settings icon
share icon
Swali

Je, ni kwa nini ni muhimu kuwa na sadikisho za kibinafsi?

Jibu


Mtu aliye na sadikisho za kibinafsi ana hakika kwamba jambo fulani ni la kweli na kushikilia kanuni hiyo, bila kujali hali na matokeo. Sadikisho za kibinafsi zinafunua mengi juu ya mtu ni nani.

Kuwa na sadikisho za kibinafsi ni muhimu ili kutuzuia tusishawishiwe na maoni ya wengine au kuyatii moja kwa moja. mtu asiye na sadikisho za kibinafsi atakuwa mwoga, asiye na maamuzi, na kupotoshwa kwa urahisi. Wakati umati unasema, “Hebu natumwasi Mungu,” inamgarimu mtu aliye na usadikisho wa kibinafsi kusimama na kusema, “La.” Shadraka, Meshaki na Abedngego walikuwa na sadikisho za kibinafsi dhidi ya kuabudu miungu ya uongo, na walishikilia msimamo wao dhidi ya kuabudu miungu ya uongo, na walishikilia msimamo wao dhidi ya wimbi la Babeli, wakisimama imara hata mbele ya hasria ya mfalme (Danieli 3).

Kila mtu ana maoni na vinavyompendeza, lakini mtu aliye na sadikisho hafanyi maoni yake kwa kutegemea matamanio ya kibinafsi au kwa faida ya kibinafsi. Mtu aliye na usadikisho wa kibanafsi ameyafikiria maswala hayo na anaishi na kusudi. Watu kama hao wana hakika juu ya kile wanachoamini, na wanasadiki mambo ya maana zaidi. Mtume Paulo alitazamia kwa hamu wakati ambapo waumini wengefikia ukomavu wa kiroho: “Ili tusiwe tena watoto wachanga, tukitupwatupwa huku na huku na kuchukuliwa na kila upepo wa mafundisho kwa hila za watu, kwa ujanja, kwa kufuata njia zao za udanganyifu” (Waefeso 4:14). Sehemu ya ukomavu ni kuwa na usakidikisho wa kibinafsi wa kutosha kutambua na kustahimili mafundisho ya uongo ya siku hizi.

Usadikisho wa kibanafsi unapaswa kuundwa kwa kutumia Biblia kama kiwango. Yale ambayo Biblia inahimiza, tunapaswa kuwa na usadikisho wa kibinafsi kuyahusu. Kile ambacho Biblia inakataza, tunapaswa kuwa na usadikisho wa kibinafsi dhidi yake. Kwa njia hii, Neno la Mungu hujulisha dhamiri zetu na lina mwanga kwa njia yetu (Zaburi 119:105). Sadikisho za kibinafsi hazipaswi kutegemea tu kile tunacho “hisi” juu ya jambo fulani. “Yeye ajitumainiaye mwenyewe ni mpumbavu, bali yeye atembeaye katika hekima hulindwa salama” (Mithali 28:26).

Biblia haishughulikii moja kwa moja kila hali. Kuunda sadikisho za kibinafsi juu ya masuala ambayo hayajaainishwa katika Maandiko kunahitaji sisi kutafuta kanuni zinazoongoza katika Neno (2 Timotheo 3:16-17; Yakobo 1:5). Biblia haitaji uavyaji mimba moja kwa moja, lakini inazungumza waziwazi kuhusu mambo kama vile mauaji na ulinzi wa wasio jiweza. Tunapojifunza na kujinyenyekeza kwa Neno la Mungu, tunajifunza kile ambacho Mungu ki sawa au sahihi (Waebrania 5:14). Tunapokomaa katika hekima na hukumu, sadikisho zetu za kibinafsi zitalingana na yale mambo ambayo ni bora kwa Mungu (Wafilipi 1:9-11; Warumi 12:1-2).

Kwa kuwa tunashughulika na sadikisho za kibinafsi, kuna baadhi ya masuala ambayo waumini tofauti wanaweza kuwa na sadikisho tofauti. Si masuala yote yamefichika au yako wazi, na si masuala yote yanaweza kupatikana katika mwongozo wa Biblia. Katika hali kama hizi, ni lazima tuache sheria ya upendo itawale. Paulo anatuambia tusiwe na ugomvi “si kwa kugombana na kubishana juu ya mawazo yake” (Warumi 14:1) kama vile kula vyakula fulani au kufanya siku moja kuwa takatifu zaidi kuliko siku nyingine. Tunapaswa kuwa na sadikisho za kibinafsi: “Basi kila mmoja awe na hakika na yale anayoamini” (aya ya 5), lakini lazima waache nafasi sadikisho za wengine: “Wewe ni nani hata umhukumu mtumishi wa mtu mwingine? Kwa bwana wake tu anasimama au kuanguka.…. Yeye anayehesabu siku moja kuwa takatifu kuliko nyingine, hufanya hivyo kwa kumheshimu Bwana. Naye alaye nyama hula kwa Bwana, kwa maana humshukuru Mungu, naye akataaye kula nyama hufanya hivyo kwa Bwana na humshukuru Mungu” (aya ya 4 na 6).

Sadikisho za kibinafsi ni muhimu kwa sababu zinatusaidia kusimama imara wakati ulimwengu hauna uhakika na unabadilika. Tunahitaji wanaume na wanawake walio na “kina cha maadili” katikati mwa kuchanganyikiwa wa kiadili unaotuzunguka. Sadikisho za kibinafsi hutuwezesha kusimama katika kweli na kutukumbusha kile kilicho cha maana. Zinatusaidia kuvumilia majaribu bila kuridhiana. Zinasafisha na kuthibitisha imani yetu.

English



Rudi kwa ukurasa wa nyumbani wa Kiswahili

Je, ni kwa nini ni muhimu kuwa na sadikisho za kibinafsi?
Shiriki ukurasa huu: Facebook icon Twitter icon Pinterest icon Email icon
© Copyright Got Questions Ministries