settings icon
share icon
Swali

Biblia inasema nini kuhusu kuombea wafu?

Jibu


Kusali kwa ajili ya wafu sio wazo la kibiblia. Maombi yetu hayana mwelekeo kwa mtu anapokufa. Ukweli ni kwamba, wakati wa kifo, hatima ya milele ya mtu imethibitishwa. Aidha anaokolewa kwa njia ya imani katika Kristo na yuko mbinguni ambako anapata mapumziko na furaha katika uwepo wa Mungu, au yuko katika maumivu katika Jahannamu. Hadithi ya mtu tajiri na Lazaro mwombaji hutupa mfano mzuri wa ukweli huu. Yesu alitumia hadithi hii kwa uwazi kuwafundisha kwamba baada ya kifo watu wasio na haki wanatenganishwa milele na Mungu, kwamba wanakumbuka wakikataa injili, wakiwa katika maumivu, na kwamba hali yao haiwezi kurekebishwa (Luka 16: 19-31).

Mara nyingi, watu ambao wamepoteza mpendwa wanahimizwa kuombea wale waliofariki na familia zao. Kwa kweli, tunapaswa kuombea wale wanaoomboleza, lakini kwa wafu, hapana. Hakuna mtu anayepaswa kuamini kwamba mtu anaweza kuomba kwa ajili yake, na hivyo atasababisha aina fulani ya matokeo mazuri, baada ya kufa. Biblia inafundisha kwamba hali ya milele ya wanadamu imedhamiriwa na matendo yetu wakati wa maisha yetu duniani. “Roho itendayo dhambi, ndiyo itakayokufa…., haki yake mwenye haki itakuwa juu yake, na uovu wake mwenye uovu utakuwa juu yake"(Ezekieli 18:20).

Mwandishi kwa Waebrania anatuambia, "Na kama vile watu wanavyowekewa kufa mara moja, na baada ya kufa hukumu" (Waebrania 9:27). Hapa tunaelewa kwamba hakuna mabadiliko katika hali ya kiroho ya mtu inaweza kufanywa baada ya kifo chake-ama yeye mwenyewe au kupitia juhudi za wengine. Ikiwa ni bure kuomba kwa ajili ya wanaoishi, ambao wanafanya "dhambi inayosababisha kifo" (1 Yohana 5:16), yaani, dhambi ya daima bila kutafuta msamaha wa Mungu, sala ya wale waliokufa itawafaidi aje, kwa kuwa hakuna mpango mwingine wa wokovu baada ya kifo?

Uhakika ni kwamba kila mmoja wetu ana maisha moja tu, na niwajibu wetu jinsi tunavyoishi maisha hayo. Wengine wanaweza kuathiri uchaguzi wetu, lakini hatimaye tunapaswa kutoa akaunti kwa uchaguzi tunaofanya. Mara baada ya uzima, hakuna uchaguzi zaidi unaofanywa; hatuna chaguo bali tukabiliana na hukumu. Sala za wengine zinaweza kutoa tamaa zao, lakini hazibadili matokeo. Wakati wa kumwombea mtu ni akiwa bado hai, anaishi na bado kuna uwezekano wa moyo wake, mitazamo, na tabia yake kubadilishwa (Warumi 2: 3-9).

Ni kawaida kuwa na hamu ya kuomba wakati wa maumivu, mateso, na kupoteza wapendwa na marafiki, lakini tunajua mipaka ya sala ya halali kama ilivyofunuliwa katika Biblia. Biblia ndio kitabu pekee cha maombi, na inafundisha kwamba sala kwa ajili ya wafu ni bure. Hata hivyo tunaona mazoezi ya kuombea wafu waliotajwa katika maeneo fulani ya "Kanisa la Kikristo." Kwa mfano, teolojia ya Kikatoliki ya Kirumi inaruhusu sala kwa wafu na kwa niaba yao. Lakini hata mamlaka ya Katoliki wanakiri kuwa hakuna idhini ya wazi ya sala kwa niaba ya wafu katika vitabu sitini na sita vya Maandiko ya kisheria. Badala yake, wanakataa Apokirifa (2 Makababe 12:46), mila ya kanisa, amri ya Baraza la Trent, nakadhalika, ili kulinda mazoezi.

Biblia inafundisha kwamba wale ambao wamejitoa kwa mapenzi ya Mwokozi (Waebrania 5:8-9) huingia moja kwa moja na mara moja mbele ya Bwana baada ya kufa (Luka 23:43; Wafilipi 1:23; 2 Wakorintho 5: 6, 8). Kwa nini wanahitaji maombi ya watu walio duniani? Tunapokuwa na huruma na wale ambao wamepoteza wapendwa, tunapaswa kukumbuka ya kwamba "tazama,wakati uliokubalika ndiyo sasa; tazama siku ya wokovu ni sasa" (2 Wakorintho 6: 2). Wakati muktadha unarejelea umri wa injili kwa ujumla, huu mstari unafaa kwa mtu yeyote asiyejiandaa kukabiliana na kifo cha kuepukika na hukumu inayofuata (Warumi 5:12, 1 Wakorintho 15:26; Waebrania 9:27). Kifo ni mwisho, na baada ya hapo, hakuna kiasi cha kuomba kitatumia mtu wa wokovu aliyekataliwa katika maisha.

English



Rudi kwa ukurasa wa nyumbani wa Kiswahili

Biblia inasema nini kuhusu kuombea wafu?
Shiriki ukurasa huu: Facebook icon Twitter icon Pinterest icon Email icon
© Copyright Got Questions Ministries