settings icon
share icon
Swali

Jinsi gani naweza leta wasiwasi na matatizo yangu yote kwa Mungu?

Jibu


Mara nyingi kwa Wakristo, ni ukweli wa kufadhaisha kwamba ingawa sisi ni wa Mungu kupitia imani katika Kristo, bado tunaonekana kupata matatizo sawa na yale ambayo yalitukumba kabla hatujapata wokovu. Mara nyingi tunakata tamaa na kuzama katika shida za maisha. Kwa vile Agano la kale na jipya linashughulikia tatizo hili kwa njia ile ile, inaonyesha kwamba Mungu anajua matatizo na wasiwasi ni jambo lisiloepukika katika maisha haya. Kwa neema yake, Mungu ametupa suluhisho sawa na lile ambalo alitoa katika Zaburi na Barua ya Petro. “Mtwike Bwana fadhaa zako, naye atakutegemeza,

hatamwacha kamwe mwenye haki wake aanguke.” (Zaburi 55:22), na “huku mkimtwika yeye fadhaa zenu zote, kwa maana yeye hujishughulisha sana kwa mambo yenu” (1 Petro 5:7).

Ndani ya aya hizi mbili kuna ukweli wa ajabu: Mungu atatuhifadhi, hatatuachilia tuanguke na anatulinda. Tukichukua kila moja kwa wakati mmoja, tunaweza kuona kwamba Mungu anatangaza uwezo wake wa nia yake ya kuwa nguvu na msaada wetu-kihisia, kiutendaji na kiroho. Yeye anaweza( na bora zaidi, yuko tayari!) kuchukua kila kitu kinachotishia kutuvunja moyo na kukitumia kwa faida yetu. Ameahidi “kuifanyia kazi pamoja mambo yote kwa wema wa wale wampendao, wale waliitwa kwa kusudi lake.” Hata wakati tunamkana, yeye bado anafanya kazi kwa wema wetu na utukufu wake. Na pia ameahidi kwamba hatayaruhusu majaribu kuwa makubwa sana kwetu kwamba hatuwezi kuvumilia kwa nguvu ya Kristo, na atatoa njia ya kutoroka (Wakorintho 10:13). Kwa hili, anamaanisha kwamba hataturuhusu tuanguke, kama alivoahidi katika zaburi 55:22.

Kauli ya tatu, “anakujali wewe,” inatupa motisha kando na ahadi zake nyingine. Mungu wetu si mwenye uongo, asiye na hisia au mwenye ukora. Bali, yeye ni Baba yetu wa mbinguni mwenye upendo na moyo wake ni mpole kwa watoto wake. Yesu anatukumbusha kwamba kama vile baba wa dunia hii hangemyima mtoto wake mkate, vivyo hivyo Mungu ameahidi kutupa “vitu vizuri” tunapomwomba (Mathayo 7:11).

Kwa roho ya kuomba vitu vizuri, kwanza tunapaswa kusali na kumwambia Bwana kwamba tunasikia kile anachosema katika Yohana 16:33, ambapo Yesu anasema, “Hayo nimwaambieni mpate kuwa na amani ndani yangu. Ulimwenguni mnayo dhiki; lakini jipeni moyo, mimi nimeushinda ulimwengu.” Kisha tunapaswa kumwomba Bwana atuonyeshe jinsi alivyoyashinda matatizo yetu, wasiwasi wetu, hasira zetu, hofu zetu na hatia zetu.

Bwana anatufunulia kupitia Neno lake, Biblia, kwamba tunaweza kuwa na “shangwe,” ambayo tunaweza:

1) Furahi katika shida zetu kwa sababu Mungu atatumia shida izo kwa manufaa yetu. “Si hivyo tu, bali twafurahi pia katika mateso, kwa sababu tunajua kuwa mateso huleta saburi, nayo saburi huleta uthabiti wa moyo, na uthabiti wa moyo huleta tumaini” (Warumi 5:3-4);

2) Ona “wasiwasi” zetu kama fursa ya kufanya yale ambayo yameandikwa katika Mithali 3:5-6, “Mtumaini Bwana kwa moyo wako wote, wala usizitegemee akili zako mwenyewe; katika njia zako zote mkiri yeye,Naye atayanyosha mapito yako”;

3) Punguza hasira zetu kwa kutii waefeso 4:32, “tena iweni wafadhili ninyi kwa ninyi, wenye huruma, mkasameheane kama na Mungu katika Kristo alivyowasamehe ninyi”; na

4) Shughulikia hisia sozote za dhambi kwa kuamini na kutenda kulingana na ukweli wa 1 Yohana 1:9, “Tukiziungama dhambi zetu, Yeye ni mwaminifu na wa haki hata atuondelee dhambi zetu, na kutusafisha na udhalimu wote.” Matatizo yetu yote yanaweza kushindwa kwa imani katika neno la Mungu.

Mungu ni mkubwa kuliko wasiwasi na matatizo yetu yakiekwa pamoja, na lazima tuelewe hili ili tupate ushindi katika maisha yetu.Kila mtu anapata taabu hizi, kwa sababu Biblia inafundisha kwamba majaribu ni “ya kawaida” kwa binadamu ( 1 Wakorintho 10:13). Hatupaswi kumruhusu shetani kutudanganya kuwa matatizo yetu yote ni makosa yetu, shida zetu zote zitapita, hasira yetu yote inatuhukumu, au kwamba hatia yetu yote inatoka kwa Mungu. Ikiwa tunatenda dhambi na kukiri, Mungu anasamehe na kutakasa. Hatupaswi kuwa na aibu, bali tumwamini Mungu kwamba yeye husamehe na kutakasa. Hakuna dhambi zetu nzito sana ambazo Mungu hawezi kuziondoa kutoka kwetu na kuzitupa baharini( angalia Zaburi 103:11-12).

Kwa kweli, hisia zinatokana na mawazo, kwa hivyo, ingawa hatuwezi badilisha jinsi tunavyojisikia, tunaweza badilisha jinsi tunavyofikiria. Na hii ndio Mungu anataka tufanye. Kwa mfano, katika Wafilipi 2:5, Wakristo wanahimizwa, “Iweni na nia iyo hiyo ndani yenu ambayo ilikuwamo pia ndani ya Kristo Yesu.” Katika wafilipi 4:8, Wakristo wanaambiwa “Hatimaye ndugu zangu, mambo yoyote yaliyo ya kweli, yoyote yaliyo ya staha, yoyote yaliyo ya haki, yoyote yaliyo safi, yoyote yenye kupendeza, yoyote yenye sifa njema; ukiwapo wema wowote, ikiwapo sifa nzuri yoyote, yatafakarini hayo.” Katika Wakolosai 3:2, tumeambiwa “Yafikirini yaliyo juu, siyo yaliyo katika nchi.” Kwa hivyo, tunapofanya hivi, hisia zetu za hatia zinapungua.

Kwa hivyo, kila siku tunapochukua hatua moja baada ya nyingine, tunapaswa kuomba Neno la Mungu lituongoze, tusome au kusikiliza Neno la Mungu, na kutafakari Neno la Mungu wakati wa matatizo, wasiwasi na shida za maisha zinapotokea. Siri ya kumwachia Kristo vitu vyetu sio siri kabisa- ni kumwomba Yesu achukue mzigo wa “dhambi ya asili” na kuwa mwokozi wetu (Yohana 3:16), pamoja na kujitolea kwa Yesu kama Bwana wetu katika maisha ya kila siku.

English



Rudi kwa ukurasa wa nyumbani wa Kiswahili

Jinsi gani naweza leta wasiwasi na matatizo yangu yote kwa Mungu?
Shiriki ukurasa huu: Facebook icon Twitter icon Pinterest icon Email icon
© Copyright Got Questions Ministries