settings icon
share icon
Swali

Je, ni kwa nini Yesu anatuagiza tuombe ‘usitutie majaribuni’ wakati Mungu anaposema kwamba hatujaribu?

Jibu


Tunajua kutoka Yakobo 1:13 kwamba Mungu hatujaribu kufanya dhambi. Ikiwa Mungu angetujaribu kutenda dhambi, angekuwa anatenda kinyume na asili yake takatifu, kinyume na tamanio yake ya sisi kuwa watakatifu kama yeye alivyo mtakatifu (1 Petro 1:16) na kinyume na amri zingine zote katika Maandiko ambazo zinatuambia tuepuke majaribu. Katika maombi ya kielelezo ya Bwana (Mathayo 6:9-13), Yesu anasema, “Usitutie majaribuni, bali utuokoe kutoka kwa yule mwovu” (aya ya 13). Kujumuishwa kwa ombi la Mungu usitutie majaribuni inatufundisha kwamba kuepuka majaribu kunapaswa kuwa moja ya mambo ya msingi ya maisha ya Kikristo.

Dhana ya Mungu kuwaongoza watu wake ni mada kuu katika Maandiko. Kitabu cha Zaburi hasa kimejaa maombi ya kutaka Mungu atuongoze katika njia Zake (Zaburi 5:8; 27:11), kwa ukweli na uadilifu Wake, na katika “njia ya milele” Zaburi 139:24). Kando na kutuongoza kuelekea mema, tunaelewa kwamba tunamwomba Mungu atuongoze kutoka kwa uovu. Ombi katika Sala ya Bwana la kutoongozwa majaribuni linaonyesha hamu ya muumini ya kuepuka hatari za dhambi kabisa. Kisha maneno haya lazima yaeleweke katika maana ya “kuruhusu.” Yesu alitufunza kusali, “Usituruhusu, tujaribiwe kutenda dhambi.” Ombi hili linamaanisha kwamba Mungu ana mamlaka juu ya anayetujaribu, kiasi cha kutuokoa kutoka kwa nguvu zake ikiwa tunamwita Baba yetu wa Mbinguni.

Kunayo namna nyingine ambayo tunapaswa kumsihi Mungu asitutie katika majaribu. Neno kishawishi pia linaweza kurejelea majaribu. Tunajua kutoka 1 Wakorintho 10:13 kwamba Mungu hawezi kutujaribu kupita uwezo wetu katika Kristo kustahimili hilo na daima atatoa njia ya kutokea. Lakini wakati mwingine Mungu hutuachilia tunaingia majaribuni ambayo yanaweza kutuweka wazi kwa mashambulio ya Shetani kwa makusudi Yake mwenyewe, kama katika kisa cha Ayubu na Petro (Luka 22:31-32). Ikiwa kishawishi katika Sala ya Bwana kinarejelea majaribu, basi maana ya Mathayo 6:13 ni “Usitutie uchungu au kutujaribu.” Si makosa kuomba kuwa tuondolewe kutoka majaribuni na mateso, maadamu tunajisalimisha kwa mapenzi ya Mungu, haijalishi ni majaribu gani. Muumini anaweza kuomba aondolewe katika majaribu na vile vile aombe nguvu ya kustahimili hilo linapokuja.

Tunaweza eleza kwa mfano maneno ya Yesu “Usitutie majaribuni” hivi: mama anawachukua watoto wake wachanga mahali pa kununua mboga na wanafika sehemu ya peremende. Anajua kuwachukua watoto wake katika hiyo sehemu kutachochea uchoyo mioyoni mwao na kusababisha vipindi vya kunung’unika na kupiga kelele. Kwa hekima, anatumia njia nyingine-chochote ambacho huenda alihitaji karibu na sehemu ya peremende itamlazimu angoje siku nyingine. Kwa njia hii mama atahepuka kukasirika na kuwahepushia watoto wake majaribu. Kusali, “Usitutie katika majaribu,” na sawa na kusali, “Mungu, usiniongoze kwenye sehemu ya peremende leo.” Ni kutambua kwamba kwa kawaida tunashikilia mambo yasiyofaa na kwamba hekima ya Mungu inaweza kuzuia ubaya wa kutafuta kwetu jambo ambalo halitatunufaisha.

Iwe tunamwomba Mungu asitutie majaribuni au vishawishi vigumu, kusudi letu linapatikana katika sehemu ya pili ya aya ya 13: “Bali utuokoe kutoka kwa yule mwovu.” Ombi linalofanana na hili latolewa na Daudi katika Zaburi 141:4: “Usiuache moyo wangu uvutwe katika jambo baya, nisije nikashiriki katika matendo maovu pamoja na watu watendao mabaya, wala nisije nikala vyakula vyao vya anasa.” Katika mambo yote, Mungu ndiye mkombozi wetu, na sisi ni wenye hekima kutafuta uwezo wake juu ya dhambi.

English



Rudi kwa ukurasa wa nyumbani wa Kiswahili

Je, ni kwa nini Yesu anatuagiza tuombe ‘usitutie majaribuni’ wakati Mungu anaposema kwamba hatujaribu?
Shiriki ukurasa huu: Facebook icon Twitter icon Pinterest icon Email icon
© Copyright Got Questions Ministries