settings icon
share icon
Swali

Ni njia gani nzuri ya kusoma Bibilia?

Jibu


Kupata maana ya maandiko in mojawapo la kazi muimu sana mshirika ako nayo katika maisha haya. Mungu hatwambii kwamba lazima tusome Bibilia. Lazima tuichunguze na tuweze kuilezea vizuri (2 Timotheo 2:15). Kuisoma Bibilia ni jambo gumu. Kuyapitia juu juu maandiko wakati mwingine waweza kuleta mwelekeo mbaya. Kwa hivyo, ni muimu kuelewa mambo makuu kwa kupata maana kamili ya maandiko.

Kwanza, mwanafunzi wa Bibilia lazima aombe na kumhulizia Roho Mtakatifu kumpa uwezo wa kuelewa, kwa maana hiyo ndiyo kazi yake. “Lakini yeye atakpokuja, huyo Roho wa kweli, atawaongoza awatie kwenye keweli yote; kwa maana atanena kwa shauri lake mwenyewe, lakini yote akatakayoyasikia atayanena, na mambo yajayo atawapasha habari yake” (Yohana 16:13). Kama vile Roho Mtakatifu aliwaongoza wanafunzi wa Yesu kuandika Agano Jipya, vilevile atatuongoza kuyaelewa maandiko. Kumbuka, Bibilia ni kitabu cha mungu, na yatupasa kumuuliza kinamaanisha nini. Kama wewe in Mkristo, mwandishi wa Bibilia-Roho Mtakatifu- anakaa ndani yako, na anataka uelewe chenye alikiandika.

Pili, hatustahili kuing’oa aya kutoka kwa maandiko mbali na zile zinazo izunguka na ujaribu kupata maana ya hiyo aya nche ya mkadhata. Kila mara lazima tusome aya zinazoizunguka na milanog ili tujue maana. Maandiko yote yatoka kwa Mungu (2 Timotheo 3:16; 2 Petero 1:21), Mungu aliwatumia watu kuandika. Hawa watu walikuwa na maudhui katika akili, lengo la kuandika, na hali fulani walikuwa wakiitatua. Lazima tusome historia ya kitabu cha Bibilia tunachokichunguza, ili tupate, nani alikiandika kitabu, aliwaandikia nani, na ni kwa nini alikiandika, kiliandikwa lini, na ni kwa sababu gani kiliandikwa. Pia lazima tuache maandiko yajinenee yenyewe. Wakati mwingine watu wataweka maana yao kwa maneno ili wapate elezo wanalolitaka.

Tatu, tusijaribu kujitegemea wakati tunaposoma Bibilia. Ni ujeuri tunapofikiri hatuwezi pata kuyaelewa kitu chochote kutoka kwa kazi ya wengine waliyoisoma Bibilia mbele yetu. Watu wengine wanaisoma Bibilia na dhana kuwa Roho Mtakatifu amewapa watu karama ya roho mtakatifu kwa mwili wa Kristo. Mojawapo ya karama hizi ni ile ya ualimu (Waefeso 4:11-12); 1 Wakorintho 12:28). Hawa walimu wamepeanwa na Mungu ili wazaidie kuyaelewa maandiko na kuyatii. Ni kitu cha busara kila mara kuichunguza Bibilia na Wakristo wengine, mkupatiana jukumu la kuielewa na kuutumia ukweli wa neno la Mungu.

Kwa mukhutasari, ni njia ipi bora ya kuisoma Bibilia? Kwanza, kupitia maombi na unyenyekevu, lazima tumtegemee Roho Mtaktifu utupe uwezo wa kuelewa. Pili, lazima tuisome katika mkudhata wa ujumbe, tukitambua kwamba Bibilia yajieleza. Tatu, lazima tuheshimu juhudi za Wakristo wengine, waliopita na waliomo, wenye wamejaribu kuisoma Bibilia. Kumbuka, Mungu ndiye mwandishi wa Bibilia na anataka tuielewe.

English



Rudi kwa ukurasa wa nyumbani wa Kiswahili

Ni njia gani nzuri ya kusoma Bibilia?
Shiriki ukurasa huu: Facebook icon Twitter icon Pinterest icon Email icon
© Copyright Got Questions Ministries