badala. 1 Wakorintho 10:31 inatuambia kwamba kiini chetu katika kila kitu kinapaswa kumtukuza Mungu. Wakati tunaendeleza uhusiano wa karibu na Yeye kupitia kuweka Imani ndani ya Yesu, anakuwa zingatio letu. Tunageuza utii kutoka kujiabudu wenyewe hadi kuabudu Mungu. Lengo letu sio kujifurahisha wenyewe lakini ni kumfurahisha Yeye (Wakolosai 1:10). Tunapata uhuru wakati tunavunja msimamo wa wanaofurahisha watu wakonayo kwa maisha yetu. Badala ya kujaribu kufurahisha mamia ya sauti, tunahitajika kusikiza moja tu (Yohana 10:27). Mwisho wa kila siku, ni swali moja tu la kufaa kwa Mkiristo: “Je, Bwana, leo nilikuwa wa kukufurahisha jinsi ninavyojua?” Wakati jibu ni “ndio” tunaweza jiburudisha katika furaha ya Mungu. Tunapata uthibitisho wakati anasema sisi ni nani.

Hatua nyingine muhimu katika kushinda tabia ya kufurahisha watu ni kulinda mioyo yetu dhidi ya tamaa. Wivu inachaza wanaofurahisha watu wakati tunatamani kibali au umaarufu wa mtu mwingine. Hii ni dhahiri sana kwa vijana kwa kupenda wanamuziki na wanaspoti, lakini watu wazima wana hatia kwa hili pia. Wanaofurahisha watu ambao msingi wao ni juu ya wivu emeenea zaidi ya ufahamu wetu, na wengi wetu tunapata athari yake mahali katika maisha yetu.

Kufurahisha watu inatuzuia kuwa kile Mungu alituita tuwe. Inatunyamazisha wakati tunapaswa kuongea na kututishia wakati tunaongea. Aina ya mwenye hila ya wanaofurahisha watu katika kanisa leo ni utabiri katika 2 Timontheo 4:3: “Maana utakuja wakati watakapoyakataa mafundisho yenye uzima; ila kwa kuzifuata nia zao wenyewe watajipatia waalimu makundi makundi, kwa kuwa wana masikio ya utafiti.” Wahubiri ambao matamanio yao kukusanya watu wengi na kuuza vitabu wanakuza dhambi ya kufurahisha watu na kuita “huduma.” Kukusanya watu si dhambi, lakini wakati motisha ni kufurahisha watu na sio Mungu, kuna shida. Ikiwa mitume walikuwa wakufurahisha watu, hawangeuuawa kwa sababu ya imani yao.

Hatuwezi tumikia mabwana wawili (Mathayo 6:24). Hatuwezi jitolea vikamilifu kwa injili ya Kristo na pia kujitolea vikamilifu kwa kibali cha watu. Haviwezi tangamana. Hiyo ni mojawapo ya sababu Yesu alifanya uanafunzi kuwa njia nyembamba sana. Alisema, “Mtu ye yote akitaka kunifuata, na ajikane mwenyewe, ajitwike msalaba wake kila siku,anifuate” (Luka 9:23). Sehemu ya kujikana wenyewe ni kusulubisha mahitaji yetu ya kufurahisha watu na kuwachukulia kama sisi (1 Wathesalonike 2:3-5; Wagalatia 1:10).

Tunasema na Petro, “Imetupasa kumtii Mungu kuliko wanadamu!” (Matendo 5:29). Sio kazi yetu kufanya watu wawe na furaha. Badala yake, tunapaswa kuishi kwa watu bora, kumtumikia Bwana kwa njia ye yote ametuita, kufa kila siku kwa matamanio yetu ya kibinafsi, na kupokea zawadi yetu kutoka Kwake (1Wakorintho 4:5). Wakati hilo ndio lengo letu la maisha, tutaacha kuwafurahisha watu.

English



Rudi kwa ukurasa wa nyumbani wa Kiswahili

Je, nitawezaje kuacha kufurahisha watu?
Shiriki ukurasa huu: Facebook icon Twitter icon Pinterest icon Email icon
© Copyright Got Questions Ministries