settings icon
share icon
Swali

Je! Ina maana gani kuwa “kuishi ni Kristo” (Wafilipi 1:21)?

Jibu


Wafilipi 1:21 inasema, “Kwa maana kwangu mimi, kuishi ni Kristo, na kufa ni faida.” Watu wengi huzingatia sehemu ya pili ya mstari, “kufa ni faida,” na kutafakari furaha ya mbinguni. Lakini hatupaswi kupuuza sehemu ya kwanza. Umuhimu wa kifungu “kuishi ni Kristo” hauwezi kutiwa chumvi. Kifungu hiki kinapaswa kuwa kiini kwa kila maisha ya Kikristo.

Katika usemi huu, mtume Paulo anasema kwamba kila kitu ambacho amejaribu kuwa, na kila kitu alichotazamia kilielekeza kwa Kristo. Tangu wakati wa kuokoka kwa Paulo hadi kifo chake, kila hatua aliyoifanya ililenga kuendeleza ufahamu, injili, na kanisa la Kristo. Lengo kuu la Paulo lilikuwa kumletea Yesu utukufu.

“Kuishi ni Kristo” inamaanisha kwamba tunatangaza injili ya Kristo. Paulo alihubiri katika masinagogi; alihubiri kando ya mito; alihubiri akiwa mfungwa; alihubiri akiwa mtume; alihubiri akiwa mtengeza mahema. Ujumbe wake ulikuwa ule ule: “Yesu Kristo aliyesulubiwa” (1 Wakorintho 2:2). Alileta ujumbe wa dhabihu ya Kristo kwa wafalme, askari-jeshi, wakuu wa serikali, makuhani, na wanafalsafa, Wayahudi na watu wa Mataifa, wanaume na wanawake. Kihalisi angehubiri kwa mtu yeyote ambaye angemsikiliza.

“Kuishi ni Kristo” inamaanisha kwamba tuige mfano wa Kristo. Kila kitu ambacho Yesu alifanya na kusema, ndivyo Paulo alitaka kufanya na kusema. Kanisa lilinufaika kutokana na mfano wake wa kimungu: “Igeni mfano wangu, kama ninavyouiga mfano wa Kristo” (1 Wakorintho 11:1). Yensu angefanya nini? Hilo ndilo tunataka kufanya.

“Kuishi ni Kristo” inamaanisha kwamba tunatafuta ufahamu wa Kristo. Tunataka kumjua Kristo vyema na bora kila siku. Sio kundi la mambo ya ukweli kuhusu, bali Kristo Mwenyewe. ”Nataka nimjue Kristo na uweza wa kufufuka kwake na ushirika wa mateso yake, ili nifanane naye katika mauti yake, ili kwa njia yoyote niweze kufikia ufufuo wa wafu” (Wafilipi 3:10-11).

“Kuishi ni Kristo” inamaanisha kwamba tuko tayari kuacha kila kitu kinachotuzuia kumpokea Kristo. Ushuhuda wa Paulo kuhusu jambo hili: “Lakini mambo yale yaliyokuwa faida kwangu, sasa nayahesabu kuwa hasara kwa ajili ya Kristo. Zaidi ya hayo, nayahesabu mambo yote kuwa hasara tupu nikiyalinganisha na faida kubwa ipitayo kiasi cha kumjua Kristo Yesu Bwana wangu, ambaye kwa ajili yake nimepata hasara ya mambo yote, nikiyahesabu kuwa kama mavi ili nimpate Kristo. Nami nionekane mbele zake bila kuwa na haki yangu mwenyewe ipatikanayo kwa sheria, bali ile ipatikanayo kwa imani katika Kristo, haki ile itokayo kwa Mungu kwa njia ya imani” (Wafilipi 3:7-9). Tunashikilia ahadi ya Bwana wetu katika Marko 10:29-30 kwamba dhabihu zetu kwa ajili ya Yesu zitalipwa mara mia moja.

“Kuishi ni Kristo” inamaanisha kwamba Kristo ndiye kitovu chetu, lengo letu, na hamu yetu kuu. Kristo ndiye kitovu cha akili yetu, moyo, mwili, na roho zetu. Kila kitu ambacho tunafanya, tunafanya kwa ajili ya utukufu kwa Kristo. Tunapokimbia “mbio ambazo tuliwekewa,” tunaweka kando dhambi inayotuzinga na vikengeusha-fikira vya ulimwengu, “tumtazame Yesu sana” (Waebrania 12:1-2). Yeye ndiye uhai wetu.

English



Rudi kwa ukurasa wa nyumbani wa Kiswahili

Je! Ina maana gani kuwa “kuishi ni Kristo” (Wafilipi 1:21)?
Shiriki ukurasa huu: Facebook icon Twitter icon Pinterest icon Email icon
© Copyright Got Questions Ministries