settings icon
share icon
Swali

Je, ni kwa nini inatajwa “mkubali Kristo” wakati wa kuinjilisha na ile hali hakujatajwa katika Biblia?

Jibu


Tangu enzi ya Agano Jipya, Wakristo wameona haja ya kubuni maneno mapya ili kurahisisha au kueleza mafundisho mbalimbali. Tunarejelea Utatu na injili ya kwanza, ingawa hakuna neno kama hilo linalopatikana katika Biblia. Ingawa “kumkubali Kristo” ni kifungu ambacho hakipatikani katika Biblia, kina msingi wa kibiblia kama vile Utatu una msingi katika Biblia.

Yesu na wafuasi wake mara nyingi waliita wokovu na kule kuendelea kujazwa kwa Roho Mtakatifu “karam”. Kwa mfano, Yesu alimwambia mwanamke kisimani hivi: “Kama ungelijua karama ya Mungu, naye ni nani anayekuambia, Nipe maji ninywe, wewe ungelimwomba yeye, naye angelikupa maji yaliyo hai” (Yohana 4:10). Paulo alisema “Kwa maana mshahara wa dhambi ni mauti, bali karama ya Mungu ni uzima wa milele katika Kristo Yesu Bwana wetu” (Warumi 6:23).

Kwa ufafanuzi, tuzo hailazimishwi- lakini ni lazima ikubalike. Zawadi inaweza kataliwa. Yohana Mbatizaji alisema kuhusu Yesu, “Yeye hushuhudia yale aliyoyaona na kuyasikia, lakini hakuna yeyote anayekubali ushuhuda wake. Lakini yeyote anayekubali huo ushuhuda anathibitisha kwamba, Mungu ni kweli” (Yohana 3:32-33). Neno kukubali hapa limetafsiriwa kutoka neno hilo hilo la Kigiriki ambalo linatafsiri wa “chukua” katika Ufunuo 22:17: “Yeyote mwenye kiu na aje, na kila anayetaka na anywe maji ya uzima bure.” “Chukua” “kubali” “pokea”- hili ndilo tunapaswa kufanya na zawadi ya bure ya Mungu. Wokovu umetolewa, lakini ni lazima tuukubali ili tuweze kupokea zawadi. Kwa kuwa tunafanya hivyo kwa kudhihirisha imani katika Kristo, kifungu/kishazi “mkubali Kristo” ni kusema kwa kifupi “weka imani yako katika Kristo na upokee wokovu Wake.”

Lengo la kutumia maneno kama “mkubali Kristo” ni kuwazilisha ukweli kwa ufanisi zaidi kwa mtu aliye na uelewo finyu wa kibiblia. Maadamu neno li sahihi kitheolojia na linasaidia kuelewa, linahitaji kuwa sehemu ya msamiati wa kibiblia. Ikiwa wakati wa uinjilisti, neno fulani linasababisha kutokuelewana, basi ni vizuri kukoma kutumia neno hilo linalochanganya na kueleza kueleza ukweli kutoka kwa Maandiko kwa subira. Ingawa kishazi “mkubali Kristo” hakionekani katika Biblia dhana ya kupokea karama inaonekana, na kishazi kinaonekana kufanya kazi vizuri katika muktadha nyingi za uinjilisti.

English



Rudi kwa ukurasa wa nyumbani wa Kiswahili

Je, ni kwa nini inatajwa “mkubali Kristo” wakati wa kuinjilisha na ile hali hakujatajwa katika Biblia?
Shiriki ukurasa huu: Facebook icon Twitter icon Pinterest icon Email icon
© Copyright Got Questions Ministries