settings icon
share icon
Swali

Uhuru wa Mkristo-Bibia inasema nini?

Jibu


Uhuru wa Mkristo unapatikana ndani ya Biblia katika dhana kadhaa. Kwa mfano, uhuru kwa Mkristo unaweza kumaanisha kwamba yeye amewekwa huru kutoka kwa adhabu ya dhambi kwa imani katika yesu Kristo (Yohana 8:31-36; Warumi 6:23). Pia, uhuru wa Mkristo unaweza kurejelea kuwa huru kutoka kwa nguvu ya dhambi katika maisha ya mtu kwa imani ya kila siku katika Yesu Kristo kama Bwana wa tabia na mwenendo wa mtu (Warumi 6:5-6,14). Zaidi ya hayo, uhuru wa Kikristo unaweza kumaanisha kwamba Wakristo wamefunguliwa kutoka kwa Sheria ya Musa kwa kuwa Sheria “hufichua” dhambi katika maisha ya mtu lakini haiwezi “kusamehe” dhambi (Warumi 3:20-22).

Hatimaye, uhuru wa Kikristo unaweza maanisha kwamba Wakristo wako huru kuhusiana na utendaji kama huo ambao haujakatazwa wazawazi katika Biblia. Kwa hiyo mtu anaweza kujisikia huru kushiriki katika shughuli kama hiyo mradi tu “haimkwazi” au “kumchukiza” Mkristo mwingine (Warumi 14:12-16). Shughuli hizi nyingi hujikita katika yale “unapaswa kufanya” na yale “hupaswi kufanya” kama vile kuvaa au kutovaa aina fulani ya mavazi, kujipodoa, vito, mchoro, kutoboa au kufanya mambo fulani, kama vile uvutaji sigara, vileo vya hafla, kucheza kamari kwa burudani, au kutazama kanda. Kama vile kifungu cha Warumi 14 kinavyosema, mambo haya yanaweza yasiwe yamekatazwa kabisa na Neno la Mungu, lakini yanaweza kuwa mabaya kwa ukuaji wa kiroho wa mtu au ushuhuda wa Kikristo na yanaweza kusababisha Wakristo wengine kujikwaa.

Zaidi ya hayo, Wakristo wanaoonekana kuendeleza uhuru huo kwa nguvu wakati mwingine wanaweza kutumbukia katika maisha potovu yasiyo na nidhamu, huku, kwa upande mwingine, Wakristo ambao wanaojaribu kuweka mipaka uhuru kama huo kwa nguvu nyakati fulani wanaweza kutumbukia katika mtindo wa maisha ya kufuata sheria ya kutambulika kwa kile “wanachopinga.” Kwa hivyo, ni busara kumtafuta Mungu katika maombi na Neno lake ili kuamua kama shughuli fulani imekatazwa au kukataliwa katika Maandiko. Ikiwa ni hivyo, inapaswa kuepukwa. Ikiwa haijakatazwa, basi tunapaswa kutafuta kujua jinsi shughuli hiyo inavyoakisi sifa yetu kama Wakristo na kama itatusaidia au itatuzuia katika kumwakilisha Yesu kwa wasio Wakristo wanaotuzunguka, iwe inawajenga ua la.

Lengo kuu la Mkristo linapaswa kuwa kumtukuza Mungu, kuwajenga waumini wanzake, na kuwa na sifa nzuri mbele ya wasioamini (Zaburi 19:14; Warumi 15:1-2; 1 Petro 2: 11-12). “Ndugu zangu, ninyi mliitwa ili mwe huru, hivyo msitumie uhuru wenu kama fursa ya kufuata tamaa za mwili, bali tumikianeni ninyi kwa ninyi kwa upendo” (Wagalatia 5:13).

English



Rudi kwa ukurasa wa nyumbani wa Kiswahili

Uhuru wa Mkristo-Bibia inasema nini?
Shiriki ukurasa huu: Facebook icon Twitter icon Pinterest icon Email icon
© Copyright Got Questions Ministries