settings icon
share icon
Swali

Je, ni msingi gani wa kusikia sauti ya Mungu?

Jibu


Watu wengi wanataka kusikia sauti ya Mungu wakati wanakumbana na uamuzi wa kufanya. Ikiwa tu Mungu anaweza kuzungumza nao na kuwambia ni chaguo gani watafanya au mwelekeo watachukua. Watu wengi watadai walisikia sauti ya Mungu, wakisema, “Mungu aliniongoza kufanya hili,” wakati kwa kweli ilikuwa ni fikira na tamaa yao wenyewe ambayo iliwaongoza katika mwelekeo maalum.

Njia ya msingi ambayo Mungu anazungumza nasi hii leo ni kupitia Neno Lake lililofichuliwa na kuandikwa. Wakati tunataka kusikia sauti ya Mungu, tunapaswa kutafuta katika Biblia. Mapenzi ya Mungu mengi kwa Maisha yetu tayari yamefichuliwa vikamilifu katika kurasa zake, na ni jambo tu la utii wetu kwake. Maandiko yote ni mapenzi ya Mungu, lakini kuna sehemu chache katika Maandiko ambazo hasa zimetumia neno mapenzi ya Mungu, ambayo labda itafurahisha mtu ambaye anataka kusikia sauti ya Mungu:
• 1 Wathesalonike 5:18: “Shukuruni kwa kila jambo: maana hayo ni mapenzi ya Mungu kwenu katika Kristo Yesu.”
• 1 Wathesalonike 4:3: “Maana haya ndiyo mapenzi ya Mungu, kutakaswa kwenu, mwepukane na uasherati.”
• 1 Petro 2:12-15: “Mwe na mwenendo mzuri kati ya Mataifa, ili, iwapo huwasingizia kuwa watenda mabaya, wayatazamapo matendo yenu mazuri, wamtukuze Mungu siku ya kujiliwa. Tiini kila kiamriwacho na watu, kwa ajili ya Bwana; ikiwa ni mfalme, kama mwenye cheo kikubwa; ikiwa ni wakubwa, kama wanaotumwa naye ili kuwalipiza kisasi watenda mabaya na kuwasifu watenda mema. Kwa sababu ndiyo mapenzi ya Mungu, kwamba kwa kutenda mema mzibe vinywa vya ujinga vya watu wapumbavu.”

Vifungu vingine pia huturuhusu kusikia sauti ya Mungu, hata kama havitumii maneno mapenzi ya Mungu. Lakini, kwa kuchukua vifungu vitatu vya hapo juu, tunajua kwamba Mkristo anapaswa kutoa shukurani kila wakati katika kila hali, kuepuka uasherati, na kuishi maisha ya kuiga mfano. Ikiwa Mkristo hatafuata haya maagizo ya wazi ambayo yamepeanwa moja kwa moja na Mungu kupita Maandiko yaliyoongozwa, kwa nini atarajie kusikia taarifa zaidi kutoka kwa Mungu? Ikiwa unataka mwelekeo zaidi kutoka kwa Mungu, tii kile mbacho tayari amekuambia. Moyo mbayo uko tayari kusikiza na kutii ndio msingi wa kusikia sauti ya Mungu.

Njia ya msingi ambayo Mkristo anasikia sauti ya Mungu ni kupitia kusoma na kujifunza Maandiko na kisha kuyatii na kufuta ambacho Maandiko yanasema. Mara nyingi watu wanategema “uongozi wa Roho Mtakatifu,” ambayo imeongelewa katika Warumi 8:14. Katika muktadha, kifungu kinazungumza juu ya Roho kutuongoza kutoka kwa matendo ya dhambi na kwa Imani katika uhusiano wetu na Mungu kama Baba. Roho Mtakatifu hawezi kamwe kutuongoza kinyume na Maandiko. Ikiwa mtu anazingatia kufanya uasherati, Roho ataongoza kwa mwelekeo mmoja tu—kueleka uaminifu wa ndoa. Roho anaweza leta msitari kama 1 Wathesalonike 4:3 kwa kufikiria mtu ambaye anajaribiwa. Wakati Roho anaongoza, hatoi taarifa “mpya” kwa vile anavutia mioyo yetu na ukweli ambao Mungu amefichua katika Maandiko na kuhutumia katika hali yetu. Ikiwa mtu atasema, “Mungu aliniambia” au “Roho aliniongoza kufanya hili na lile,” na hatua iliyochukuliwa ni kinyume na Maandiko, tutakuwa na hakika kwamba huyo mtu amekosea.

Pia tunaweza kusikia sauti ya Mungu kwa vile Mungu anazungumza kupitia watu wengine. “Pasipo mashauri makusudi hubatilika; bali kwa wingi wa mashauri huthibithika” (Methali 15:22). Washauri wazuri wanaweza kutusaidia kuona hali na macho mpya. Tena, Biblia ni msingi. Mahubiri ya Kibiblia na vifaa vya kibiblia vya kikristo vinaweza kuwekwa katika aina ya “washauri”. Neno la Mungu ndilo udhibiti. Ikiwa kundi la washauri limshauri mtu kufanya kitu kinyume na Maandiko, basi wote wemekosea, haijalishi masomo yao; hata hivyo, ikiwa washsuri watasaidia mtu kuelewa na kufuata Maandiko, basi watakuwa wa msaada. Washauri wa Kimungu wanaweza mara kwa mara kuona sehemu ambazo mtu ni kipofu kwazo. Kundi la washauri wanaweza kutambua kwamba mtu natafuta kisikia sauti ya Mungu kuhusu mpango maalum, kwa hakika anatafuta kibali ya ajenda yake mwenyewe binafsi.

Njia nyingine ya kusikia sauti ya Mungu ni kwa kuomba na kuomba hekima: “Lakini mtuwa kwenu akipungukiwa na hekima, na aombe dua kwa Mungu, awapaye wote, kwa ukarimu, wala hakemei; naye atapewa” (Yakobo 1:5). Wakati Mkristo anakumbana na hali ngumu na anahitaji kusikia kutoka kwa Mungu, Mkristo anapaswa kuomba hakima ambayo Mungu anahidi kutoa. Hekima hii atimaye hutoka kutoka kwa Mungu, lakini inaweza kuja kupitia neno la rafiki; kupitia mahubiri, makala, au kitabu; au kutoka kwa uhamasisho wa ndani wa Roho Mtakatifu. Tena, Neno la Mungu lililoandikwa ni kiwango ambacho mafikirio yote, matendo yote, dhana zote, na hisia sote lazima zihukumiwe.

Katika siku hizi za wanabii waliojitangaza na ukuzaji wa “maono mpya” kutoka kwa Mungu, watu mara nyingi huchukulia kimakosa sauti ya Mungu kwa mafikirio yao wenyewe au mapendekezo ya watu wengine. Ikiwa unasikia sauti ya Mungu, basi ujumbe kila wakati utakuwa kulingana na Maandiko. Sisi sote tunapaswa kuwa makini sana ili tusitoe habari za kupotosha za Mungu. Badala ya kusema, “Mungu aliniambia hili,” mbinu bora inaweza kuwa kusema, “nafikiria Mungu labda anasema hivi—unafikiaje?”

Watu mara nyinyi wanataka kusikia neno maalum kutoka kwa Mungu wakati tayari amezungumza kwa jumla. Kwa mfano, mtu labda anazingatia chaguo la ikiwa atapeleka familia safari fupi ya kazi au likizo pwani. Pengine neno maalum kutoka kwa Mungu si muhimu. Cha muhimu ni hekima. Ni safari gani itafaidi familia? Ni safari gani itafaidi zaidi ufalme wa Mungu? Familia itafaidi kwa kujenga ufalme. Ufalme utafaidi kutoka kwa familia yenye nguvu. Moja yao itakuwa chaguo mzuri. Sababu zingine kama vile gharama na hali ya sasa ya familia lazima izingatiwe. (Je, watoto ni binafsi na wenye haki ili kuona jinsi watu wengine wanaishi? Je, familia imekuwa chini ya msukumo na wanahitaji kutoka na kupumzika? Je, gharama ni ya kuweza kulinganishwa? Ikiwa ni la, ni gani wanaweza mudu?). Ikiwa wataenda pwani, wanatafuta fursa ya kushiriki Imani yao na kuwa wa uhamasisho kwa waumini wengine. Ikiwa wataenda safari ya kazi, wanatafuta njia za kujenga mahusiano kati yao na kujifurahisha wenyewe kama familia. Chaguzi zote ni nzuri. Wala kwa asili si dhambi. Hatimaye, mme na mke wanaelewana na wanajirusha wenyewe kwa moyo wote, wakiamini kwamba, ikiwa uamuzi ni mbaya, Mungu kwa namna fulani ataifanya wazi kwao kwamba wafanye kitu tofauti. Atafanyaje hili? Labda sio kupitia sauti ya kusikika lakini kupitia muungano wa hali, ushauri kutoka kwa watu wengine, tathmini ya vipaumbele vyao kwa msingi wa Neno la Mungu, na kukosa Amani ya ndani ya Roho Mtakatifu.

English



Rudi kwa ukurasa wa nyumbani wa Kiswahili

Je, ni msingi gani wa kusikia sauti ya Mungu?
Shiriki ukurasa huu: Facebook icon Twitter icon Pinterest icon Email icon
© Copyright Got Questions Ministries